< Hagai 2 >
1 Katika siku ya ishirini na moja ya mwezi wa saba, neno la Bwana lilikuja kupitia nabii Hagai, kusema:
In the seventh month, in the twenty-first day of the month, the word of Jehovah came by Haggai the prophet, saying,
2 “Sema na Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda, kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki, na mabaki ya watu. Uwaulize,
Speak now to Zerubbabel the son of Shealtiel, governor of Judah, and to Joshua the son of Jehozadak, the high priest, and to the remnant of the people, saying,
3 ‘Ni nani miongoni mwenu aliyebaki ambaye aliiona hii nyumba katika utukufu wake wa mwanzo? Sasa inaonekanaje kwenu? Je, haionekani kwenu kama si kitu?
Who is left among you that saw this house in its former glory? And how do ye see it now? Is it not in your eyes as nothing?
4 Lakini sasa uwe imara, ee Zerubabeli,’ asema Bwana. ‘Kuwa imara, ee kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki. Mwe imara, enyi watu wote wa nchi,’ asema Bwana, ‘na mfanye kazi. Kwa kuwa mimi nipo pamoja nanyi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Yet now be strong, O Zerubbabel, says Jehovah, and be strong, O Joshua, son of Jehozadak, the high priest, and be strong, all ye people of the land, says Jehovah, and work. For I am with you, says Jehovah of hosts,
5 ‘Hili ndilo nililoagana nanyi mlipotoka katika nchi ya Misri. Pia Roho wangu anadumu katikati yenu. Msiogope.’
according to the word that I covenanted with you when ye came out of Egypt, and my Spirit abode among you. Fear ye not.
6 “Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Baada ya muda kidogo kwa mara nyingine nitazitikisa mbingu na nchi, bahari na nchi kavu.
For thus says Jehovah of hosts: Yet once, it is a little while, and I will shake the heavens, and the earth, and the sea, and the dry land.
7 Nitatikisa mataifa yote, nacho kile kinachotamaniwa na mataifa yote kitakuja, nami nitaujaza utukufu katika nyumba hii,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
And I will shake all nations, and the precious things of all nations shall come, and I will fill this house with glory, says Jehovah of hosts.
8 ‘Fedha ni mali yangu na dhahabu ni mali yangu,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
The silver is mine, and the gold is mine, says Jehovah of hosts.
9 ‘Utukufu wa nyumba hii ya sasa utakuwa mkubwa kuliko utukufu wa ile nyumba ya mwanzoni,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. ‘Na mahali hapa nitawapa amani,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.”
The latter glory of this house shall be greater than the former, says Jehovah of hosts, and in this place I will give peace, says Jehovah of hosts.
10 Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa tisa, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilikuja kwa nabii Hagai:
In the twenty-fourth day of the ninth month, in the second year of Darius, the word of Jehovah came by Haggai the prophet, saying,
11 “Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Ulizeni makuhani jinsi sheria inavyosema:
Thus says Jehovah of hosts: Ask now the priests concerning the law, saying,
12 Kama mtu akibeba nyama iliyowekwa wakfu katika pindo la vazi lake, kisha lile pindo likagusa mkate au mchuzi, divai, mafuta au chakula kingine, je, kitu hicho kitakuwa kimewekwa wakfu?’” Makuhani wakajibu, “La hasha.”
If a man bears holy flesh in the skirt of his garment, and with his skirt touches bread, or pottage, or wine, or oil, or any food, shall it become holy? And the priests answered and said, No.
13 Kisha Hagai akasema, “Je, kama mtu aliyetiwa unajisi kwa kugusa maiti akigusa mojawapo ya vitu hivi, kitu hicho kitakuwa kimetiwa unajisi?” Makuhani wakajibu, “Ndiyo, huwa kimenajisiwa.”
Then Haggai said, If a man who is unclean because of a dead body touches any of these, shall it be unclean? And the priests answered and said, It shall be unclean.
14 Kisha Hagai akasema, “‘Basi ndivyo walivyo machoni pangu hawa watu na taifa hili,’ asema Bwana. ‘Lolote wafanyalo na chochote watoacho hapo ni najisi.
Then Haggai answered and said, So is this people, and so is this nation before me, says Jehovah, and so is every work of their hands. And that which they offer there is unclean.
15 “‘Sasa fikirini kwa uangalifu kuanzia leo na kuendelea: tafakarini jinsi mambo yalivyokuwa kabla halijawekwa jiwe moja juu ya lingine katika Hekalu la Bwana.
And now, I pray you, consider from this day and backward, before a stone was laid upon a stone in the temple of Jehovah.
16 Wakati mtu alipoendea lundo la nafaka la vipimo ishirini, kulikuwa na vipimo kumi tu. Wakati mtu alipoendea pipa la mvinyo ili kuchota vipimo hamsini, kulikuwa na vipimo ishirini tu.
Through all that time, when a man came to a heap of twenty measures, there were but ten. When he came to the wine vat to draw out fifty vessels, there were but twenty.
17 Kazi zenu zote za mikono nilizipiga kwa ukame, ukungu na mvua ya mawe, lakini hata hivyo, hamkunigeukia mimi,’ asema Bwana.
I smote you with blasting and with mildew and with hail in all the work of your hands, yet ye turned not to me, says Jehovah.
18 ‘Tangu leo na kuendelea, kuanzia siku hii ya ishirini na nne ya mwezi wa tisa, tafakarini siku ambayo msingi wa Hekalu la Bwana uliwekwa. Tafakarini:
Consider, I pray you, from this day and backward, from the twenty-fourth day of the ninth month, since the day that the foundation of Jehovah's temple was laid, consider it.
19 Je, bado kuna mbegu iliyobakia ghalani? Mpaka sasa, hakuna mzabibu au mtini, mkomamanga wala mzeituni uliozaa tunda. “‘Kuanzia leo na kuendelea, nitawabariki.’”
Is the seed yet in the barn? Yea, the vine, and the fig tree, and the pomegranate, and the olive tree have not brought forth. From this day I will bless you.
20 Neno la Bwana likamjia Hagai kwa mara ya pili katika siku ya ishirini na nne ya mwezi kusema:
And the word of Jehovah came the second time to Haggai in the twenty-fourth day of the month, saying,
21 “Mwambie Zerubabeli mtawala wa Yuda kwamba nitazitikisa mbingu na nchi.
Speak to Zerubbabel, governor of Judah, saying, I will shake the heavens and the earth.
22 Nitapindua viti vya enzi vya falme, na kuziharibu kabisa nguvu za falme za kigeni. Nitapindua magari ya vita pamoja na waendeshaji wake; farasi na wapanda farasi wataanguka, kila mmoja kwa upanga wa ndugu yake.
And I will overthrow the throne of kingdoms, and I will destroy the strength of the kingdoms of the nations. And I will overthrow the chariots, and those who ride in them. And the horses and their riders shall come down, each one by the sword of his brother.
23 “‘Katika siku ile,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nitakuchukua wewe, mtumishi wangu Zerubabeli mwana wa Shealtieli,’ asema Bwana. ‘Nitakufanya kama pete yangu ya muhuri, kwa kuwa nimekuchagua,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.”
In that day, says Jehovah of hosts, I will take thee, O Zerubbabel, my servant, the son of Shealtiel, says Jehovah, and will make thee as a signet. For I have chosen thee, says Jehovah of hosts.