< Hagai 1 >
1 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario wa Uajemi, katika siku ya kwanza ya mwezi wa sita, neno la Bwana lilikuja kupitia kwa nabii Hagai kwenda kwa Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda na kwa Yoshua mwana wa kuhani mkuu Yehosadaki:
Ķēniņa Dārija otrā gadā, sestā mēnesi, pirmā mēneša dienā, Tā Kunga vārds notika caur pravieti Hagaju uz Zerubabeli Šealtiēļa dēlu, Jūda valdnieku, un uz Jozua, Jocadaka dēlu, augsto priesteri, un sacīja:
2 Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Hawa watu husema, ‘Wakati haujawadia wa kujenga nyumba ya Bwana.’”
Tā runā Tas Kungs Cebaot un saka: šie ļaudis runā: laiks vēl nav nācis, uzcelt Tā Kunga namu.
3 Kisha neno la Bwana likaja kupitia kwa nabii Hagai:
Un Tā Kunga vārds notika caur pravieti Hagaju sacīdams:
4 “Je, ni wakati wenu ninyi wa kuishi katika nyumba zenu zilizojengwa vizuri, wakati hii nyumba ikibaki, gofu?”
Vai tad jums ir laiks, dzīvot glītos namos un šim namam būs stāvēt postā?
5 Sasa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Zitafakarini vyema njia zenu.
Nu tad tā saka Tas Kungs Cebaot: ņemat vērā savus ceļus.
6 Mmepanda vingi, lakini mmevuna haba. Mnakula lakini hamshibi, mnakunywa, lakini hamtosheki. Mnavaa nguo, lakini hamsikii joto. Mnapata mishahara, lakini inatoweka kama imewekwa kwenye mfuko uliotobokatoboka.”
Jūs sējat daudz un pļaujat maz, jūs ēdat, bet nepaēdat, jūs dzerat bet nepadzerat, jūs ģērbjaties, bet jums nepaliek silti, un algādzis pelna algu cauram makam.
7 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Zitafakarini vyema njia zenu.
Tā saka Tas Kungs Cebaot: liekat vērā savus ceļus.
8 Pandeni milimani mkalete miti na kujenga nyumba, ili nipate kuifurahia, na nitukuzwe,” asema Bwana.
Ejat augšā kalnos un vediet kokus un uztaisiet šo namu; pie tā Man būs labs prāts, un Es tapšu pagodināts, saka Tas Kungs.
9 “Mlitarajia mengi, kumbe, yametokea kidogo. Ulichokileta nyumbani nilikipeperusha. Kwa nini?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Ni kwa sababu ya nyumba yangu, inayobaki katika hali ya magofu, wakati kila mmoja wenu anajishughulisha na nyumba yake mwenyewe.
Jūs gan gaidāt uz daudz, bet redzi, jūs dabūjat maz, un jebšu jūs to esat mājās pārnesuši, taču Es to izputināju. Kāpēc tā? saka Tas Kungs Cebaot. Mana nama labad, kas stāv postā, kamēr ikviens skrien sava nama labad.
10 Kwa hiyo, kwa sababu yenu mbingu zimezuia umande wake na ardhi mavuno yake.
Tādēļ debess jums aiztur rasu, un zeme aiztur savus augļus.
11 Niliita ukame mashambani na milimani, kwenye nafaka, mvinyo mpya, mafuta pamoja na chochote kinachozalishwa na ardhi, juu ya watu na ngʼombe, pamoja na kazi za mikono yenu.”
Un sausumu Es saucu(sūtu) pār zemi un pār kalniem un pār labību un pār vīnu un pār eļļu un pār visu, kas izaug no zemes, un pār cilvēkiem un pār lopiem un pār ikvienu rokas darbu.
12 Kisha Zerubabeli mwana wa Shealtieli, Yoshua kuhani mkuu mwana wa Yehosadaki, pamoja na mabaki yote ya watu wakaitii sauti ya Bwana Mungu wao pamoja na ujumbe wa nabii Hagai, kwa sababu alikuwa ametumwa na Bwana Mungu wao. Watu walimwogopa Bwana.
Tad Zerubabels, Šealtiēļa dēls, un Jozuas, Jocadaka dēls, augstais priesteris, un visi atlikušie ļaudis klausīja Tā Kunga, sava Dieva, balsij un pravieša Hagaja vārdiem it(tieši) kā Tas Kungs, viņu Dievs, to bija sūtījis, un tie ļaudis bijās no Tā Kunga.
13 Kisha Hagai, mjumbe wa Bwana, akawapa watu ujumbe huu wa Bwana: “Mimi niko pamoja nanyi,” asema Bwana.
Tad sacīja Hagaja, Tā Kunga vēstnesis, kam Tā Kunga vēsts bija uz tiem ļaudīm: Es esmu ar jums, saka Tas Kungs.
14 Kwa hiyo Bwana akachochea roho ya Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda, na roho ya kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki, pamoja na roho za mabaki yote ya watu. Walikuja wakaanza kufanya kazi katika nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wao,
Un Tas Kungs pamodināja Zerubabela, Šealtiēļa dēla, Jūdas ķēniņa garu un Jozuas, Jocadaka dēla, augstā priestera garu un visu atlikušo ļaužu garu, ka tie gāja un darīja darbu pie Tā Kunga Cebaot, sava Dieva, nama,
15 katika siku ya ishirini na nne mwezi wa sita, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario.
Sestā mēneša divdesmit ceturtā dienā ķēniņa Dārija otrā gadā.