< Hagai 1 >

1 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario wa Uajemi, katika siku ya kwanza ya mwezi wa sita, neno la Bwana lilikuja kupitia kwa nabii Hagai kwenda kwa Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda na kwa Yoshua mwana wa kuhani mkuu Yehosadaki:
La seconde année du roi Darius, le sixième mois, le premier jour du mois, la parole de l'Éternel fut adressée par Aggée, le prophète, à Zorobabel, fils de Salathiel, gouverneur de Juda, et à Josué, fils de Jéhotsadak, grand sacrificateur, en ces mots:
2 Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Hawa watu husema, ‘Wakati haujawadia wa kujenga nyumba ya Bwana.’”
Ainsi parle l'Éternel des armées: Ce peuple dit: Le moment n'est pas encore venu, le moment où la maison de l'Éternel doit être rebâtie.
3 Kisha neno la Bwana likaja kupitia kwa nabii Hagai:
C'est pourquoi la parole de l'Éternel fut adressée par Aggée, le prophète, en ces mots:
4 “Je, ni wakati wenu ninyi wa kuishi katika nyumba zenu zilizojengwa vizuri, wakati hii nyumba ikibaki, gofu?”
Est-ce le moment pour vous-mêmes de vous loger dans vos maisons lambrissées, tandis que cette maison est en ruine?
5 Sasa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Zitafakarini vyema njia zenu.
Or ainsi parle l'Éternel des armées: Soyez attentifs à la voie où vous êtes!
6 Mmepanda vingi, lakini mmevuna haba. Mnakula lakini hamshibi, mnakunywa, lakini hamtosheki. Mnavaa nguo, lakini hamsikii joto. Mnapata mishahara, lakini inatoweka kama imewekwa kwenye mfuko uliotobokatoboka.”
Vous semez beaucoup et récoltez peu, vous mangez, mais non pas jusqu'à rassasiement, vous buvez, mais non pas votre soûl; vous avez des habits, mais non jusqu'à avoir chaud, et celui qui sert pour un gage, met ses gains dans une bourse trouée.
7 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Zitafakarini vyema njia zenu.
Ainsi parle l'Éternel des armées: Soyez attentifs à la voie où vous êtes!
8 Pandeni milimani mkalete miti na kujenga nyumba, ili nipate kuifurahia, na nitukuzwe,” asema Bwana.
Montez à la montagne et en amenez du bois, et bâtissez la maison, afin que j'en aie du plaisir et que gloire me soit rendue, dit l'Éternel.
9 “Mlitarajia mengi, kumbe, yametokea kidogo. Ulichokileta nyumbani nilikipeperusha. Kwa nini?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Ni kwa sababu ya nyumba yangu, inayobaki katika hali ya magofu, wakati kila mmoja wenu anajishughulisha na nyumba yake mwenyewe.
Vous comptiez sur beaucoup, et voici, vous avez peu; et si vous l'amenez à la maison, je le dissipe. Pourquoi? dit l'Éternel des armées. A cause de ma maison qui est en ruine, tandis que vous êtes empressés chacun pour sa maison.
10 Kwa hiyo, kwa sababu yenu mbingu zimezuia umande wake na ardhi mavuno yake.
C'est pourquoi au-dessus de vous les Cieux retiennent la rosée, et la terre retient son produit;
11 Niliita ukame mashambani na milimani, kwenye nafaka, mvinyo mpya, mafuta pamoja na chochote kinachozalishwa na ardhi, juu ya watu na ngʼombe, pamoja na kazi za mikono yenu.”
et j'ai appelé la sécheresse sur le pays et sur les montagnes, et sur le blé, et sur le moût, et sur l'huile, et sur tout ce que produit le sol, et sur l'homme, et sur le bétail, et sur tout le travail des mains.
12 Kisha Zerubabeli mwana wa Shealtieli, Yoshua kuhani mkuu mwana wa Yehosadaki, pamoja na mabaki yote ya watu wakaitii sauti ya Bwana Mungu wao pamoja na ujumbe wa nabii Hagai, kwa sababu alikuwa ametumwa na Bwana Mungu wao. Watu walimwogopa Bwana.
Et Zorobabel, fils de Salathiel, et Josué, fils de Jéhotsadak, grand sacrificateur, et tous les restes du peuple furent dociles à la voix de l'Éternel, leur Dieu, et aux paroles d'Aggée, le prophète, parce que l'Éternel, leur Dieu, l'avait envoyé, et le peuple eut crainte de l'Éternel.
13 Kisha Hagai, mjumbe wa Bwana, akawapa watu ujumbe huu wa Bwana: “Mimi niko pamoja nanyi,” asema Bwana.
Et Aggée, envoyé de l'Éternel, parla en vertu de la mission de l'Éternel au peuple en ces mots: Je suis avec vous, dit l'Éternel.
14 Kwa hiyo Bwana akachochea roho ya Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda, na roho ya kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki, pamoja na roho za mabaki yote ya watu. Walikuja wakaanza kufanya kazi katika nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wao,
Et l'Éternel donna l'éveil à l'esprit de Zorobabel, fils de Salathiel, gouverneur de Juda, et à l'esprit de Josué, fils de Jéhotsadak, grand sacrificateur, et à l'esprit de tous les restes du peuple, et ils vinrent et se mirent à l'œuvre dans la maison de l'Éternel des armées, leur Dieu,
15 katika siku ya ishirini na nne mwezi wa sita, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario.
le vingt-quatrième jour du sixième mois, la seconde année du roi Darius.

< Hagai 1 >