< Habakuki 1 >
1 Neno alilopokea nabii Habakuki.
THE BURDEN which Habakkuk the prophet did see.
2 Ee Bwana, hata lini nitakuomba msaada, lakini wewe husikilizi? Au kukulilia, “Udhalimu!” Lakini hutaki kuokoa?
How long, O LORD, shall I cry, and Thou wilt not hear? I cry out unto Thee of violence, and Thou wilt not save.
3 Kwa nini unanifanya nitazame dhuluma? Kwa nini unavumilia makosa? Uharibifu na udhalimu viko mbele yangu; kuna mabishano na mapambano kwa wingi.
Why dost Thou show me iniquity, and beholdest mischief? And why are spoiling and violence before me? so that there is strife, and contention ariseth.
4 Kwa hiyo sheria imepotoshwa, nayo haki haipo kabisa. Waovu wanawazunguka wenye haki, kwa hiyo haki imepotoshwa.
Therefore the law is slacked, and right doth never go forth; for the wicked doth beset the righteous; therefore right goeth forth perverted.
5 “Yatazame mataifa, uangalie na ushangae kabisa. Kwa sababu katika siku zako nitafanya kitu ambacho hungeamini, hata kama ungeambiwa.
Look ye among the nations, and behold, and wonder marvellously; for, behold, a work shall be wrought in your days, which ye will not believe though it be told you.
6 Nitawainua Wakaldayo, watu hao wakatili na wenye haraka, ambao hupita dunia yote kuteka mahali pa kuishi pasipo pao wenyewe.
For, lo, I raise up the Chaldeans, that bitter and impetuous nation, that march through the breadth of the earth, to possess dwelling-places that are not theirs.
7 Ni watu wanoogopwa na wanaotisha; wenyewe ndio sheria yao, na huinua heshima yao wenyewe.
They are terrible and dreadful; their law and their majesty proceed from themselves.
8 Farasi wao ni wepesi kuliko chui, na wakali kuliko mbwa mwitu wakati wa machweo. Askari wapanda farasi wao huenda mbio; waendesha farasi wao wanatoka mbali. Wanaruka kasi kama tai ili kurarua;
Their horses also are swifter than leopards, and are more fierce than the wolves of the desert; and their horsemen spread themselves; yea, their horsemen come from far, they fly as a vulture that hasteth to devour.
9 wote wanakuja tayari kwa fujo. Makundi yao ya wajeuri yanasonga mbele kama upepo wa jangwani, na kukusanya wafungwa kama mchanga.
They come all of them for violence; their faces are set eagerly as the east wind; and they gather captives as the sand.
10 Wanawabeza wafalme, na kuwadhihaki watawala. Wanaicheka miji yote iliyozungushiwa maboma; wanafanya malundo ya udongo na kuiteka hiyo miji.
And they scoff at kings, and princes are a derision unto them; they deride every stronghold, for they heap up earth, and take it.
11 Kisha wanapita kasi kama upepo na kusonga mbele: watu wenye hatia, ambao nguvu zao ndio mungu wao.”
Then their spirit doth pass over and transgress, and they become guilty: even they who impute their might unto their god.
12 Ee Bwana, je, wewe sio wa tangu milele? Mungu wangu, Uliye Mtakatifu wangu, hatutakufa. Ee Bwana, umewachagua wao ili watekeleze hukumu; Ee Mwamba, umewaamuru watuadhibu.
Art not Thou from everlasting, O LORD my God, my Holy One? We shall not die. O LORD, Thou hast ordained them for judgment, and Thou, O Rock, hast established them for correction.
13 Macho yako ni safi mno hata yasiweze kuutazama uovu, wala huwezi kuvumilia makosa. Kwa nini basi unawavumilia wadanganyifu? Kwa nini unakuwa kimya wakati waovu wanawameza wale wenye haki kuliko wao wenyewe?
Thou that art of eyes too pure to behold evil, and that canst not look on mischief, wherefore lookest Thou, when they deal treacherously, and holdest Thy peace, when the wicked swalloweth up the man that is more righteous than he;
14 Umewafanya watu kama samaki baharini, kama viumbe wa bahari wasio na mtawala.
And makest men as the fishes of the sea, as the creeping things, that have no ruler over them?
15 Adui mwovu anawavuta wote kwa ndoana, anawakamata katika wavu wake, anawakusanya katika juya lake; kwa hiyo anashangilia na anafurahi.
They take up all of them with the angle, they catch them in their net, and gather them in their drag; therefore they rejoice and exult.
16 Kwa hiyo anatoa kafara kwa wavu wake, na kuchoma uvumba kwa juya lake, kwa kuwa kwa wavu wake anaishi kwa starehe, na anafurahia chakula kizuri.
Therefore they sacrifice unto their net, and offer unto their drag; because by them their portion is fat, and their food plenteous.
17 Je, aendelee kuwatoa walio katika wavu wake, akiangamiza mataifa bila huruma?
Shall they therefore empty their net, and not spare to slay the nations continually?