< Habakuki 3 >

1 Sala ya nabii Habakuki iliyoimbwa kwa shigionothi.
Una oración del profeta Habacuc, con música victoriosa.
2 Bwana, nimezisikia sifa zako; nami naogopa kwa matendo yako, Ee Bwana. Fufua kazi yako katikati ya miaka, katikati ya miaka tangaza habari yako; katika ghadhabu kumbuka rehema.
Yahvé, he oído hablar de tu fama. Me asombro de tus actos, Yahvé. Renueva tu trabajo en la medio de los años. En medio de los años hazlo saber. En la ira, te acuerdas de la misericordia.
3 Mungu alitoka Temani, yeye Aliye Mtakatifu kutoka Mlima Parani. Utukufu wake ulifunika mbingu, na sifa zake zikaifunika dunia.
Dios vino de Temán, el Santo del Monte Parán. (Selah) Su gloria cubrió los cielos, y su alabanza llenó la tierra.
4 Mngʼao wake ulikuwa kama jua lichomozalo; mionzi ilimulika kutoka mkononi mwake, ambako nguvu zake zilifichwa.
Su esplendor es como la salida del sol. Los rayos brillan desde su mano, donde se esconde su poder.
5 Tauni ilimtangulia; maradhi ya kuambukiza yalifuata nyayo zake.
La peste iba delante de él, y la pestilencia seguía sus pies.
6 Alisimama, akaitikisa dunia; alitazama, na kuyafanya mataifa yatetemeke. Milima ya zamani iligeuka mavumbi na vilima vilivyozeeka vikaanguka. Njia zake ni za milele.
Se puso de pie y sacudió la tierra. Miró, e hizo temblar a las naciones. Las antiguas montañas se desmoronaron. Las colinas milenarias se derrumbaron. Sus caminos son eternos.
7 Niliona watu wa Kushani katika dhiki, na makazi ya Midiani katika maumivu makali.
Vi las tiendas de Cusán afligidas. Las viviendas de la tierra de Madián temblaban.
8 Ee Bwana, uliikasirikia mito? Je, ghadhabu yako ilikuwa dhidi ya vijito? Je, ulighadhibikia bahari ulipoendesha farasi wako na magari yako ya ushindi?
¿Se disgustó Yahvé con los ríos? ¿Fue su ira contra los ríos, o tu ira contra el mar, que montasteis en vuestros caballos, en sus carros de salvación?
9 Uliufunua upinde wako na kuita mishale mingi. Uliigawa dunia kwa mito;
Descubriste tu arco. Llamaste a tus flechas juradas. (Selah) Divides la tierra con ríos.
10 milima ilikuona ikatetemeka. Mafuriko ya maji yakapita huko; vilindi vilinguruma na kuinua mawimbi yake juu.
Las montañas te vieron y tuvieron miedo. La tormenta de aguas pasó de largo. Las profundidades rugieron y levantaron sus manos en lo alto.
11 Jua na mwezi vilisimama kimya mbinguni katika mngʼao wa mishale yako inayoruka, na katika mngʼao wa mkuki wako umeremetao.
El sol y la luna se detuvieron en el cielo a la luz de sus flechas cuando pasaron, ante el brillo de tu reluciente lanza.
12 Kwa ghadhabu ulipita juu ya dunia, na katika hasira ulikanyaga mataifa.
Marchaste por la tierra con ira. Trillaste a las naciones con ira.
13 Ulikuja kuwaokoa watu wako, kumwokoa uliyemtia mafuta. Ulimponda kiongozi wa nchi ya uovu, ukamvua toka kichwani hadi wayo.
Saliste por la salvación de tu pueblo, para la salvación de tu ungido. Aplastaste la cabeza de la tierra de la maldad. Los desnudaste de pies a cabeza. (Selah)
14 Kwa mkuki wake mwenyewe ulitoboa kichwa chake wakati mashujaa wake walifurika nje kwa kishindo kututawanya, wakifurahi kama walio karibu kutafuna wale wanyonge waliokuwa mafichoni.
Atravesaste las cabezas de sus guerreros con sus propias lanzas. Vinieron como un torbellino a dispersarme, regodeándose como si fuera a devorar a los desdichados en secreto.
15 Ulikanyaga bahari kwa farasi wako, ukisukasuka maji makuu.
Has pisoteado el mar con tus caballos, agitando las poderosas aguas.
16 Nilisikia na moyo wangu ukagonga kwa nguvu, midomo yangu ikatetemeka kwa hofu niliposikia sauti; uchakavu ukanyemelea mifupa yangu, na miguu yangu ikatetemeka. Hata hivyo nitasubiri kwa uvumilivu siku ya maafa kuyajilia mataifa yaliyotuvamia.
Lo oí, y mi cuerpo se estremeció. Mis labios temblaron al oír la voz. La podredumbre entra en mis huesos, y tiemblo en mi lugar porque debo esperar tranquilamente el día de la angustia, por la llegada de la gente que nos invade.
17 Ingawa mtini hauchanui maua na hakuna zabibu juu ya mizabibu, ingawaje mzeituni hauzai, na hata mashamba hayatoi chakula, iwapo hakuna kondoo katika banda, wala ngʼombe katika zizi,
Porque aunque la higuera no florezca ni haya frutos en las viñas, el trabajo de la aceituna falle, y los campos no den comida, los rebaños sean quitados del redil, y no haya manadas en los establos,
18 hata hivyo nitashangilia katika Bwana, nitamfurahia Mungu Mwokozi wangu.
aún me regocijaré en Yahvé. Estaré alegre en el Dios de mi salvación.
19 Bwana Mwenyezi ni nguvu yangu; huifanya miguu yangu kama miguu ya ayala, huniwezesha kupita juu ya vilima. Kwa kiongozi wa uimbaji. Kwa vinanda vyangu vya nyuzi.
Yahvé, el Señor, es mi fuerza. Hace mis pies como pies de ciervo, y me permite ir a lugares altos. Para el director de música, en mis instrumentos de cuerda.

< Habakuki 3 >