< Habakuki 3 >

1 Sala ya nabii Habakuki iliyoimbwa kwa shigionothi.
Molitev preroka Habakúka na Šiginot.
2 Bwana, nimezisikia sifa zako; nami naogopa kwa matendo yako, Ee Bwana. Fufua kazi yako katikati ya miaka, katikati ya miaka tangaza habari yako; katika ghadhabu kumbuka rehema.
Oh Gospod, slišal sem tvoj govor in bil sem prestrašen. Oh Gospod, oživi svoje delo v sredi let, v sredi let ga daj spoznati, v besu se spomni usmiljenja.
3 Mungu alitoka Temani, yeye Aliye Mtakatifu kutoka Mlima Parani. Utukufu wake ulifunika mbingu, na sifa zake zikaifunika dunia.
Bog je prišel iz Temána in Sveti z gore Parán. (Sela) Njegova slava je pokrila nebo in zemlja je bila polna njegove hvale.
4 Mngʼao wake ulikuwa kama jua lichomozalo; mionzi ilimulika kutoka mkononi mwake, ambako nguvu zake zilifichwa.
Njegov sijaj je bil kakor svetloba; imel je rogove, izhajajoče iz njegove roke in tam je bilo skrivališče njegove moči.
5 Tauni ilimtangulia; maradhi ya kuambukiza yalifuata nyayo zake.
Pred njim je odšla kužna bolezen in goreče oglje je šlo naprej ob njegovih stopalih.
6 Alisimama, akaitikisa dunia; alitazama, na kuyafanya mataifa yatetemeke. Milima ya zamani iligeuka mavumbi na vilima vilivyozeeka vikaanguka. Njia zake ni za milele.
Stal je in izmeril zemljo. Pogledal je in razgnal narode in večne gore so bile razkropljene, starodavni hribi so se upognili. Njegove poti so večne.
7 Niliona watu wa Kushani katika dhiki, na makazi ya Midiani katika maumivu makali.
Videl sem kušánske šotore v stiski in zavese midjánske dežele so trepetale.
8 Ee Bwana, uliikasirikia mito? Je, ghadhabu yako ilikuwa dhidi ya vijito? Je, ulighadhibikia bahari ulipoendesha farasi wako na magari yako ya ushindi?
Mar je bil Gospod nezadovoljen zoper reke? Je bila tvoja jeza zoper reke? Je bil tvoj bes zoper morje, da si jahal na svojih konjih in svojih bojnih vozovih rešitve duš?
9 Uliufunua upinde wako na kuita mishale mingi. Uliigawa dunia kwa mito;
Tvoj lok je bil razgaljen, glede na prisege rodov, celo tvojo besedo. (Sela) Zemljo si oklenil z rekami.
10 milima ilikuona ikatetemeka. Mafuriko ya maji yakapita huko; vilindi vilinguruma na kuinua mawimbi yake juu.
Gore so te videle in so trepetale, preplavljanje vodá je šlo mimo, globina je izustila svoj glas in svoje roke vzdignila na visoko.
11 Jua na mwezi vilisimama kimya mbinguni katika mngʼao wa mishale yako inayoruka, na katika mngʼao wa mkuki wako umeremetao.
Sonce in luna sta mirno stala v svojem prebivališču. Ob svetlobi tvojih puščic sta šla in ob siju tvoje lesketajoče sulice.
12 Kwa ghadhabu ulipita juu ya dunia, na katika hasira ulikanyaga mataifa.
V ogorčenju si korakal skozi deželo, pogane si mlatil v jezi.
13 Ulikuja kuwaokoa watu wako, kumwokoa uliyemtia mafuta. Ulimponda kiongozi wa nchi ya uovu, ukamvua toka kichwani hadi wayo.
Šel si naprej zaradi rešitve duš svojega ljudstva, celó zaradi rešitve duš s svojim maziljenim. Ti raniš poglavarja hiše zlobnih z razkritjem temelja do vratu. (Sela)
14 Kwa mkuki wake mwenyewe ulitoboa kichwa chake wakati mashujaa wake walifurika nje kwa kishindo kututawanya, wakifurahi kama walio karibu kutafuna wale wanyonge waliokuwa mafichoni.
Z njegovimi kopji si prebodel poglavarja njegovih vasi. Ven so prišli kakor vrtinčast veter, da me razkropijo. Njihovo razveseljevanje je bilo kakor, da bi na skrivaj požrli ubogega.
15 Ulikanyaga bahari kwa farasi wako, ukisukasuka maji makuu.
Skozi morje si hodil s svojimi konji, skozi kup velikih vodá.
16 Nilisikia na moyo wangu ukagonga kwa nguvu, midomo yangu ikatetemeka kwa hofu niliposikia sauti; uchakavu ukanyemelea mifupa yangu, na miguu yangu ikatetemeka. Hata hivyo nitasubiri kwa uvumilivu siku ya maafa kuyajilia mataifa yaliyotuvamia.
Ko sem slišal, je moj trebuh trepetal, moje ustnice so drgetale ob glasu. Gniloba je vstopila v moje kosti in v sebi sem trepetal, da bi lahko počival na dan stiske. Ko prihaja gor k ljudstvu, jih bo preplavil s svojimi krdeli.
17 Ingawa mtini hauchanui maua na hakuna zabibu juu ya mizabibu, ingawaje mzeituni hauzai, na hata mashamba hayatoi chakula, iwapo hakuna kondoo katika banda, wala ngʼombe katika zizi,
Čeprav figovo drevo ne bo cvetelo niti ne bo sadu na trtah, [čeprav] bo trud oljke odpovedal in polja ne bodo obrodila nobene hrane; [čeprav] bo trop odrezan od staje in v hlevih ne bo črede,
18 hata hivyo nitashangilia katika Bwana, nitamfurahia Mungu Mwokozi wangu.
se bom vendar veselil v Gospodu, užival bom v Bogu rešitve moje duše.
19 Bwana Mwenyezi ni nguvu yangu; huifanya miguu yangu kama miguu ya ayala, huniwezesha kupita juu ya vilima. Kwa kiongozi wa uimbaji. Kwa vinanda vyangu vya nyuzi.
Gospod Bog je moja moč in on bo moja stopala naredil podobna košutinim stopalom in dal mi bo, da hodim na svojih visokih krajih. Vodilnemu pevcu na moja glasbila na strune.

< Habakuki 3 >