< Habakuki 3 >

1 Sala ya nabii Habakuki iliyoimbwa kwa shigionothi.
Pravieša Habakuka lūgšana, pēc augstas dziesmas dziedama: Kungs, kad es dzirdēju Tavu slavu, tad es izbijos.
2 Bwana, nimezisikia sifa zako; nami naogopa kwa matendo yako, Ee Bwana. Fufua kazi yako katikati ya miaka, katikati ya miaka tangaza habari yako; katika ghadhabu kumbuka rehema.
Kungs, tas ir Tavs darbs, izdari to gadiem ritot, gadiem ritot dari to zināmu. Dusmībā piemini žēlastību.
3 Mungu alitoka Temani, yeye Aliye Mtakatifu kutoka Mlima Parani. Utukufu wake ulifunika mbingu, na sifa zake zikaifunika dunia.
Dievs nāk no Tēmana un tas Svētais no Pārana kalniem. (Sela) Viņa augstība apklāj debesis, un zeme ir pilna Viņa slavas.
4 Mngʼao wake ulikuwa kama jua lichomozalo; mionzi ilimulika kutoka mkononi mwake, ambako nguvu zake zilifichwa.
Un spožums atspīd kā (saules) gaisma un stari Viņam abējās pusēs, un tur Viņa spēcība slēpjās.
5 Tauni ilimtangulia; maradhi ya kuambukiza yalifuata nyayo zake.
Viņa priekšā iet mēris, un sērga uz viņa pēdām.
6 Alisimama, akaitikisa dunia; alitazama, na kuyafanya mataifa yatetemeke. Milima ya zamani iligeuka mavumbi na vilima vilivyozeeka vikaanguka. Njia zake ni za milele.
Viņš stāv un satrīcina zemi, Viņš skatās un biedina tautas, mūžīgie kalni šķīst, vecu vecie pakalni grimst; Viņš staigā mūžības ceļus.
7 Niliona watu wa Kushani katika dhiki, na makazi ya Midiani katika maumivu makali.
Es redzēju Moru ļaužu teltis postā un Midijaniešu dzīvokļus drebam.
8 Ee Bwana, uliikasirikia mito? Je, ghadhabu yako ilikuwa dhidi ya vijito? Je, ulighadhibikia bahari ulipoendesha farasi wako na magari yako ya ushindi?
Vai Tu par upēm esi apskaities, ak Kungs, vai Tev dusmas par ūdeņiem, vai Tev bardzība par jūru, ka Tu brauci ar Saviem zirgiem uz Saviem glābšanas ratiem?
9 Uliufunua upinde wako na kuita mishale mingi. Uliigawa dunia kwa mito;
Tavs stops izvilkts spīd, rīkste, vārdos zvērēta (Sela) Zemi Tu skaldi upēs.
10 milima ilikuona ikatetemeka. Mafuriko ya maji yakapita huko; vilindi vilinguruma na kuinua mawimbi yake juu.
Kalni Tevi ierauga, un tiem paliek bail, ūdens plūdi plūst, dziļums kauc, un augsti paceļ savas rokas.
11 Jua na mwezi vilisimama kimya mbinguni katika mngʼao wa mishale yako inayoruka, na katika mngʼao wa mkuki wako umeremetao.
Saule un mēness paliek stāvot savā mājoklī, Tavām bultām šaujoties un spīdot, Taviem šķēpiem spīdot un zibot.
12 Kwa ghadhabu ulipita juu ya dunia, na katika hasira ulikanyaga mataifa.
Dusmībā Tu samini zemi, bardzībā Tu sadragā tautas.
13 Ulikuja kuwaokoa watu wako, kumwokoa uliyemtia mafuta. Ulimponda kiongozi wa nchi ya uovu, ukamvua toka kichwani hadi wayo.
Tu izej, glābt Savus ļaudis, glābt Savu svaidīto, Tu satrieci bezdievīgā nama galvu, atsegdams pamatu līdz pat kaklam. (Sela)
14 Kwa mkuki wake mwenyewe ulitoboa kichwa chake wakati mashujaa wake walifurika nje kwa kishindo kututawanya, wakifurahi kama walio karibu kutafuna wale wanyonge waliokuwa mafichoni.
Ar viņa paša šķēpiem Tu satrieci viņa karavīru galvu, kas kā vētra nāk, mani izkaisīt, kam prieks, nabagu aprīt slepenībā.
15 Ulikanyaga bahari kwa farasi wako, ukisukasuka maji makuu.
Tu jāji ar saviem zirgiem pa jūru, pa varenu ūdeņu plūdiem.
16 Nilisikia na moyo wangu ukagonga kwa nguvu, midomo yangu ikatetemeka kwa hofu niliposikia sauti; uchakavu ukanyemelea mifupa yangu, na miguu yangu ikatetemeka. Hata hivyo nitasubiri kwa uvumilivu siku ya maafa kuyajilia mataifa yaliyotuvamia.
Kad es to dzirdēju, tad manas iekšas trīcēja, no tās balss drebēja manas lūpas; puveši nāk manos kaulos, es trīcu savā vietā, ka man klusu jāgaida tā bēdu diena, kad celsies pret tiem ļaudīm, kas tos spaidīs.
17 Ingawa mtini hauchanui maua na hakuna zabibu juu ya mizabibu, ingawaje mzeituni hauzai, na hata mashamba hayatoi chakula, iwapo hakuna kondoo katika banda, wala ngʼombe katika zizi,
Ja vīģes koks nezaļos, un augļu nebūs vīna kokam; eļļas koka augums nepiepilda cerības, un tīrumi nenes barību, avis izzudušas no ganībām un lopa nav laidaros.
18 hata hivyo nitashangilia katika Bwana, nitamfurahia Mungu Mwokozi wangu.
Bet tomēr es priecāšos iekš Tā Kunga, es līksmošos iekš Dieva, sava Pestītāja.
19 Bwana Mwenyezi ni nguvu yangu; huifanya miguu yangu kama miguu ya ayala, huniwezesha kupita juu ya vilima. Kwa kiongozi wa uimbaji. Kwa vinanda vyangu vya nyuzi.
Tas Kungs Dievs ir mans stiprums, viņš dara man kājas kā stirnām un mani vedīs pa maniem kalniem. - Dziedātāju vadonim uz manām koklēm.

< Habakuki 3 >