< Habakuki 3 >

1 Sala ya nabii Habakuki iliyoimbwa kwa shigionothi.
Prière d’Habacuc, le prophète, pour les ignorances.
2 Bwana, nimezisikia sifa zako; nami naogopa kwa matendo yako, Ee Bwana. Fufua kazi yako katikati ya miaka, katikati ya miaka tangaza habari yako; katika ghadhabu kumbuka rehema.
Seigneur, j’ai entendu votre parole, et j’ai craint, Seigneur, votre œuvre; au milieu des années, vivifiez-la. Au milieu des années vous la ferez connaître; lorsque vous serez en colère, vous vous souviendrez de la miséricorde.
3 Mungu alitoka Temani, yeye Aliye Mtakatifu kutoka Mlima Parani. Utukufu wake ulifunika mbingu, na sifa zake zikaifunika dunia.
Dieu viendra du midi, et le saint de la montagne de Pharan; Sa gloire a couvert les deux, et de sa louange est pleine la terre.
4 Mngʼao wake ulikuwa kama jua lichomozalo; mionzi ilimulika kutoka mkononi mwake, ambako nguvu zake zilifichwa.
Sa splendeur brillera comme la lumière, ses cornes sont dans ses mains; Là a été cachée sa puissance;
5 Tauni ilimtangulia; maradhi ya kuambukiza yalifuata nyayo zake.
Devant sa face ira la mort. Et le diable sortira devant ses pieds.
6 Alisimama, akaitikisa dunia; alitazama, na kuyafanya mataifa yatetemeke. Milima ya zamani iligeuka mavumbi na vilima vilivyozeeka vikaanguka. Njia zake ni za milele.
Il s’est arrêté, et il a mesuré la terre. Il a regardé, et il a dissipé les nations; et les montagnes du siècle se sont entrouvertes. Les collines du monde ont été abaissées par les marches de son éternité.
7 Niliona watu wa Kushani katika dhiki, na makazi ya Midiani katika maumivu makali.
J’ai vu les tentes de l’Ethiopie renversées pour son iniquité; les pavillons de la terre de Madian seront troublés.
8 Ee Bwana, uliikasirikia mito? Je, ghadhabu yako ilikuwa dhidi ya vijito? Je, ulighadhibikia bahari ulipoendesha farasi wako na magari yako ya ushindi?
Est-ce contre les fleuves que vous êtes en colère, Seigneur? ou contre les fleuves qu’est votre fureur; ou bien contre la mer qu’est votre indignation? Vous qui monterez sur vos chevaux; et vos quadriges seront le salut.
9 Uliufunua upinde wako na kuita mishale mingi. Uliigawa dunia kwa mito;
Préparant, vous préparerez votre arc, selon les serments que vous avez faits aux tribus. Vous diviserez les fleuves de la terre.
10 milima ilikuona ikatetemeka. Mafuriko ya maji yakapita huko; vilindi vilinguruma na kuinua mawimbi yake juu.
Les montagnes vous ont vu et elles ont été dans la douleur. La masse des eaux s’est écoulée. L’abîme a fait entendre sa voix; il a levé en haut ses mains.
11 Jua na mwezi vilisimama kimya mbinguni katika mngʼao wa mishale yako inayoruka, na katika mngʼao wa mkuki wako umeremetao.
Le soleil et la lune se sont arrêtés dans leur demeure; ils iront à la lumière de vos flèches, à l’éclat de votre lance foudroyante.
12 Kwa ghadhabu ulipita juu ya dunia, na katika hasira ulikanyaga mataifa.
Dans votre frémissement, vous foulerez aux pieds la terre; dans votre fureur, vous épouvanterez les nations.
13 Ulikuja kuwaokoa watu wako, kumwokoa uliyemtia mafuta. Ulimponda kiongozi wa nchi ya uovu, ukamvua toka kichwani hadi wayo.
Vous êtes sorti pour le salut de votre peuple, pour le salut avec votre Christ. Vous avez frappé le chef de la maison de l’impie; vous l’avez mis à nu depuis les pieds jusqu’au cou.
14 Kwa mkuki wake mwenyewe ulitoboa kichwa chake wakati mashujaa wake walifurika nje kwa kishindo kututawanya, wakifurahi kama walio karibu kutafuna wale wanyonge waliokuwa mafichoni.
Vous avez maudit ses sceptres, le chef de ses guerriers qui venaient comme un tourbillon pour me mettre en déroute. Leur exultation était comme l’exultation de celui qui dévore le pauvre en secret.
15 Ulikanyaga bahari kwa farasi wako, ukisukasuka maji makuu.
Vous avez fait une voie dans la mer à vos chevaux, dans la fange des grandes eaux.
16 Nilisikia na moyo wangu ukagonga kwa nguvu, midomo yangu ikatetemeka kwa hofu niliposikia sauti; uchakavu ukanyemelea mifupa yangu, na miguu yangu ikatetemeka. Hata hivyo nitasubiri kwa uvumilivu siku ya maafa kuyajilia mataifa yaliyotuvamia.
J’ai entendu, et mes entrailles ont été émues; à cette voix, mes lèvres ont frémi. Que la pourriture entre dans mes os, et qu’elle abonde sous moi; Afin que je me repose au jour de la tribulation, afin que je monte vers notre peuple ceint.
17 Ingawa mtini hauchanui maua na hakuna zabibu juu ya mizabibu, ingawaje mzeituni hauzai, na hata mashamba hayatoi chakula, iwapo hakuna kondoo katika banda, wala ngʼombe katika zizi,
Car le figuier ne fleurira pas, et il n’y aura pas de germe dans les vignes. Le produit de l’olivier trompera l’attente, et les champs ne porteront pas de grains. Le troupeau de menu bétail sera arraché de la bergerie, et il n’y aura pas de troupeau de gros bétail dans les étables.
18 hata hivyo nitashangilia katika Bwana, nitamfurahia Mungu Mwokozi wangu.
Mais moi, je me réjouirai dans le Seigneur, et j’exulterai en Dieu mon Jésus.
19 Bwana Mwenyezi ni nguvu yangu; huifanya miguu yangu kama miguu ya ayala, huniwezesha kupita juu ya vilima. Kwa kiongozi wa uimbaji. Kwa vinanda vyangu vya nyuzi.
Dieu le Seigneur est ma force; et il rendra mes pieds comme ceux des cerfs. Et vainqueur il me conduira sur mes hauteurs, pendant que je chanterai des psaumes.

< Habakuki 3 >