< Habakuki 3 >

1 Sala ya nabii Habakuki iliyoimbwa kwa shigionothi.
Seigneur, j'ai entendu Ta voix, et j'ai eu crainte.
2 Bwana, nimezisikia sifa zako; nami naogopa kwa matendo yako, Ee Bwana. Fufua kazi yako katikati ya miaka, katikati ya miaka tangaza habari yako; katika ghadhabu kumbuka rehema.
J'ai considéré Tes œuvres, et je me suis extasié. Entre deux animaux Tu Te manifestes; quand les années seront proches, on Te connaîtra; quand les temps seront venus, Tu apparaîtras; quand mon âme est troublée de Ta colère, souviens-Toi de Ta miséricorde.
3 Mungu alitoka Temani, yeye Aliye Mtakatifu kutoka Mlima Parani. Utukufu wake ulifunika mbingu, na sifa zake zikaifunika dunia.
Dieu viendra de Théman, et le Saint de la montagne ténébreuse de Pharan. Sa vertu est le vêtement des cieux, et la terre est pleine de Sa louange.
4 Mngʼao wake ulikuwa kama jua lichomozalo; mionzi ilimulika kutoka mkononi mwake, ambako nguvu zake zilifichwa.
Sa splendeur sera comme la lumière; Il a dans Sa main des cornes (de puissance), et de la force Il a fait un puissant amour.
5 Tauni ilimtangulia; maradhi ya kuambukiza yalifuata nyayo zake.
Devant Sa face ira une parole; elle cheminera dans les plaines; sur Ses pieds
6 Alisimama, akaitikisa dunia; alitazama, na kuyafanya mataifa yatetemeke. Milima ya zamani iligeuka mavumbi na vilima vilivyozeeka vikaanguka. Njia zake ni za milele.
Il S'est dressé, et la terre en a tremblé; Il a regardé, et les nations se sont évanouies. les montagnes ont été violemment agitées; les collines se sont fendues, sous les pas de Sa marche éternelle.
7 Niliona watu wa Kushani katika dhiki, na makazi ya Midiani katika maumivu makali.
À cause des troubles, j'ai vu les tentes des Éthiopiens renversées; les tentes de la terre de Madian seront aussi frappées d'épouvante.
8 Ee Bwana, uliikasirikia mito? Je, ghadhabu yako ilikuwa dhidi ya vijito? Je, ulighadhibikia bahari ulipoendesha farasi wako na magari yako ya ushindi?
Seigneur, est-ce contre les fleuves que Tu es irrité? Est-ce que Ta colère s'en prend aux fleuves? Attaques-Tu la mer? Car Tu es monté sur Ton char, et Tes chevaux amènent le salut.
9 Uliufunua upinde wako na kuita mishale mingi. Uliigawa dunia kwa mito;
Tu as fortement tendu ton arc contre les sceptres, dit le Seigneur. le cours des fleuves sera déchiré.
10 milima ilikuona ikatetemeka. Mafuriko ya maji yakapita huko; vilindi vilinguruma na kuinua mawimbi yake juu.
Les peuples Te verront, Seigneur, et ils auront des douleurs comme celles de l'enfantement. Quand Tu détruis la voie par une inondation, l'abîme a fait entendre sa voix, et il a élevé ses vagues contre Toi.
11 Jua na mwezi vilisimama kimya mbinguni katika mngʼao wa mishale yako inayoruka, na katika mngʼao wa mkuki wako umeremetao.
Le soleil s'est levé; la lune s'est tenue au lieu qui lui est prescrit: Tes rayons s'avanceront dans la lumière, à la lueur des éclairs qui jaillissent de Tes armes.
12 Kwa ghadhabu ulipita juu ya dunia, na katika hasira ulikanyaga mataifa.
Par Tes menaces, Tu abaisses la terre, et dans Ton courroux Tu abats les nations.
13 Ulikuja kuwaokoa watu wako, kumwokoa uliyemtia mafuta. Ulimponda kiongozi wa nchi ya uovu, ukamvua toka kichwani hadi wayo.
Tu es venu pour le salut de Ton peuple, pour sauver Ton Christ; Tu enverras la mort sur la tête des impies; Tu les as chargés de chaînes jusqu'au cou.
14 Kwa mkuki wake mwenyewe ulitoboa kichwa chake wakati mashujaa wake walifurika nje kwa kishindo kututawanya, wakifurahi kama walio karibu kutafuna wale wanyonge waliokuwa mafichoni.
Tu as frappé de stupeur les bêtes des puissants; ils en trembleront; ils laisseront voir leur frein en ouvrant la bouche, comme un pauvre qui mange en se cachant.
15 Ulikanyaga bahari kwa farasi wako, ukisukasuka maji makuu.
Et, monté sur Tes chevaux, Tu es entré dans la mer, et ils en ont troublé l'eau profonde.
16 Nilisikia na moyo wangu ukagonga kwa nguvu, midomo yangu ikatetemeka kwa hofu niliposikia sauti; uchakavu ukanyemelea mifupa yangu, na miguu yangu ikatetemeka. Hata hivyo nitasubiri kwa uvumilivu siku ya maafa kuyajilia mataifa yaliyotuvamia.
J'ai veillé, et mes entrailles ont frémi au son de la prière de mes lèvres, et l'effroi est entré dans mes os, et tout mon être a été bouleversé. Je me reposerai au jour de l'affliction, et je monterai chez le peuple où je suis passager.
17 Ingawa mtini hauchanui maua na hakuna zabibu juu ya mizabibu, ingawaje mzeituni hauzai, na hata mashamba hayatoi chakula, iwapo hakuna kondoo katika banda, wala ngʼombe katika zizi,
Car alors le figuier ne portera pas de fruits; il n'y aura pas de raisin à la vigne; l'œuvre de l'olivier sera trompeuse, et les champs ne produiront pas de nourriture. Les brebis manqueront de fourrage, et il n'y aura pas de bœufs à la crèche.
18 hata hivyo nitashangilia katika Bwana, nitamfurahia Mungu Mwokozi wangu.
Pour moi, je tressaillirai dans le Seigneur; je mettrai ma joie en Dieu, mon Sauveur.
19 Bwana Mwenyezi ni nguvu yangu; huifanya miguu yangu kama miguu ya ayala, huniwezesha kupita juu ya vilima. Kwa kiongozi wa uimbaji. Kwa vinanda vyangu vya nyuzi.
Le Seigneur mon Dieu est ma force; Il placera mes pieds sur une base inébranlable; Il m'a fait monter sur les hautes cimes, pour chanter en Son honneur un chant de triomphe.

< Habakuki 3 >