< Habakuki 3 >
1 Sala ya nabii Habakuki iliyoimbwa kwa shigionothi.
Prière d’Habacuc le prophète. Sur le mode dithyrambique.
2 Bwana, nimezisikia sifa zako; nami naogopa kwa matendo yako, Ee Bwana. Fufua kazi yako katikati ya miaka, katikati ya miaka tangaza habari yako; katika ghadhabu kumbuka rehema.
Yahweh, j’ai entendu ce que tu as fait entendre, je suis saisi de crainte, Yahweh! Ton œuvre, dans le cours des âges, fais-la vivre; dans le cours des âges fais-la connaître! Dans ta colère, souviens-toi d’avoir pitié.
3 Mungu alitoka Temani, yeye Aliye Mtakatifu kutoka Mlima Parani. Utukufu wake ulifunika mbingu, na sifa zake zikaifunika dunia.
Dieu vient de Théman, et le Saint de la montagne de Pharan (Séla). Sa majesté a couvert les cieux, et la terre a été remplie de sa gloire.
4 Mngʼao wake ulikuwa kama jua lichomozalo; mionzi ilimulika kutoka mkononi mwake, ambako nguvu zake zilifichwa.
C’est un éclat comme la lumière du soleil levant; des rayons partent de ses mains; là se cache sa puissance.
5 Tauni ilimtangulia; maradhi ya kuambukiza yalifuata nyayo zake.
Devant lui marche la mortalité, et la fièvre brûlante est sur ses pas.
6 Alisimama, akaitikisa dunia; alitazama, na kuyafanya mataifa yatetemeke. Milima ya zamani iligeuka mavumbi na vilima vilivyozeeka vikaanguka. Njia zake ni za milele.
Il s’est arrêté et a fait trembler la terre, il a regardé et a secoué les nations; les montagnes éternelles se sont brisées, les collines antiques se sont affaissées; il suit ses voies d’autrefois.
7 Niliona watu wa Kushani katika dhiki, na makazi ya Midiani katika maumivu makali.
J’ai vu dans la détresse les tentes de Cuschan; les pavillons de la terre de Moab frémissent.
8 Ee Bwana, uliikasirikia mito? Je, ghadhabu yako ilikuwa dhidi ya vijito? Je, ulighadhibikia bahari ulipoendesha farasi wako na magari yako ya ushindi?
Est-ce contre des fleuves que Yahweh s’est irrité? Ou bien est-ce contre les fleuves que s’enflamme ta colère; contre la mer que se déchaîne ta fureur, lorsque tu montes sur tes chevaux, sur tes chars de délivrance?
9 Uliufunua upinde wako na kuita mishale mingi. Uliigawa dunia kwa mito;
A nu ton arc se découvre; tes traits sont les serments que tu as prononcés (Séla). En torrents tu fends la terre.
10 milima ilikuona ikatetemeka. Mafuriko ya maji yakapita huko; vilindi vilinguruma na kuinua mawimbi yake juu.
Les montagnes t’ont vu et tremblent; une trombe d’eau a passé; l’abîme a fait entendre sa voix, il tend ses mains en haut.
11 Jua na mwezi vilisimama kimya mbinguni katika mngʼao wa mishale yako inayoruka, na katika mngʼao wa mkuki wako umeremetao.
Le soleil et la lune sont restés dans leur demeure; on marche à la clarté de tes flèches à la lueur des éclairs de ta lance.
12 Kwa ghadhabu ulipita juu ya dunia, na katika hasira ulikanyaga mataifa.
Tu parcours la terre avec fureur, tu foules les nations avec colère.
13 Ulikuja kuwaokoa watu wako, kumwokoa uliyemtia mafuta. Ulimponda kiongozi wa nchi ya uovu, ukamvua toka kichwani hadi wayo.
Tu es sorti pour la délivrance de ton peuple; pour la délivrance de ton Oint; tu as brisé le faîte de la maison du méchant, mettant à nu les fondements jusqu’en bas (Séla).
14 Kwa mkuki wake mwenyewe ulitoboa kichwa chake wakati mashujaa wake walifurika nje kwa kishindo kututawanya, wakifurahi kama walio karibu kutafuna wale wanyonge waliokuwa mafichoni.
Tu as percé de ses propres traits le chef de ses bandes, qui se précipitaient pour me disperser, en poussant des cris de joie, comme s’ils allaient dévorer le malheureux dans leur repaire.
15 Ulikanyaga bahari kwa farasi wako, ukisukasuka maji makuu.
Tu foules la mer sous les pieds de tes chevaux, l’amas des grandes eaux.
16 Nilisikia na moyo wangu ukagonga kwa nguvu, midomo yangu ikatetemeka kwa hofu niliposikia sauti; uchakavu ukanyemelea mifupa yangu, na miguu yangu ikatetemeka. Hata hivyo nitasubiri kwa uvumilivu siku ya maafa kuyajilia mataifa yaliyotuvamia.
J’ai entendu, et mes entrailles se sont émues; à cette voix mes lèvres frémissent, la carie entre dans mes os, mes genoux tremblent sous moi, de ce que je dois attendre en repos le jour de détresse; où l’ennemi montera contre un peuple pour l’opprimer.
17 Ingawa mtini hauchanui maua na hakuna zabibu juu ya mizabibu, ingawaje mzeituni hauzai, na hata mashamba hayatoi chakula, iwapo hakuna kondoo katika banda, wala ngʼombe katika zizi,
Car alors le figuier ne fleurira pas, il n’y aura rien à récolter dans les vignes; le fruit de l’olivier manquera, et les champs ne donneront pas de nourriture; la brebis disparaîtra de la bergerie, et il n’y aura plus de bœufs dans les étables.
18 hata hivyo nitashangilia katika Bwana, nitamfurahia Mungu Mwokozi wangu.
Et moi, je veux me réjouir en Yahweh, tressaillir de joie dans le Dieu de mon salut.
19 Bwana Mwenyezi ni nguvu yangu; huifanya miguu yangu kama miguu ya ayala, huniwezesha kupita juu ya vilima. Kwa kiongozi wa uimbaji. Kwa vinanda vyangu vya nyuzi.
Yahweh, le Seigneur, est ma force; il rend mes pieds pareils à ceux des biches, et me fait marcher sur mes lieux élevés. Au chef des chantres, sur mes instruments à cordes.