< Habakuki 2 >
1 Nitasimama katika zamu yangu, na kujiweka mwenyewe juu ya maboma; nitatazama nione atakaloniambia, na ni jibu gani nitakalotoa kuhusu lalamiko hili.
Me pondré a vigilar y me situaré en las murallas, y miraré a ver qué me dice y qué respondo sobre mi queja.
2 Kisha Bwana akajibu: “Andika ufunuo huu, na ukaufanye wazi juu ya vibao, ili mpiga mbiu akimbie nao.
El Señor me respondió: “Escribe la visión, y hazla clara en tablas, para que el que corra pueda leerla.
3 Kwa kuwa ufunuo huu unasubiri wakati uliokubalika; unazungumzia mambo ya mwisho, na kamwe hautakosea. Iwapo utakawia, wewe usubiri; kwa hakika utakuja na hautachelewa.
Porque la visión es todavía para el tiempo señalado, y se apresura hacia el fin, y no resultará falsa. Aunque se demore, espérala, porque seguramente vendrá. No se demorará.
4 “Tazama, amejaa majivuno; anavyovitamani si vya unyofu: lakini mwenye haki ataishi kwa imani yake:
He aquí que su alma está hinchada. No es recto en él, pero el justo vivirá por su fe.
5 hakika mvinyo humsaliti; ni mwenye kiburi na hana amani. Kwa sababu ni mlafi kama kuzimu na kama kifo kamwe hatosheki; anajikusanyia mataifa yote na kuchukua watu wote mateka. (Sheol )
Sí, además, el vino es traicionero: un arrogante que no se queda en casa, que agranda su deseo como el Seol; es como la muerte y no puede saciarse, sino que reúne para sí todas las naciones y amontona para sí todos los pueblos. (Sheol )
6 “Je, watu wote hawatamsuta kwa dhihaka na kumbeza, wakisema, “‘Ole wake yeye akusanyaye bidhaa zilizoibwa na kujifanyia utajiri kwa kutoza kwa nguvu! Ataendelea hivi kwa muda gani?’
¿No tomarán todos estos una parábola contra él, y un proverbio burlón contra él, y dirán: ‘¡Ay del que aumenta lo que no es suyo, y del que se enriquece con la extorsión! ¿Hasta cuándo?’
7 Je, wadai wako hawatainuka ghafula? Je, hawataamka na kukufanya utetemeke? Kisha utakuwa mhanga kwao.
¿No se levantarán de repente tus deudores, y despertarán los que te hacen temblar, y serás su víctima?
8 Kwa kuwa umeteka nyara mataifa mengi, watu waliobaki watakuteka nyara wewe. Kwa kuwa umemwaga damu ya mtu; umeharibu nchi na miji, na kila mmoja ndani yake.
Porque has saqueado a muchas naciones, todo el resto de los pueblos te saqueará a causa de la sangre de los hombres, y por la violencia hecha a la tierra, a la ciudad y a todos los que la habitan.
9 “Ole wake yeye ajengaye milki yake kwa mapato ya udhalimu, awekaye kiota chake juu, ili kukimbia makucha ya uharibifu!
¡Ay del que obtiene una mala ganancia para su casa, para poner su nido en alto, para librarse de la mano del mal!
10 Umefanya shauri la maangamizi ya watu wengi, ukiaibisha nyumba yako mwenyewe, na kupotewa na maisha yako.
Has ideado una vergüenza para tu casa, despojando a muchos pueblos, y has pecado contra tu alma.
11 Mawe ya kuta yatapiga kelele, na mihimili ya kazi ya mbao itarudisha mwangwi wake.
Porque la piedra clamará desde la pared, y la viga desde la madera le responderá.
12 “Ole wake yeye ajengaye mji kwa kumwaga damu na kuusimamisha mji kwa uhalifu!
¡Ay del que construye un pueblo con sangre, y establece una ciudad con iniquidad!
13 Je, Bwana Mwenye Nguvu Zote hakuonyesha kwamba kazi ya wanadamu ni mafuta tu kwa ajili ya moto, na kwamba mataifa yanajichosha bure?
He aquí, ¿no es de Yahvé de los Ejércitos que los pueblos se afanen por el fuego, y las naciones se fatiguen por la vanidad?
14 Kwa kuwa dunia itajazwa na maarifa ya utukufu wa Bwana, kama maji yaifunikavyo bahari.
Porque la tierra se llenará del conocimiento de la gloria de Yahvé, como las aguas cubren el mar.
15 “Ole wake yeye awapaye jirani zake kileo, akiimimina kutoka kwenye kiriba cha mvinyo mpaka wamelewa, ili apate kutazama miili yao iliyo uchi.
“¡Ay del que da de beber a su prójimo, derramando tu vino inflamable hasta que se emborrachen, para que puedas contemplar sus cuerpos desnudos!
16 Utajazwa na aibu badala ya utukufu. Sasa ni zamu yako! Kunywa na ujifunue! Kikombe kutoka kwenye mkono wa kuume wa Bwana kinakujia, na aibu itafunika utukufu wako.
Os llenáis de vergüenza y no de gloria. ¡Tú también beberás y quedarás al descubierto! La copa de la mano derecha de Yahvé se volverá sobre ti, y la desgracia cubrirá tu gloria.
17 Ukatili ulioifanyia Lebanoni utakufunika, na uharibifu uliowafanyia wanyama utakutisha. Kwa sababu umemwaga damu ya mtu; umeharibu nchi na miji na kila mmoja aliyeko ndani yake.
Porque la violencia hecha al Líbano te abrumará, y la destrucción de los animales te aterrorizará, a causa de la sangre de los hombres y por la violencia hecha a la tierra, a cada ciudad y a los que la habitan.
18 “Sanamu ina thamani gani, kwani mwanadamu ndiye alichonga? Ama kinyago kinachofundisha uongo? Kwa kuwa yeye aliyekitengeneza hutegemea kazi ya mikono yake mwenyewe; hutengeneza sanamu zisizoweza kuzungumza.
“¿Qué valor tiene la imagen grabada, para que su hacedor la haya grabado; la imagen fundida, maestra de la mentira, para que el que modela su forma confíe en ella, para hacer ídolos mudos?
19 Ole wake yeye auambiaye mti, ‘Uwe hai!’ Ama asemaye na jiwe lisilo na uhai, ‘Amka!’ Je, linaweza kuongoza? Limefunikwa kwa dhahabu na fedha; hakuna pumzi ndani yake.
¡Ay de aquel que dice a la madera: “Despierta”, o a la piedra muda: “Levántate”! ¿Acaso esto enseña? He aquí que está recubierto de oro y plata, y no hay en él aliento alguno.
20 Lakini Bwana yuko katika Hekalu lake takatifu; dunia yote na inyamaze mbele yake.”
Pero Yahvé está en su santo templo. Que toda la tierra guarde silencio ante él”.