< Habakuki 2 >
1 Nitasimama katika zamu yangu, na kujiweka mwenyewe juu ya maboma; nitatazama nione atakaloniambia, na ni jibu gani nitakalotoa kuhusu lalamiko hili.
Je me tiendrai en garde, et je monterai sur une roche, et je veillerai pour savoir ce qu'on dira contre moi, et ce que je répondrai quand je serai repris.
2 Kisha Bwana akajibu: “Andika ufunuo huu, na ukaufanye wazi juu ya vibao, ili mpiga mbiu akimbie nao.
Et le Seigneur me parla, et Il me dit: Écris ta vision, écris-la clairement sur une tablette, afin qu'on la lise couramment.
3 Kwa kuwa ufunuo huu unasubiri wakati uliokubalika; unazungumzia mambo ya mwisho, na kamwe hautakosea. Iwapo utakawia, wewe usubiri; kwa hakika utakuja na hautachelewa.
Car ta vision est véritable; elle se réalisera au temps marqué; elle ne sera point vaine. S'il ne vient pas encore, attends-le; car sûrement il viendra et ne tardera point.
4 “Tazama, amejaa majivuno; anavyovitamani si vya unyofu: lakini mwenye haki ataishi kwa imani yake:
Celui qui se retire de Moi, Mon âme ne se complaira pas avec lui; le juste vivra de sa foi en Moi.
5 hakika mvinyo humsaliti; ni mwenye kiburi na hana amani. Kwa sababu ni mlafi kama kuzimu na kama kifo kamwe hatosheki; anajikusanyia mataifa yote na kuchukua watu wote mateka. (Sheol )
L'homme présomptueux, méprisant, imposteur, n'arrivera point à ses fins; celui qui a rendu son âme vaste comme l'enfer est aussi insatiable que la mort; il réunira sous lui toutes les nations, et il recevra sous lui tous les peuples. (Sheol )
6 “Je, watu wote hawatamsuta kwa dhihaka na kumbeza, wakisema, “‘Ole wake yeye akusanyaye bidhaa zilizoibwa na kujifanyia utajiri kwa kutoza kwa nguvu! Ataendelea hivi kwa muda gani?’
Mais toutes ces choses ne feront-elles pas de lui un sujet d'histoires et de récits qu'on se répétera? On dira: Malheur à l'homme qui, sans se lasser, accumule les biens d'autrui, et fait cruellement sentir le poids de son collier!
7 Je, wadai wako hawatainuka ghafula? Je, hawataamka na kukufanya utetemeke? Kisha utakuwa mhanga kwao.
Car soudain s'élèveront contre toi des gens qui te mordront, et autour de toi veilleront des assassins, et tu seras pour eux une proie.
8 Kwa kuwa umeteka nyara mataifa mengi, watu waliobaki watakuteka nyara wewe. Kwa kuwa umemwaga damu ya mtu; umeharibu nchi na miji, na kila mmoja ndani yake.
Parce que tu as pillé une multitude de nations, les peuples qui restent encore te pilleront à leur tour, à cause du sang des hommes, à cause de tes impiétés contre la terre, contre la ville et ses habitants.
9 “Ole wake yeye ajengaye milki yake kwa mapato ya udhalimu, awekaye kiota chake juu, ili kukimbia makucha ya uharibifu!
Malheur à celui qui, en sa maison, a de mauvaises convoitises, qui veut placer haut son nid, pour se délivrer de la main du malheur!
10 Umefanya shauri la maangamizi ya watu wengi, ukiaibisha nyumba yako mwenyewe, na kupotewa na maisha yako.
Tu as médité la honte de ta maison, tu as épuisé beaucoup de peuples, et ton âme a péché.
11 Mawe ya kuta yatapiga kelele, na mihimili ya kazi ya mbao itarudisha mwangwi wake.
Aussi la pierre des murailles criera-t-elle contre toi, et l'escarbot du haut des solives lui fera écho.
12 “Ole wake yeye ajengaye mji kwa kumwaga damu na kuusimamisha mji kwa uhalifu!
Malheur à celui qui bâtit une maison avec le sang, et qui la fonde avec l'iniquité!
13 Je, Bwana Mwenye Nguvu Zote hakuonyesha kwamba kazi ya wanadamu ni mafuta tu kwa ajili ya moto, na kwamba mataifa yanajichosha bure?
Ces choses ne sont-elles pas du Seigneur tout-puissant? Maints peuples forts ont été épuisés par le feu, et maintes nations ont défailli,
14 Kwa kuwa dunia itajazwa na maarifa ya utukufu wa Bwana, kama maji yaifunikavyo bahari.
pour que la terre soit remplie de la connaissance de la gloire du Seigneur, qui la couvrira comme l'eau.
15 “Ole wake yeye awapaye jirani zake kileo, akiimimina kutoka kwenye kiriba cha mvinyo mpaka wamelewa, ili apate kutazama miili yao iliyo uchi.
Malheur à celui qui donne à boire à son ami de la lie de vin, et l'enivre pour voir dans ses cavernes!
16 Utajazwa na aibu badala ya utukufu. Sasa ni zamu yako! Kunywa na ujifunue! Kikombe kutoka kwenye mkono wa kuume wa Bwana kinakujia, na aibu itafunika utukufu wako.
Toi aussi, bois, au lieu de gloire, la plénitude de la honte; que ton cœur s'agite et tremble: te voilà plongé dans le calice que tient la main droite du Seigneur, et l'opprobre s'est amassé sur ta gloire;
17 Ukatili ulioifanyia Lebanoni utakufunika, na uharibifu uliowafanyia wanyama utakutisha. Kwa sababu umemwaga damu ya mtu; umeharibu nchi na miji na kila mmoja aliyeko ndani yake.
car l'impiété du Liban te couvrira, et les ravages des bêtes fauves te feront trembler, à cause du sang des hommes et de tes impiétés contre la terre, contre la vile et tous ses habitants.
18 “Sanamu ina thamani gani, kwani mwanadamu ndiye alichonga? Ama kinyago kinachofundisha uongo? Kwa kuwa yeye aliyekitengeneza hutegemea kazi ya mikono yake mwenyewe; hutengeneza sanamu zisizoweza kuzungumza.
À quoi peut servir une statue qu'eux-mêmes ont sculptée? On l'a jetée en fonte, apparence mensongère, et, pour faire une idole muette, l'artiste a eu foi en l'œuvre qu'il a façonnée.
19 Ole wake yeye auambiaye mti, ‘Uwe hai!’ Ama asemaye na jiwe lisilo na uhai, ‘Amka!’ Je, linaweza kuongoza? Limefunikwa kwa dhahabu na fedha; hakuna pumzi ndani yake.
Malheur à celui qui dit au bois: Sors de ton assoupissement, réveille-toi; et à la pierre: Lève-toi; car ce n'est qu'une image; c'est de l'or ou de l'argent battus au marteau, et il n'y a en cette œuvre aucun esprit.
20 Lakini Bwana yuko katika Hekalu lake takatifu; dunia yote na inyamaze mbele yake.”
Mais le Seigneur réside en Son saint temple; que toute la terre révère Son visage!