< Habakuki 2 >

1 Nitasimama katika zamu yangu, na kujiweka mwenyewe juu ya maboma; nitatazama nione atakaloniambia, na ni jibu gani nitakalotoa kuhusu lalamiko hili.
Je me tiendrai à ma garde et je me placerai sur les remparts, et je regarderai pour voir ce qu'il me dira, et ce que je répondrai au sujet de ma plainte.
2 Kisha Bwana akajibu: “Andika ufunuo huu, na ukaufanye wazi juu ya vibao, ili mpiga mbiu akimbie nao.
Yahvé me répondit: « Écris la vision, et mets-la en évidence sur des tablettes, afin que celui qui court puisse la lire.
3 Kwa kuwa ufunuo huu unasubiri wakati uliokubalika; unazungumzia mambo ya mwisho, na kamwe hautakosea. Iwapo utakawia, wewe usubiri; kwa hakika utakuja na hautachelewa.
Car la vision est encore pour le temps fixé, et elle se hâte vers la fin, et ne se démentira pas. Même si elle prend du temps, attendez-la, car elle viendra sûrement. Elle ne tardera pas.
4 “Tazama, amejaa majivuno; anavyovitamani si vya unyofu: lakini mwenye haki ataishi kwa imani yake:
Voici, son âme s'enfle d'orgueil. Il n'est pas droit en lui, mais le juste vivra par sa foi.
5 hakika mvinyo humsaliti; ni mwenye kiburi na hana amani. Kwa sababu ni mlafi kama kuzimu na kama kifo kamwe hatosheki; anajikusanyia mataifa yote na kuchukua watu wote mateka. (Sheol h7585)
Oui, de plus, le vin est perfide: un homme arrogant qui ne reste pas chez lui, qui élargit son désir comme le séjour des morts; il est comme la mort et ne peut être satisfait, mais il rassemble à lui toutes les nations et entasse à lui tous les peuples. (Sheol h7585)
6 “Je, watu wote hawatamsuta kwa dhihaka na kumbeza, wakisema, “‘Ole wake yeye akusanyaye bidhaa zilizoibwa na kujifanyia utajiri kwa kutoza kwa nguvu! Ataendelea hivi kwa muda gani?’
Tous ne prendront-ils pas contre lui une parabole et un proverbe de raillerie, et ne diront-ils pas: « Malheur à celui qui augmente ce qui ne lui appartient pas, et qui s'enrichit par l'extorsion! ». Jusqu'à quand? »
7 Je, wadai wako hawatainuka ghafula? Je, hawataamka na kukufanya utetemeke? Kisha utakuwa mhanga kwao.
Tes débiteurs ne vont-ils pas se lever soudainement, réveiller ceux qui te font trembler, et tu seras leur victime?
8 Kwa kuwa umeteka nyara mataifa mengi, watu waliobaki watakuteka nyara wewe. Kwa kuwa umemwaga damu ya mtu; umeharibu nchi na miji, na kila mmoja ndani yake.
Parce que tu as pillé de nombreuses nations, tout le reste des peuples te pillera à cause du sang des hommes, des violences faites au pays, à la ville et à tous ceux qui l'habitent.
9 “Ole wake yeye ajengaye milki yake kwa mapato ya udhalimu, awekaye kiota chake juu, ili kukimbia makucha ya uharibifu!
Malheur à celui qui obtient un mauvais gain pour sa maison, afin de placer son nid en haut, afin d'être délivré de la main du malheur!
10 Umefanya shauri la maangamizi ya watu wengi, ukiaibisha nyumba yako mwenyewe, na kupotewa na maisha yako.
Tu as conçu la honte de ta maison en exterminant de nombreux peuples, et tu as péché contre ton âme.
11 Mawe ya kuta yatapiga kelele, na mihimili ya kazi ya mbao itarudisha mwangwi wake.
Car la pierre criera de la muraille, et la poutre de la charpente y répondra.
12 “Ole wake yeye ajengaye mji kwa kumwaga damu na kuusimamisha mji kwa uhalifu!
Malheur à celui qui bâtit une ville par le sang, et qui affermit une cité par l'iniquité!
13 Je, Bwana Mwenye Nguvu Zote hakuonyesha kwamba kazi ya wanadamu ni mafuta tu kwa ajili ya moto, na kwamba mataifa yanajichosha bure?
Voici, n'est-ce pas de la part de l'Éternel des armées que les peuples travaillent pour le feu, et que les nations se fatiguent pour la vanité?
14 Kwa kuwa dunia itajazwa na maarifa ya utukufu wa Bwana, kama maji yaifunikavyo bahari.
Car la terre sera remplie de la connaissance de la gloire de l'Éternel, comme les eaux couvrent la mer.
15 “Ole wake yeye awapaye jirani zake kileo, akiimimina kutoka kwenye kiriba cha mvinyo mpaka wamelewa, ili apate kutazama miili yao iliyo uchi.
« Malheur à celui qui donne à boire à son prochain, en versant votre vin brûlant jusqu'à ce qu'ils soient ivres, afin que vous puissiez contempler leurs corps nus!
16 Utajazwa na aibu badala ya utukufu. Sasa ni zamu yako! Kunywa na ujifunue! Kikombe kutoka kwenye mkono wa kuume wa Bwana kinakujia, na aibu itafunika utukufu wako.
Vous êtes remplis de honte, et non de gloire. Vous aussi, vous boirez et serez exposés! La coupe de la main droite de Yahvé se retournera contre vous, et l'opprobre couvrira votre gloire.
17 Ukatili ulioifanyia Lebanoni utakufunika, na uharibifu uliowafanyia wanyama utakutisha. Kwa sababu umemwaga damu ya mtu; umeharibu nchi na miji na kila mmoja aliyeko ndani yake.
Car la violence faite au Liban vous accablera, et la destruction des animaux vous terrifiera, à cause du sang des hommes et de la violence faite au pays, à chaque ville et à ceux qui y habitent.
18 “Sanamu ina thamani gani, kwani mwanadamu ndiye alichonga? Ama kinyago kinachofundisha uongo? Kwa kuwa yeye aliyekitengeneza hutegemea kazi ya mikono yake mwenyewe; hutengeneza sanamu zisizoweza kuzungumza.
« Quelle valeur a l'image gravée, pour que son créateur l'ait gravée; l'image fondue, pour que celui qui en façonne la forme s'y fie, pour fabriquer des idoles muettes?
19 Ole wake yeye auambiaye mti, ‘Uwe hai!’ Ama asemaye na jiwe lisilo na uhai, ‘Amka!’ Je, linaweza kuongoza? Limefunikwa kwa dhahabu na fedha; hakuna pumzi ndani yake.
Malheur à celui qui dit au bois: « Réveille-toi! » ou à la pierre muette: « Lève-toi! ». Est-ce là un enseignement? Voici, elle est recouverte d'or et d'argent, et il n'y a en elle aucun souffle.
20 Lakini Bwana yuko katika Hekalu lake takatifu; dunia yote na inyamaze mbele yake.”
Mais Yahvé est dans son temple saint. Que toute la terre se taise devant lui! »

< Habakuki 2 >