< Habakuki 2 >
1 Nitasimama katika zamu yangu, na kujiweka mwenyewe juu ya maboma; nitatazama nione atakaloniambia, na ni jibu gani nitakalotoa kuhusu lalamiko hili.
Upon my watch-tower, will I stand, and will station myself upon the bulwark, —so will I keep outlook, to see—what he will speak with me, and what I shall reply, when I am reproved.
2 Kisha Bwana akajibu: “Andika ufunuo huu, na ukaufanye wazi juu ya vibao, ili mpiga mbiu akimbie nao.
Then Yahweh answered me, and said, Write the vision, Yea, make it plain on tablets, that one may swiftly read it;
3 Kwa kuwa ufunuo huu unasubiri wakati uliokubalika; unazungumzia mambo ya mwisho, na kamwe hautakosea. Iwapo utakawia, wewe usubiri; kwa hakika utakuja na hautachelewa.
For yet is the vision for an appointed time, still, it presseth towards an end, and will not deceive, —if it tarry, wait thou for it, for it, surely cometh, —will not be too late.
4 “Tazama, amejaa majivuno; anavyovitamani si vya unyofu: lakini mwenye haki ataishi kwa imani yake:
Lo! as for the conceited one, crooked is his soul within him, - but, one who is righteous, by his faithfulness, shall live.
5 hakika mvinyo humsaliti; ni mwenye kiburi na hana amani. Kwa sababu ni mlafi kama kuzimu na kama kifo kamwe hatosheki; anajikusanyia mataifa yote na kuchukua watu wote mateka. (Sheol )
Moreover also, when wine betrayeth, a man, is arrogant, and findeth no rest, —because he hath enlarged, like hades, his desire, yea, he, is like death, and cannot be satisfied, —but hath gathered unto himself, all the nations, and assembled unto himself, all the peoples. (Sheol )
6 “Je, watu wote hawatamsuta kwa dhihaka na kumbeza, wakisema, “‘Ole wake yeye akusanyaye bidhaa zilizoibwa na kujifanyia utajiri kwa kutoza kwa nguvu! Ataendelea hivi kwa muda gani?’
Shall not, these, all of them, against him, take up—a taunt, a mocking poem, enigmatical sentences—concerning him? And say—Alas! for him who maketh abundance in what is not his own, How long? that he should be burdening himself with heavy debts?
7 Je, wadai wako hawatainuka ghafula? Je, hawataamka na kukufanya utetemeke? Kisha utakuwa mhanga kwao.
Will not thy creditors, suddenly rise up? and they who shall violently shake thee, all at once become active? Then shalt thou serve for booties, unto them!
8 Kwa kuwa umeteka nyara mataifa mengi, watu waliobaki watakuteka nyara wewe. Kwa kuwa umemwaga damu ya mtu; umeharibu nchi na miji, na kila mmoja ndani yake.
Because, thou, hast plundered many nations, all the residue of the peoples, shall plunder thee, —for shedding Human blood, and doing violence to the earth, to the city, and to all who dwell therein.
9 “Ole wake yeye ajengaye milki yake kwa mapato ya udhalimu, awekaye kiota chake juu, ili kukimbia makucha ya uharibifu!
Alas! for him who extorteth an extortion of wrong for his own house, —that he may set on high his nest, that he may be delivered from the grasp of calamity.
10 Umefanya shauri la maangamizi ya watu wengi, ukiaibisha nyumba yako mwenyewe, na kupotewa na maisha yako.
Thou hast counseled shame to thy house—making an end of many peoples, and endangering thine own life.
11 Mawe ya kuta yatapiga kelele, na mihimili ya kazi ya mbao itarudisha mwangwi wake.
Surely, the stone out of the wall, will make outcry, —and, the tie out of the timber, will answer it.
12 “Ole wake yeye ajengaye mji kwa kumwaga damu na kuusimamisha mji kwa uhalifu!
Alas! for him who buildeth a city with deeds of blood, —and establisheth a town with perversity.
13 Je, Bwana Mwenye Nguvu Zote hakuonyesha kwamba kazi ya wanadamu ni mafuta tu kwa ajili ya moto, na kwamba mataifa yanajichosha bure?
Lo! is it not from Yahweh of hosts—that peoples labour for fire, and, populations, for emptiness, weary themselves?
14 Kwa kuwa dunia itajazwa na maarifa ya utukufu wa Bwana, kama maji yaifunikavyo bahari.
For the earth shall be filled with the knowledge of the glory of Yahweh, —as, the waters, cover the sea.
15 “Ole wake yeye awapaye jirani zake kileo, akiimimina kutoka kwenye kiriba cha mvinyo mpaka wamelewa, ili apate kutazama miili yao iliyo uchi.
Alas! for him who causeth his neighbour to drink, from the goblet of thy fury, and also, making him drunk, —to the end thou mayest gloat over their parts of shame.
16 Utajazwa na aibu badala ya utukufu. Sasa ni zamu yako! Kunywa na ujifunue! Kikombe kutoka kwenye mkono wa kuume wa Bwana kinakujia, na aibu itafunika utukufu wako.
Thou art sated with contempt, more than glory, drink, thou too, and expose thy person, —the cup of the right hand of Yahweh, shall come round unto thee, and ignominious filth be upon thy glory;
17 Ukatili ulioifanyia Lebanoni utakufunika, na uharibifu uliowafanyia wanyama utakutisha. Kwa sababu umemwaga damu ya mtu; umeharibu nchi na miji na kila mmoja aliyeko ndani yake.
For, the violence [done] to Lebanon, shall cover thee, and wasting by wild beasts shall cause them terror, —for shedding Human blood, and doing violence to the earth, to the city, and to all who dwell therein.
18 “Sanamu ina thamani gani, kwani mwanadamu ndiye alichonga? Ama kinyago kinachofundisha uongo? Kwa kuwa yeye aliyekitengeneza hutegemea kazi ya mikono yake mwenyewe; hutengeneza sanamu zisizoweza kuzungumza.
What hath a carved image, profited, though the fashioner thereof, carved it? a molten image, and a teacher of falsehood, —though the fashioner of his fashioned thing trusted therein? that men should make Dumb Nonentities!
19 Ole wake yeye auambiaye mti, ‘Uwe hai!’ Ama asemaye na jiwe lisilo na uhai, ‘Amka!’ Je, linaweza kuongoza? Limefunikwa kwa dhahabu na fedha; hakuna pumzi ndani yake.
Alas! for him who saith to wood, Awake, bestir thee! to a silent stone, he, shall teach! Though he is overlaid with gold and silver, yet, no spirit whatsoever, is in him!
20 Lakini Bwana yuko katika Hekalu lake takatifu; dunia yote na inyamaze mbele yake.”
Howbeit, Yahweh, is in his holy temple, —Hush before him, all the earth.