+ Mwanzo 1 >
1 Hapo mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia.
In the beginning, God created the heavens and the earth.
2 Wakati huu dunia ilikuwa haina umbo, tena ilikuwa tupu. Giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji, naye Roho wa Mungu alikuwa ametulia juu ya maji.
The earth was without form and empty. Darkness was upon the surface of the deep. The Spirit of God was moving above the surface of the waters.
3 Mungu akasema, “Iwepo nuru,” nayo nuru ikawepo.
God said, “Let there be light,” and there was light.
4 Mungu akaona ya kuwa nuru ni njema, ndipo Mungu akatenganisha nuru na giza.
God saw the light, that it was good. He divided the light from the darkness.
5 Mungu akaiita nuru “mchana,” na giza akaliita “usiku.” Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya kwanza.
God called the light “day,” and the darkness he called “night.” This was evening and morning, the first day.
6 Mungu akasema, “Iwepo nafasi kati ya maji igawe maji na maji.”
God said, “Let there be an expanse between the waters, and let it divide the waters from the waters.”
7 Kwa hiyo Mungu akafanya nafasi, akatenganisha maji yaliyo chini ya hiyo nafasi na maji yaliyo juu yake. Ikawa hivyo.
God made the expanse and divided the waters which were under the expanse from the waters which were above the expanse. It was so.
8 Mungu akaiita hiyo nafasi “anga.” Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya pili.
God called the expanse “sky.” This was evening and morning, the second day.
9 Mungu akasema, “Maji yaliyopo chini ya anga na yakusanyike mahali pamoja, pawepo na nchi kavu.” Ikawa hivyo.
God said, “Let the waters under the sky be gathered together to one place, and let the dry land appear.” It was so.
10 Mungu akaiita nchi kavu “ardhi,” nalo lile kusanyiko la maji akaliita “bahari.” Mungu akaona kuwa ni vyema.
God called the dry land “earth,” and the gathered waters he called “seas.” He saw that it was good.
11 Kisha Mungu akasema, “Ardhi na itoe mimea: miche itoayo mbegu, miti juu ya nchi itoayo matunda yenye mbegu ndani yake, kila mmea kulingana na aina zake mbalimbali.” Ikawa hivyo.
God said, “Let the earth sprout vegetation: plants yielding seed and fruit trees bearing fruit whose seed is in the fruit, each according to its own kind.” It was so.
12 Ardhi ikachipua mimea: Mimea itoayo mbegu kulingana na aina zake, na miti itoayo matunda yenye mbegu kulingana na aina zake. Mungu akaona ya kuwa hili ni jema.
The earth produced vegetation, plants producing seed after their kind, and trees bearing fruit whose seed was in it, after their kind. God saw that it was good.
13 Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya tatu.
This was evening and morning, the third day.
14 Mungu akasema, “Iwepo mianga kwenye nafasi ya anga ili itenganishe usiku na mchana, nayo iwe alama ya kutambulisha majira mbalimbali, siku na miaka,
God said, “Let there be lights in the sky to divide the day from the night and let them be as signs, for seasons, for days and years.
15 nayo iwe mianga kwenye nafasi ya anga ya kutia nuru juu ya dunia.” Ikawa hivyo.
Let them be lights in the sky to give light upon the earth.” It was so.
16 Mungu akafanya mianga miwili mikubwa: mwanga mkubwa utawale mchana, na mwanga mdogo utawale usiku. Pia Mungu akafanya nyota.
God made the two great lights, the greater light to rule the day, and the lesser light to rule the night. He made the stars also.
17 Mungu akaiweka katika nafasi ya anga iangaze dunia,
God set them in the sky to give light upon the earth,
18 itawale usiku na mchana, na ikatenganishe nuru na giza. Mungu akaona kuwa hili ni jema.
to rule over the day and over the night, and to divide the light from the darkness. God saw that it was good.
19 Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya nne.
This was evening and morning, the fourth day.
20 Mungu akasema, “Kuwepo na viumbe hai tele kwenye maji, nao ndege waruke juu ya dunia katika nafasi ya anga.”
God said, “Let the waters be filled with great numbers of living creatures, and let birds fly above the earth in the expanse of the sky.”
21 Kwa hiyo Mungu akaumba viumbe wakubwa wa baharini na kila kiumbe hai kiendacho majini kulingana na aina zake, na kila ndege mwenye mabawa kulingana na aina yake. Mungu akaona kuwa hili ni jema.
God created the great sea creatures, as well as every living creature after its kind, creatures that move and which fill the waters everywhere, and every winged bird after its kind. God saw that it was good.
22 Mungu akavibariki, akasema, “Zaeni mwongezeke, mkayajaze maji ya bahari, nao ndege waongezeke katika dunia.”
God blessed them, saying, “Be fruitful and multiply, and fill the waters in the seas. Let birds multiply on the earth.”
23 Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya tano.
This was evening and morning, the fifth day.
24 Mungu akasema, “Ardhi na itoe viumbe hai kulingana na aina zake: wanyama wa kufugwa, viumbe vitambaavyo ardhini na wanyama pori, kila mnyama kulingana na aina yake.” Ikawa hivyo.
God said, “Let the earth produce living creatures, each according to its own kind, livestock, creeping things, and beasts of the earth, each according to its own kind.” It was so.
25 Mungu akafanya wanyama pori kulingana na aina zake, wanyama wa kufugwa kulingana na aina zake, na viumbe vyote vitambaavyo juu ya ardhi kulingana na aina zake. Mungu akaona kuwa hili ni jema.
God made the beasts of the earth after their kind, the livestock after their kinds, and everything that creeps upon the ground after its kind. He saw that it was good.
26 Ndipo Mungu akasema, “Tufanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu, wakatawale juu ya samaki wa baharini na ndege wa angani, juu ya mifugo, juu ya dunia yote, na juu ya viumbe wote watambaao juu ya nchi.”
God said, “Let us make man in our image, after our likeness. Let them have dominion over the fish of the sea, over the birds of the sky, over the livestock, over all the earth, and over every creeping thing that creeps on the earth.”
27 Kwa hiyo Mungu akamuumba mtu kwa mfano wake mwenyewe, kwa mfano wa Mungu alimuumba; mwanaume na mwanamke aliwaumba.
God created man in his own image. In his own image he created him. Male and female he created them.
28 Mungu akawabariki na akawaambia, “Zaeni na mkaongezeke, mkaijaze tena dunia na kuitiisha. Mkatawale samaki wa baharini, ndege wa angani, na kila kiumbe hai kiendacho juu ya ardhi.”
God blessed them and said to them, “Be fruitful, and multiply. Fill the earth, and subdue it. Have dominion over the fish of the sea, over the birds of the sky, and over every living thing that moves upon the earth.”
29 Kisha Mungu akasema, “Nimewapa kila mche utoao mbegu juu ya uso wa dunia yote, na kila mti wenye matunda yenye mbegu ndani yake. Vitakuwa chakula chenu.
God said, “See, I have given you every plant yielding seed which is upon the surface of all the earth, and every tree with fruit which has seed in it. They will be food to you.
30 Nao wanyama wote wa dunia, ndege wote wa angani, na viumbe vyote viendavyo juu ya ardhi: yaani kila kiumbe chenye pumzi ya uhai, ninawapa kila mche wa kijani kuwa chakula.” Ikawa hivyo.
To every beast of the earth, to every bird of the heavens, and to everything that creeps upon the earth, and to every creature that has the breath of life I have given every green plant for food.” It was so.
31 Mungu akaona vyote alivyoumba, na tazama, ilikuwa vizuri sana. Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya sita.
God saw everything that he had made. Behold, it was very good. This was evening and morning, the sixth day.