+ Mwanzo 1 >

1 Hapo mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia.
In the begynnynge God created heaven and erth.
2 Wakati huu dunia ilikuwa haina umbo, tena ilikuwa tupu. Giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji, naye Roho wa Mungu alikuwa ametulia juu ya maji.
The erth was voyde and emptie ad darcknesse was vpon the depe and the spirite of god moved vpon the water
3 Mungu akasema, “Iwepo nuru,” nayo nuru ikawepo.
Than God sayd: let there be lyghte and there was lyghte.
4 Mungu akaona ya kuwa nuru ni njema, ndipo Mungu akatenganisha nuru na giza.
And God sawe the lyghte that it was good: and devyded the lyghte from the darcknesse
5 Mungu akaiita nuru “mchana,” na giza akaliita “usiku.” Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya kwanza.
and called the lyghte daye and the darcknesse nyghte: and so of the evenynge and mornynge was made the fyrst daye
6 Mungu akasema, “Iwepo nafasi kati ya maji igawe maji na maji.”
And God sayd: let there be a fyrmament betwene the waters ad let it devyde the waters a sonder.
7 Kwa hiyo Mungu akafanya nafasi, akatenganisha maji yaliyo chini ya hiyo nafasi na maji yaliyo juu yake. Ikawa hivyo.
Than God made the fyrmament and parted the waters which were vnder the fyrmament from the waters that were above the fyrmament: And it was so.
8 Mungu akaiita hiyo nafasi “anga.” Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya pili.
And God called the fyrmament heaven And so of the evenynge and morninge was made the seconde daye
9 Mungu akasema, “Maji yaliyopo chini ya anga na yakusanyike mahali pamoja, pawepo na nchi kavu.” Ikawa hivyo.
And God sayd let the waters that are vnder heaven gather them selves vnto one place that the drye londe may appere: And it came so to passe.
10 Mungu akaiita nchi kavu “ardhi,” nalo lile kusanyiko la maji akaliita “bahari.” Mungu akaona kuwa ni vyema.
And god called the drye lande the erth and the gatheringe togyther of waters called he the see. And God sawe that it was good
11 Kisha Mungu akasema, “Ardhi na itoe mimea: miche itoayo mbegu, miti juu ya nchi itoayo matunda yenye mbegu ndani yake, kila mmea kulingana na aina zake mbalimbali.” Ikawa hivyo.
And God sayd: let the erth bringe forth herbe and grasse that sowe seed and frutefull trees that bere frute every one in his kynde havynge their seed in them selves vpon the erth. And it came so to passe:
12 Ardhi ikachipua mimea: Mimea itoayo mbegu kulingana na aina zake, na miti itoayo matunda yenye mbegu kulingana na aina zake. Mungu akaona ya kuwa hili ni jema.
ad the erth brought forth herbe and grasse sowenge seed every one in his kynde and trees berynge frute and havynge their seed in the selves every one in his kynde. And God sawe that it was good:
13 Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya tatu.
and the of the evenynge and mornynge was made the thyrde daye.
14 Mungu akasema, “Iwepo mianga kwenye nafasi ya anga ili itenganishe usiku na mchana, nayo iwe alama ya kutambulisha majira mbalimbali, siku na miaka,
Than sayd God: let there be lyghtes in ye firmament of heaven to devyde the daye fro the nyghte that they may be vnto sygnes seasons days and yeares.
15 nayo iwe mianga kwenye nafasi ya anga ya kutia nuru juu ya dunia.” Ikawa hivyo.
And let them be lyghtes in the fyrmament of heave to shyne vpon the erth. and so it was.
16 Mungu akafanya mianga miwili mikubwa: mwanga mkubwa utawale mchana, na mwanga mdogo utawale usiku. Pia Mungu akafanya nyota.
And God made two great lyghtes A greater lyghte to rule the daye and a lesse lyghte to rule the nyghte and he made sterres also.
17 Mungu akaiweka katika nafasi ya anga iangaze dunia,
And God put them in the fyrmament of heaven to shyne vpon the erth
18 itawale usiku na mchana, na ikatenganishe nuru na giza. Mungu akaona kuwa hili ni jema.
and to rule the daye and the nyghte ad to devyde the lyghte from darcknesse. And god sawe yt it was good:
19 Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya nne.
and so of the evenynge ad mornynge was made the fourth daye.
20 Mungu akasema, “Kuwepo na viumbe hai tele kwenye maji, nao ndege waruke juu ya dunia katika nafasi ya anga.”
And God sayd let the water bryng forth creatures that move and have lyfe and foules for to flee over the erth vnder the fyrmament of heaven.
21 Kwa hiyo Mungu akaumba viumbe wakubwa wa baharini na kila kiumbe hai kiendacho majini kulingana na aina zake, na kila ndege mwenye mabawa kulingana na aina yake. Mungu akaona kuwa hili ni jema.
And God created greate whalles and all maner of creatures that lyve and moue which the waters brought forth in their kindes ad all maner of federed foules in their kyndes. And God sawe that it was good:
22 Mungu akavibariki, akasema, “Zaeni mwongezeke, mkayajaze maji ya bahari, nao ndege waongezeke katika dunia.”
and God blessed them saynge. Growe and multiplye ad fyll the waters of the sees and let the foules multiplye vpo the erth.
23 Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya tano.
And so of the evenynge and morninge was made the fyfth daye.
24 Mungu akasema, “Ardhi na itoe viumbe hai kulingana na aina zake: wanyama wa kufugwa, viumbe vitambaavyo ardhini na wanyama pori, kila mnyama kulingana na aina yake.” Ikawa hivyo.
And God sayd: leth the erth bring forth lyvynge creatures in thir kyndes: catell and wormes and beastes of the erth in their kyndes and so it came to passe.
25 Mungu akafanya wanyama pori kulingana na aina zake, wanyama wa kufugwa kulingana na aina zake, na viumbe vyote vitambaavyo juu ya ardhi kulingana na aina zake. Mungu akaona kuwa hili ni jema.
And god made the beastes of the erth in their kyndes and catell in their kyndes ad all maner wormes of the erth in their kyndes: and God sawe that it was good.
26 Ndipo Mungu akasema, “Tufanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu, wakatawale juu ya samaki wa baharini na ndege wa angani, juu ya mifugo, juu ya dunia yote, na juu ya viumbe wote watambaao juu ya nchi.”
And God sayd: let vs make man in oure symilitude ad after oure lycknesse: that he may have rule over the fysh of the see and over the foules of the ayre and over catell and over all the erth and over all wormes that crepe on the erth.
27 Kwa hiyo Mungu akamuumba mtu kwa mfano wake mwenyewe, kwa mfano wa Mungu alimuumba; mwanaume na mwanamke aliwaumba.
And God created man after hys lycknesse after the lycknesse of god created he him: male and female created he them.
28 Mungu akawabariki na akawaambia, “Zaeni na mkaongezeke, mkaijaze tena dunia na kuitiisha. Mkatawale samaki wa baharini, ndege wa angani, na kila kiumbe hai kiendacho juu ya ardhi.”
And God blessed them and God sayd vnto them. Growe and multiplye and fyll the erth and subdue it and have domynyon over the fysh of the see and over the foules of the ayre and over all the beastes that move on the erth.
29 Kisha Mungu akasema, “Nimewapa kila mche utoao mbegu juu ya uso wa dunia yote, na kila mti wenye matunda yenye mbegu ndani yake. Vitakuwa chakula chenu.
And God sayd: se I have geven yow all herbes that sowe seed which are on all the erth and all maner trees that haue frute in them and sowe seed: to be meate for yow
30 Nao wanyama wote wa dunia, ndege wote wa angani, na viumbe vyote viendavyo juu ya ardhi: yaani kila kiumbe chenye pumzi ya uhai, ninawapa kila mche wa kijani kuwa chakula.” Ikawa hivyo.
and for all beastes of the erth and vnto all foules of the ayre and vnto all that crepeth on the erth where in is lyfe that they may haue all maner herbes and grasse for to eate and even so it was.
31 Mungu akaona vyote alivyoumba, na tazama, ilikuwa vizuri sana. Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya sita.
And God behelde al that he had made ad loo they were exceadynge good: and so of the evenynge and mornynge was made the syxth daye

+ Mwanzo 1 >