< Mwanzo 9 >

1 Ndipo Mungu akambariki Noa na wanawe, akiwaambia, “Zaeni mkaongezeke kwa idadi na mkaijaze tena dunia.
Et Dieu bénit Noé et ses fils, et il leur dit: Croissez, multipliez vous, et remplissez la terre.
2 Wanyama wote wa duniani, ndege wote wa angani, kila kiumbe kitambaacho juu ya ardhi, na samaki wote wa baharini wamekabidhiwa mikononi mwenu, nao watawaogopa na kuwahofu.
Soyez la terreur et l’épouvante de tous les animaux de la terre, de tous les oiseaux du ciel et de tout ce qui se meut sur la terre; tous les poissons de la mer ont été mis entre vos mains.
3 Kila kitu chenye uhai kiendacho kitakuwa chakula chenu. Kama vile nilivyowapa mimea mbalimbali, sasa nawapa kila kitu.
Tout ce qui se meut et vit sera votre nourriture: de même que les légumes verts, je vous ai donné toutes ces choses.
4 “Lakini kamwe msile nyama ambayo bado ina damu ya uhai wake, kwa maana damu ni uhai.
Excepté que vous ne mangerez point de chair avec son sang.
5 Hakika damu ya uhai wenu nitaidai. Nitaidai kutoka kwa kila mnyama. Kutoka kwa kila mwanadamu pia nitaidai kwa ajili ya uhai wa mtu mwenzake.
Car le sang de vos âmes, j’en demanderai compte à la main de tous les animaux, et à la main de l’homme, et à la main de son frère, je demanderai compte de l’âme de l’homme.
6 “Yeyote amwagaye damu ya mwanadamu, damu yake itamwagwa na mwanadamu, kwa kuwa katika mfano wa Mungu, Mungu alimuumba mwanadamu.
Quiconque aura répandu le sang de l’homme, son sang sera répandu; car c’est à l’image de Dieu qu’a été fait l’homme.
7 Kuhusu ninyi, zaeni mwongezeke kwa wingi, mzidi katika dunia na kuijaza.”
Pour vous, croissez et multipliez-vous: entrez sur la terre et la remplissez.
8 Ndipo Mungu akamwambia Noa na wanawe pamoja naye:
Dieu dit encore à Noé et à ses fils comme à lui:
9 “Sasa mimi ninaweka Agano langu nanyi, pamoja na uzao wenu baada yenu,
Voilà que moi j’établirai mon alliance avec vous, et avec votre postérité après vous;
10 pia na kila kiumbe hai kilichokuwa pamoja nanyi: Ndege, wanyama wa kufugwa na wanyama wote wa porini, wale wote waliotoka katika safina pamoja nanyi, kila kiumbe hai duniani.
Et avec toute âme vivante, qui est avec vous, tant parmi les oiseaux, que parmi les animaux domestiques, et toutes les bêtes de la terre qui sont sorties de l’arche et tous les animaux de la terre.
11 Ninaweka Agano nanyi: Kamwe uhai hautafutwa tena kwa gharika, kamwe haitakuwepo tena gharika ya kuangamiza dunia.”
J’établirai mon alliance avec vous, et toute chair ne sera plus détruite par les eaux d’un déluge, car il n’y aura plus à l’avenir de déluge ravageant la terre.
12 Mungu akasema, “Hii ni ishara ya Agano ninalofanya kati yangu na ninyi na kila kiumbe hai kilicho pamoja nanyi, Agano kwa vizazi vyote vijavyo:
Dieu dit ensuite: Voilà le signe de l’alliance que j’établis entre moi et vous et toute âme vivante qui est avec vous pour des générations éternelles:
13 Nimeweka upinde wangu wa mvua mawinguni, nao utakuwa ishara ya Agano nifanyalo kati yangu na dunia.
Je placerai mon arc dans les nues, et il sera un signe d’alliance entre moi et la terre.
14 Wakati wowote ninapotanda mawingu juu ya dunia na upinde wa mvua ukijitokeza mawinguni,
Et quand j’aurai couvert le ciel de nuages, mon arc paraîtra dans les nues;
15 nitakumbuka Agano langu kati yangu na ninyi na viumbe vyote vilivyo hai vya kila aina. Kamwe maji hayatakuwa tena gharika ya kuangamiza uhai wote.
Et je me souviendrai de mon alliance avec vous, et avec toute âme vivante qui anime la chair; et il n’y aura plus d’eaux de déluge pour détruire toute chair.
16 Wakati wowote upinde wa mvua unapotokea mawinguni, nitauona na kukumbuka Agano la milele kati ya Mungu na viumbe vyote vilivyo hai vya kila aina duniani.”
L’arc sera donc dans les nues; je le verrai, et je me souviendrai de l’alliance éternelle qui est établie entre Dieu et toute âme vivante de toute chair qui est sur la terre.
17 Hivyo Mungu akamwambia Noa, “Hii ndiyo ishara ya Agano ambalo nimelifanya kati yangu na viumbe vyote vilivyo hai duniani.”
Dieu dit encore à Noé: Voici le signe de l’alliance que j’ai établie entre moi et toute chair sur la terre.
18 Wana wa Noa waliotoka ndani ya safina ni: Shemu, Hamu na Yafethi. (Hamu ndiye alikuwa baba wa Kanaani.)
Les fils de Noé qui sortirent de l’arche, étaient donc Sem, Cham et Japhet: or ce même Cham est le père de Chanaan.
19 Hawa ndio waliokuwa wana watatu wa Noa, kutokana nao watu walienea katika dunia.
Ce sont là les trois fils de Noé, et c’est par eux que toute la race des hommes s’est répandue sur la terre entière.
20 Noa akawa mkulima, akawa mtu wa kwanza kupanda mizabibu.
Noé agriculteur, commença à cultiver la terre, et planta une vigne.
21 Alipokunywa huo mvinyo wake akalewa na akalala uchi kwenye hema lake.
Et ayant bu du vin, il s’enivra et se trouva nu dans sa tente.
22 Hamu, baba wa Kanaani, akauona uchi wa baba yake na kuwaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje.
Lorsque Cham, père de Chanaan, eut vu cela, c’est-à-dire, la nudité de son père, il l’annonça à ses deux frères dehors.
23 Lakini Shemu na Yafethi wakachukua nguo wakaitanda mabegani mwao wote wawili, kisha wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao. Nyuso zao zilielekea upande mwingine ili wasiuone uchi wa baba yao.
Mais Sem et Japhet mirent un manteau sur leurs épaules, et marchant en arrière, ils couvrirent la nudité de leur père; ainsi leurs visages étaient détournés, et ils ne virent pas la nudité de leur père.
24 Noa alipolevuka kutoka kwenye mvinyo wake na kujua lile ambalo mwanawe mdogo kuliko wote alilokuwa amemtendea,
Mais Noé, réveillé de son ivresse, lorsqu’il eut appris ce que lui avait fait son second fils,
25 akasema, “Alaaniwe Kanaani! Atakuwa mtumwa wa chini sana kuliko watumwa wote kwa ndugu zake.”
Dit: Maudit Chanaan! il sera l’esclave des esclaves de ses frères.
26 Pia akasema, “Abarikiwe Bwana, Mungu wa Shemu! Kanaani na awe mtumwa wa Shemu.
Mais il ajouta: Béni le Seigneur, le Dieu de Sem! que Chanaan soit son esclave.
27 Mungu na apanue mipaka ya Yafethi; Yafethi na aishi katika mahema ya Shemu, na Kanaani na awe mtumwa wake.”
Que Dieu donne de l’étendue à Japheth, et qu’il habite dans les tentes de Sem, et que Chanaan soit son esclave.
28 Baada ya gharika Noa aliishi miaka 350.
Or Noé vécut après le déluge trois cent cinquante ans.
29 Noa alikuwa na jumla ya miaka 950, ndipo akafa.
Et tous ses jours accomplirent neuf cent cinquante ans, et il mourut.

< Mwanzo 9 >