< Mwanzo 9 >

1 Ndipo Mungu akambariki Noa na wanawe, akiwaambia, “Zaeni mkaongezeke kwa idadi na mkaijaze tena dunia.
Derpaa velsignede Gud Noa og hans Sønner og sagde til dem: »Bliv frugtbare og mangfoldige og opfyld Jorden!
2 Wanyama wote wa duniani, ndege wote wa angani, kila kiumbe kitambaacho juu ya ardhi, na samaki wote wa baharini wamekabidhiwa mikononi mwenu, nao watawaogopa na kuwahofu.
Frygt for eder og Rædsel for eder skal være over alle Jordens vildtlevende Dyr og alle Himmelens Fugle og i alt, hvad Jorden vrimler med, og i alle Havets Fisk; i eders Haand er de givet!
3 Kila kitu chenye uhai kiendacho kitakuwa chakula chenu. Kama vile nilivyowapa mimea mbalimbali, sasa nawapa kila kitu.
Alt, hvad der rører sig og lever, skal tjene eder til Føde; ligesom de grønne Urter giver jeg eder det alt sammen.
4 “Lakini kamwe msile nyama ambayo bado ina damu ya uhai wake, kwa maana damu ni uhai.
Dog Kød med Sjælen, det er Blodet, maa I ikke spise!
5 Hakika damu ya uhai wenu nitaidai. Nitaidai kutoka kwa kila mnyama. Kutoka kwa kila mwanadamu pia nitaidai kwa ajili ya uhai wa mtu mwenzake.
Men for eders eget Blod kræver jeg Hævn; af ethvert Dyr kræver jeg Hævn for det, og af Menneskene indbyrdes kræver jeg Hævn for Menneskenes Liv.
6 “Yeyote amwagaye damu ya mwanadamu, damu yake itamwagwa na mwanadamu, kwa kuwa katika mfano wa Mungu, Mungu alimuumba mwanadamu.
Om nogen udøser Menneskers Blod, ved Mennesker skal hans Blod udøses, thi i sit Billede gjorde Gud Menneskene.
7 Kuhusu ninyi, zaeni mwongezeke kwa wingi, mzidi katika dunia na kuijaza.”
Men I skal blive frugtbare og mangfoldige! Opfyld Jorden og gør eder til Herre over den!«
8 Ndipo Mungu akamwambia Noa na wanawe pamoja naye:
Derpaa sagde Gud til Noa og hans Sønner:
9 “Sasa mimi ninaweka Agano langu nanyi, pamoja na uzao wenu baada yenu,
»Se, jeg opretter min Pagt med eder og eders Efterkommere efter eder
10 pia na kila kiumbe hai kilichokuwa pamoja nanyi: Ndege, wanyama wa kufugwa na wanyama wote wa porini, wale wote waliotoka katika safina pamoja nanyi, kila kiumbe hai duniani.
og med hvert levende Væsen, som er hos eder, Fuglene, Kvæget og alle Jordens vildtlevende Dyr, alt, hvad der gik ud af Arken, alle Jordens Dyr;
11 Ninaweka Agano nanyi: Kamwe uhai hautafutwa tena kwa gharika, kamwe haitakuwepo tena gharika ya kuangamiza dunia.”
jeg opretter min Pagt med eder og lover, at aldrig mere skal alt Kød udryddes af Flodens Vande, og aldrig mere skal der komme en Vandflod for at ødelægge Jorden!«
12 Mungu akasema, “Hii ni ishara ya Agano ninalofanya kati yangu na ninyi na kila kiumbe hai kilicho pamoja nanyi, Agano kwa vizazi vyote vijavyo:
Fremdeles sagde Gud: »Dette er Tegnet paa den Pagt, jeg til evige Tider opretter mellem mig og eder og hvert levende Væsen, som er hos eder:
13 Nimeweka upinde wangu wa mvua mawinguni, nao utakuwa ishara ya Agano nifanyalo kati yangu na dunia.
Min Bue sætter jeg i Skyen, og den skal være Pagtstegn mellem mig og Jorden!
14 Wakati wowote ninapotanda mawingu juu ya dunia na upinde wa mvua ukijitokeza mawinguni,
Naar jeg trækker Skyer sammen over Jorden, og Buen da viser sig i Skyerne,
15 nitakumbuka Agano langu kati yangu na ninyi na viumbe vyote vilivyo hai vya kila aina. Kamwe maji hayatakuwa tena gharika ya kuangamiza uhai wote.
vil jeg komme den Pagt i Hu, som bestaar mellem mig og eder og hvert levende Væsen, det er alt Kød, og Vandet skal ikke mere blive til en Vandflod, som ødelægger alt Kød.
16 Wakati wowote upinde wa mvua unapotokea mawinguni, nitauona na kukumbuka Agano la milele kati ya Mungu na viumbe vyote vilivyo hai vya kila aina duniani.”
Naar Buen da staar i Skyerne, vil jeg se hen til den og ihukomme den evige Pagt mellem Gud og hvert levende Væsen, det er alt Kød paa Jorden.«
17 Hivyo Mungu akamwambia Noa, “Hii ndiyo ishara ya Agano ambalo nimelifanya kati yangu na viumbe vyote vilivyo hai duniani.”
Og Gud sagde til Noa: »Det er Tegnet paa den Pagt, jeg opretter imellem mig og alt Kød paa Jorden!«
18 Wana wa Noa waliotoka ndani ya safina ni: Shemu, Hamu na Yafethi. (Hamu ndiye alikuwa baba wa Kanaani.)
Noas Sønner, der gik ud af Arken, var Sem, Kam og Jafet; Kam var Fader til Kana'an;
19 Hawa ndio waliokuwa wana watatu wa Noa, kutokana nao watu walienea katika dunia.
det var Noas tre Sønner, og fra dem stammer hele Jordens Befolkning.
20 Noa akawa mkulima, akawa mtu wa kwanza kupanda mizabibu.
Noa var Agerdyrker og den første, der plantede en Vingaard.
21 Alipokunywa huo mvinyo wake akalewa na akalala uchi kwenye hema lake.
Da han nu drak af Vinen, blev han beruset og blottede sig inde i, sit Telt.
22 Hamu, baba wa Kanaani, akauona uchi wa baba yake na kuwaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje.
Da saa Kana'ans Fader Kam sin Faders Blusel og gik ud og fortalte sine Brødre det;
23 Lakini Shemu na Yafethi wakachukua nguo wakaitanda mabegani mwao wote wawili, kisha wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao. Nyuso zao zilielekea upande mwingine ili wasiuone uchi wa baba yao.
men Sem og Jafet tog Kappen, lagde den paa deres Skuldre og gik baglæns ind og tildækkede deres Faders Blusel med bortvendte Ansigter, saa de ikke saa deres Faders Blusel.
24 Noa alipolevuka kutoka kwenye mvinyo wake na kujua lile ambalo mwanawe mdogo kuliko wote alilokuwa amemtendea,
Da Noa vaagnede af sin Rus og fik at vide, hvad hans yngste Søn havde gjort ved ham,
25 akasema, “Alaaniwe Kanaani! Atakuwa mtumwa wa chini sana kuliko watumwa wote kwa ndugu zake.”
sagde han: »Forbandet være Kana'an, Trælles Træl blive han for sine Brødre!«
26 Pia akasema, “Abarikiwe Bwana, Mungu wa Shemu! Kanaani na awe mtumwa wa Shemu.
Fremdeles sagde han: »Lovet være HERREN, Sems Gud, og Kana'an blive hans Træl!
27 Mungu na apanue mipaka ya Yafethi; Yafethi na aishi katika mahema ya Shemu, na Kanaani na awe mtumwa wake.”
Gud skaffe Jafet Plads, at han maa bo i Sems Telte; og Kana'an blive hans Træl!«
28 Baada ya gharika Noa aliishi miaka 350.
Noa levede 350 Aar efter Vandfloden;
29 Noa alikuwa na jumla ya miaka 950, ndipo akafa.
saaledes blev Noas fulde Levetid 950 Aar, og derpaa døde han.

< Mwanzo 9 >