< Mwanzo 9 >
1 Ndipo Mungu akambariki Noa na wanawe, akiwaambia, “Zaeni mkaongezeke kwa idadi na mkaijaze tena dunia.
天主祝福諾厄和他的兒子們說:「你們要滋生繁殖,充滿大地。
2 Wanyama wote wa duniani, ndege wote wa angani, kila kiumbe kitambaacho juu ya ardhi, na samaki wote wa baharini wamekabidhiwa mikononi mwenu, nao watawaogopa na kuwahofu.
地上的各種野獸,天空的各種飛鳥,地上的各種爬蟲和水中的各種游魚,都要對你們表示驚恐畏懼:這一切都已交在你們手中。
3 Kila kitu chenye uhai kiendacho kitakuwa chakula chenu. Kama vile nilivyowapa mimea mbalimbali, sasa nawapa kila kitu.
凡有生命的動物,都可作你們的食物;我將這一切賜給你們,有如以前賜給你們蔬菜一樣;
4 “Lakini kamwe msile nyama ambayo bado ina damu ya uhai wake, kwa maana damu ni uhai.
凡有生命,帶血的肉,你們不可吃;
5 Hakika damu ya uhai wenu nitaidai. Nitaidai kutoka kwa kila mnyama. Kutoka kwa kila mwanadamu pia nitaidai kwa ajili ya uhai wa mtu mwenzake.
並且,我要追討害你們生命的血債:向一切野獸追討,向人,向為弟兄的人,追討人命。
6 “Yeyote amwagaye damu ya mwanadamu, damu yake itamwagwa na mwanadamu, kwa kuwa katika mfano wa Mungu, Mungu alimuumba mwanadamu.
凡流人血的,他的血也要為人所流,因為人是照天主的肖像造的。
7 Kuhusu ninyi, zaeni mwongezeke kwa wingi, mzidi katika dunia na kuijaza.”
你們要生育繁殖,在地上滋生繁衍。」
8 Ndipo Mungu akamwambia Noa na wanawe pamoja naye:
天主對諾厄和他的兒子們說:「
9 “Sasa mimi ninaweka Agano langu nanyi, pamoja na uzao wenu baada yenu,
看,我現在與你們和你們未來的後裔立約,
10 pia na kila kiumbe hai kilichokuwa pamoja nanyi: Ndege, wanyama wa kufugwa na wanyama wote wa porini, wale wote waliotoka katika safina pamoja nanyi, kila kiumbe hai duniani.
並與同你們在一起的一切生物:飛鳥、牲畜和一切地上野獸,即凡由方舟出來的一切地上生物立約。
11 Ninaweka Agano nanyi: Kamwe uhai hautafutwa tena kwa gharika, kamwe haitakuwepo tena gharika ya kuangamiza dunia.”
我與你們立約:凡有血肉的,以後決不再受洪水湮滅,再沒有洪水來毀滅大地。」
12 Mungu akasema, “Hii ni ishara ya Agano ninalofanya kati yangu na ninyi na kila kiumbe hai kilicho pamoja nanyi, Agano kwa vizazi vyote vijavyo:
天主說:「這是我在我與你們以及同你們在一起的一切生物之間,立約的永遠標記:
13 Nimeweka upinde wangu wa mvua mawinguni, nao utakuwa ishara ya Agano nifanyalo kati yangu na dunia.
我把虹霓放在雲間,作我與大地之間立約的標記。
14 Wakati wowote ninapotanda mawingu juu ya dunia na upinde wa mvua ukijitokeza mawinguni,
幾時我興雲遮蓋大地,雲中要出現虹霓,
15 nitakumbuka Agano langu kati yangu na ninyi na viumbe vyote vilivyo hai vya kila aina. Kamwe maji hayatakuwa tena gharika ya kuangamiza uhai wote.
那時我便想起我與你們以及各種屬血肉的生物之間所立的盟約:這樣水就不會再成為洪水,毀滅一切血肉的生物。
16 Wakati wowote upinde wa mvua unapotokea mawinguni, nitauona na kukumbuka Agano la milele kati ya Mungu na viumbe vyote vilivyo hai vya kila aina duniani.”
幾時虹霓在雲間出現,我一看見,就想起在天主與地上各種屬血肉的生物之間所立的永遠盟約。」
17 Hivyo Mungu akamwambia Noa, “Hii ndiyo ishara ya Agano ambalo nimelifanya kati yangu na viumbe vyote vilivyo hai duniani.”
天主對諾厄說:「這就是我在我與地上一切有血肉的生物之間,所立的盟約的標記。」
18 Wana wa Noa waliotoka ndani ya safina ni: Shemu, Hamu na Yafethi. (Hamu ndiye alikuwa baba wa Kanaani.)
諾厄的兒子由方舟出來的,有閃、含、和耶斐特。含是客納罕的父親。
19 Hawa ndio waliokuwa wana watatu wa Noa, kutokana nao watu walienea katika dunia.
這三人是諾厄的兒子;人類就由這三人分布天下。
20 Noa akawa mkulima, akawa mtu wa kwanza kupanda mizabibu.
諾厄原是農夫,遂開始種植葡萄園。
21 Alipokunywa huo mvinyo wake akalewa na akalala uchi kwenye hema lake.
一天他喝酒喝醉了,就在自己的帳幕內脫去了衣服。
22 Hamu, baba wa Kanaani, akauona uchi wa baba yake na kuwaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje.
客納罕的父親含看見了父親赤身露體,遂去告訴外面的兩個兄弟。
23 Lakini Shemu na Yafethi wakachukua nguo wakaitanda mabegani mwao wote wawili, kisha wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao. Nyuso zao zilielekea upande mwingine ili wasiuone uchi wa baba yao.
閃和耶斐特二人於是拿了件外衣,搭在肩上,倒退著走進去,蓋上父親的裸體。他們的臉背著,沒有看見父親的裸體。
24 Noa alipolevuka kutoka kwenye mvinyo wake na kujua lile ambalo mwanawe mdogo kuliko wote alilokuwa amemtendea,
諾厄醒了後,知道了小兒對他作的事,
25 akasema, “Alaaniwe Kanaani! Atakuwa mtumwa wa chini sana kuliko watumwa wote kwa ndugu zake.”
就說:「客納罕是可咒罵的,給兄弟當最下賤的奴隸。」
26 Pia akasema, “Abarikiwe Bwana, Mungu wa Shemu! Kanaani na awe mtumwa wa Shemu.
又說:「上主,閃的天主,應受讚美,客納罕應作他的奴隸。
27 Mungu na apanue mipaka ya Yafethi; Yafethi na aishi katika mahema ya Shemu, na Kanaani na awe mtumwa wake.”
願天主擴展耶斐特,使他住在閃的帳幕內;客納罕應作他的奴隸。」
28 Baada ya gharika Noa aliishi miaka 350.
洪水以後,諾厄又活了三百五十年。
29 Noa alikuwa na jumla ya miaka 950, ndipo akafa.
諾厄共活了九百五十歲死了。