< Mwanzo 9 >
1 Ndipo Mungu akambariki Noa na wanawe, akiwaambia, “Zaeni mkaongezeke kwa idadi na mkaijaze tena dunia.
Hottelah Cathut ni Noah hoi a canaw yawhawinae a poe teh, ahnimouh koe, ca moi khe awh, pungdaw awh nateh, talai van kawi awh.
2 Wanyama wote wa duniani, ndege wote wa angani, kila kiumbe kitambaacho juu ya ardhi, na samaki wote wa baharini wamekabidhiwa mikononi mwenu, nao watawaogopa na kuwahofu.
Talai van moithang, saring phunkuep, kalvan e tava phunkuep, talai van a von hoi kâva e pueng, hoi tui thung e tanga pueng ni nangmouh na taki vaiteh a pâyaw awh han. Hote moithang pueng teh nangmae kut dawk na poe.
3 Kila kitu chenye uhai kiendacho kitakuwa chakula chenu. Kama vile nilivyowapa mimea mbalimbali, sasa nawapa kila kitu.
Kahring ni teh kâroe e pueng nangmouh han rawca lah ao han. Hnopai pueng, anhla kahring pueng totouh na poe awh han.
4 “Lakini kamwe msile nyama ambayo bado ina damu ya uhai wake, kwa maana damu ni uhai.
Hottelah a moi hah a hringnae a thi hoi hmai na cat awh mahoeh.
5 Hakika damu ya uhai wenu nitaidai. Nitaidai kutoka kwa kila mnyama. Kutoka kwa kila mwanadamu pia nitaidai kwa ajili ya uhai wa mtu mwenzake.
Hahoi, nangmae hringnae thi phu teh ka hei han. Tami saring pueng koe ka hei han. Tami tangkuem e hmaunawnghanaw koe, tami e hringnae phu teh ka hei roeroe han.
6 “Yeyote amwagaye damu ya mwanadamu, damu yake itamwagwa na mwanadamu, kwa kuwa katika mfano wa Mungu, Mungu alimuumba mwanadamu.
Apipatethai tami e thi ka palawng e tami teh tami ni thi palawng lah ao van han. Bangkongtetpawiteh, tami teh Cathut ni amae meikalat lah a sak e doeh.
7 Kuhusu ninyi, zaeni mwongezeke kwa wingi, mzidi katika dunia na kuijaza.”
Hateiteh, nangmouh teh ca khe awh nateh pungdaw awh. Talai van vah canaw moi khe awh nateh pungdaw awh telah atipouh.
8 Ndipo Mungu akamwambia Noa na wanawe pamoja naye:
Cathut ni Noah hoi a capanaw koe bout a dei pouh e teh,
9 “Sasa mimi ninaweka Agano langu nanyi, pamoja na uzao wenu baada yenu,
Nangmouh hoi thoseh, nangmae catoun hoi thoseh,
10 pia na kila kiumbe hai kilichokuwa pamoja nanyi: Ndege, wanyama wa kufugwa na wanyama wote wa porini, wale wote waliotoka katika safina pamoja nanyi, kila kiumbe hai duniani.
Nangmouh koe kaawm e kahring e moithang pueng, tava pueng, saring pueng, long thung hoi tâcokhai e saring pueng koe lawkkam ka caksak han.
11 Ninaweka Agano nanyi: Kamwe uhai hautafutwa tena kwa gharika, kamwe haitakuwepo tena gharika ya kuangamiza dunia.”
Nangmouh koe lawkkam ka caksak e teh, tuikamuem lahoi nâtuek hai moithang pueng ka raphoe mahoeh toe. Talai teh tui hoi ka raphoe mahoeh toe telah ati.
12 Mungu akasema, “Hii ni ishara ya Agano ninalofanya kati yangu na ninyi na kila kiumbe hai kilicho pamoja nanyi, Agano kwa vizazi vyote vijavyo:
Cathut ni kai hoi nang rahak, nang koe kaawm e kâroe ni teh kahring e pueng hoi na catounnaw rahak vah ka sak e lawkkam mitnoutnae doeh.
13 Nimeweka upinde wangu wa mvua mawinguni, nao utakuwa ishara ya Agano nifanyalo kati yangu na dunia.
Kaie salumpa hah tâmai dawk ka hruek vaiteh, kai hoi talai rahak lawkkam mitnoutnae lah ao han.
14 Wakati wowote ninapotanda mawingu juu ya dunia na upinde wa mvua ukijitokeza mawinguni,
Kai ni tâmai ka tabo sak navah, tâmai dawk salumpa a kamnue han.
15 nitakumbuka Agano langu kati yangu na ninyi na viumbe vyote vilivyo hai vya kila aina. Kamwe maji hayatakuwa tena gharika ya kuangamiza uhai wote.
Kai hoi nang rahak, kahring ni teh kâroe e pueng koe, ka lawkkam e pou ka pouk vaiteh, saring moithang pueng tuikamuem hoi ka raphoe mahoeh toe.
16 Wakati wowote upinde wa mvua unapotokea mawinguni, nitauona na kukumbuka Agano la milele kati ya Mungu na viumbe vyote vilivyo hai vya kila aina duniani.”
Tâmai dawk salumpa a paham e ka khet vaiteh, Cathut hoi talai van kaawm e kahring e saring moithang pueng rahak vah, yungyoe e lawkkam ka pouk han.
17 Hivyo Mungu akamwambia Noa, “Hii ndiyo ishara ya Agano ambalo nimelifanya kati yangu na viumbe vyote vilivyo hai duniani.”
Hahoi Cathut ni Noah koe, hete teh kai hoi talai van kaawm e moithang saring pueng rahak vah, ka caksak e lawkkam mitnoutnae doeh telah atipouh.
18 Wana wa Noa waliotoka ndani ya safina ni: Shemu, Hamu na Yafethi. (Hamu ndiye alikuwa baba wa Kanaani.)
Long thung hoi a tâco navah Noah e a capanaw teh Shem, Ham, Japheth. Ham teh Kanaan e a na pa lah ao.
19 Hawa ndio waliokuwa wana watatu wa Noa, kutokana nao watu walienea katika dunia.
Ahnimanaw kathum touh teh Noah e a capanaw lah ao teh, ahnimanaw koehoi talai van taminaw a pungdaw.
20 Noa akawa mkulima, akawa mtu wa kwanza kupanda mizabibu.
Noah ni law sak a kamtawng teh, misur takha a sak.
21 Alipokunywa huo mvinyo wake akalewa na akalala uchi kwenye hema lake.
Misurtui hai a nei dawkvah a parui teh tawngtai lah ao.
22 Hamu, baba wa Kanaani, akauona uchi wa baba yake na kuwaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje.
Kanaan e na pa Ham ni a na pa caici lah ao e a hmu teh alawilah kaawm e a hmaunawngha kahni touh koe a dei pouh.
23 Lakini Shemu na Yafethi wakachukua nguo wakaitanda mabegani mwao wote wawili, kisha wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao. Nyuso zao zilielekea upande mwingine ili wasiuone uchi wa baba yao.
Hatei Shem hoi Japheth ni teh hni a la roi teh a loung dawk a thueng roi teh, kâhnawn laihoi a na pa e caicinae teh a ramuk pouh roi. Ahnimouh roi teh alawilah a kangvawi roi dawkvah, a na pa caici lah ao e hah hmawt roi hoeh.
24 Noa alipolevuka kutoka kwenye mvinyo wake na kujua lile ambalo mwanawe mdogo kuliko wote alilokuwa amemtendea,
Noah ni misur parui e a thangcuem torei teh a capa cahnoung e ni a sak e a panue.
25 akasema, “Alaaniwe Kanaani! Atakuwa mtumwa wa chini sana kuliko watumwa wote kwa ndugu zake.”
Hatdawkvah, Kanaan teh thoebo lah awm seh. A hmau roi koe san thung dawk e san lah awm seh.
26 Pia akasema, “Abarikiwe Bwana, Mungu wa Shemu! Kanaani na awe mtumwa wa Shemu.
Hahoi, Shem e BAWIPA Cathut teh yawhawinae awm seh. Kanaan teh ahni koe san lah awm seh.
27 Mungu na apanue mipaka ya Yafethi; Yafethi na aishi katika mahema ya Shemu, na Kanaani na awe mtumwa wake.”
Cathut ni Japheth teh len nateh roung seh. Shem e lukkareiim dawk awm seh. Kanaan teh ahni koe san lah awm seh telah atipouh.
28 Baada ya gharika Noa aliishi miaka 350.
Noah teh tuikamuem a tho hnukkhu kum 350 a hring.
29 Noa alikuwa na jumla ya miaka 950, ndipo akafa.
Noah e a hringnae teh kum 950 touh a pha teh a due.