< Mwanzo 8 >

1 Mungu akamkumbuka Noa na wanyama wote wa porini na wa kufugwa waliokuwa naye ndani ya safina, akatuma upepo ukavuma katika dunia, nayo maji yakaondoka.
Dieu se souvint de Noé, de toutes les bêtes et de tous les animaux domestiques qui étaient avec lui dans l’arche, et Dieu fit passer un vent sur la terre, et les eaux baissèrent;
2 Zile chemchemi zilizo chini sana ya ardhi pamoja na malango ya mafuriko ya mbinguni yakawa yamefungwa nayo mvua ikawa imekoma kunyesha kutoka angani.
les sources de l’abîme et les écluses du ciel se fermèrent, et la pluie cessa de tomber du ciel.
3 Maji yakaendelea kupungua taratibu katika nchi. Kunako mwisho wa siku ya 150, maji yalikuwa yamepungua,
Les eaux se retirèrent de dessus la terre, allant et revenant, et elles s’abaissèrent au bout de cent cinquante jours.
4 katika siku ya kumi na saba ya mwezi wa saba, safina ikatua katika milima ya Ararati.
Au septième mois, le dix-septième jour du mois, l’arche s’arrêta sur les montagnes d’Ararat.
5 Maji yakaendelea kupungua hadi mwezi wa kumi, na siku ya kwanza ya mwezi wa kumi, vilele vya milima vikaonekana.
Les eaux allèrent se retirant jusqu’au dixième mois; et, au dixième mois, le premier jour du mois, apparurent les sommets des montagnes.
6 Baada ya siku arobaini Noa akafungua dirisha alilokuwa amelifanya katika safina
Au bout de quarante jours, Noé ouvrit la fenêtre qu’il avait faite à l’arche,
7 na akamtoa kunguru, akawa akiruka kwenda na kurudi mpaka maji yalipokwisha kukauka juu ya nchi.
et lâcha le corbeau, qui sortit, allant et revenant, jusqu’à ce que les eaux fussent séchées au-dessus de la terre.
8 Kisha akamtoa hua ili aone kama maji yameondoka juu ya uso wa ardhi.
Il lâcha ensuite la colombe d’auprès de lui, pour voir si les eaux avaient diminué de la surface de la terre.
9 Lakini hua hakupata mahali pa kutua kwa kuwa maji yalienea juu ya uso wa dunia yote, kwa hiyo akarudi kwa Noa ndani ya safina. Noa akanyoosha mkono akamchukua yule hua akamrudisha ndani ya safina.
Mais la colombe, n’ayant pas trouvé où poser la plante de son pied, revint vers lui dans l’arche; parce qu’il y avait encore des eaux à la surface de toute la terre. Il étendit la main et, l’ayant prise, il la fit rentrer auprès de lui dans l’arche.
10 Noa akangojea siku saba zaidi kisha akamtoa tena hua kutoka safina.
Il attendit encore sept autres jours, et il lâcha de nouveau la colombe hors de l’arche,
11 Wakati hua aliporejea kwa Noa jioni, alikuwa amechukua katika mdomo wake jani bichi la mzeituni, lililochumwa wakati ule ule! Ndipo Noa akajua ya kuwa maji yameondoka juu ya uso wa dunia.
et la colombe revint vers lui sur le soir, et voici, une feuille d’olivier toute fraîche était dans son bec; et Noé reconnut que les eaux ne couvraient plus la terre.
12 Akangojea siku saba zaidi na akamtuma tena hua, lakini wakati huu hua hakurudi tena kwa Noa.
Il attendit encore sept autres jours, et il lâcha la colombe; et elle ne revint plus vers lui.
13 Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza ya mwaka 601, wa kuishi kwake Noa, maji yalikuwa yamekauka duniani. Kisha Noa akafungua mlango wa safina akaona ya kuwa uso wa ardhi ulikuwa umekauka.
L’an six cent un, au premier mois, le premier jour du mois, les eaux avaient séché sur la terre. Noé ôta la couverture de l’arche et regarda, et voici, la surface du sol avait séché.
14 Katika siku ya ishirini na saba ya mwezi wa pili dunia ilikuwa imekauka kabisa.
Au second mois, le vingt-septième jour du mois, la terre fut sèche.
15 Ndipo Mungu akamwambia Noa,
Alors Dieu parla à Noé, en disant:
16 “Toka ndani ya safina, wewe na mkeo na wanao na wake zao.
« Sors de l’arche, toi et ta femme, tes fils et les femmes de tes fils avec toi.
17 Utoe nje kila aina ya kiumbe hai aliye pamoja nawe: Ndege, wanyama na viumbe vyote vitambaavyo juu ya ardhi, ili wakazae, na kuongezeka na kuijaza tena dunia.”
Toutes les bêtes de toute chair, qui sont avec toi, oiseaux, animaux domestiques, et tous les reptiles qui rampent sur la terre, fais-les sortir avec toi; qu’ils se répandent sur la terre, qu’ils soient féconds et multiplient sur la terre. »
18 Kwa hiyo Noa akatoka nje pamoja na mkewe, wanawe na wake zao.
Noé sortit, lui et ses fils, sa femme et les femmes de ses fils.
19 Wanyama wote na viumbe vyote vitambaavyo juu ya ardhi na ndege wote, kila kitu kiendacho juu ya nchi, aina moja baada ya nyingine vikatoka katika safina, kila aina ya kiumbe, kimoja baada ya kingine.
Toutes les bêtes, tous les reptiles et tous les oiseaux, tous les êtres qui se meuvent sur la terre, selon leurs espèces, sortirent de l’arche.
20 Kisha Noa akamjengea Bwana madhabahu, akachukua baadhi ya wale wanyama na ndege wote walio safi, akatoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu.
Noé construisit un autel à Yahweh et, ayant pris de tous les animaux purs et de tous les oiseaux purs, il offrit des holocaustes sur l’autel.
21 Bwana akasikia harufu nzuri ya kupendeza, naye akasema moyoni mwake, “Kamwe sitailaani tena ardhi kwa sababu ya mwanadamu, hata ingawa kila mwelekeo wa moyo wake ni mbaya tangu ujana. Kamwe sitaangamiza tena viumbe hai vyote kama nilivyofanya.
Yahweh sentit une odeur agréable, et Yahweh dit en son cœur: « Je ne maudirai plus désormais la terre à cause de l’homme, parce que les pensées du cœur de l’homme sont mauvaises dès sa jeunesse, et je ne frapperai plus tout être vivant, comme je l’ai fait.
22 “Kwa muda dunia idumupo, wakati wa kupanda na wa kuvuna, wakati wa baridi na wa joto, wakati wa kiangazi na wa masika, usiku na mchana kamwe havitakoma.”
Désormais, tant que la terre durera, les semailles et la moisson, le froid et le chaud, l’été et l’hiver, le jour et la nuit ne cesseront point. »

< Mwanzo 8 >

A Dove is Sent Forth from the Ark
A Dove is Sent Forth from the Ark