< Mwanzo 7 >
1 Ndipo Bwana akamwambia Noa, “Ingia katika safina wewe na jamaa yako yote, kwa sababu katika kizazi hiki nimeona ya kuwa wewe ni mwenye haki.
Et l'Éternel dit à Noé: Entre, toi et toute ta maison, dans l'arche; car je t'ai vu juste devant moi dans cette génération.
2 Uchukue wanyama saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, na wanyama wawili wawili wa kila aina walio najisi wa kiume na wa kike.
Tu prendras avec toi de tous les animaux purs, sept paires de chaque espèce, le mâle et sa femelle; mais des bêtes qui ne sont pas pures, deux, le mâle et sa femelle.
3 Pia uchukue ndege saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, ili kuhifadhi aina zao mbalimbali katika dunia yote.
Tu prendras aussi des oiseaux des cieux, sept paires, mâle et femelle, pour en conserver la race sur la face de toute la terre.
4 Siku saba kuanzia sasa nitaleta mvua juu ya nchi kwa siku arobaini usiku na mchana, nami nitafutilia mbali kutoka uso wa nchi kila kiumbe hai nilichokiumba.”
Car dans sept jours je ferai pleuvoir sur la terre, pendant quarante jours et quarante nuits; et j'exterminerai de dessus la terre tous les êtres que j'ai faits.
5 Noa akafanya yote kama Bwana alivyomwamuru.
Et Noé fit tout ce que l'Éternel lui avait commandé.
6 Noa alikuwa na miaka 600 gharika ilipokuja juu ya dunia.
Or, Noé était âgé de six cents ans, quand le déluge eut lieu, et que les eaux vinrent sur la terre.
7 Noa na mkewe na wanawe na wake zao wakaingia katika safina ili waepuke ile gharika.
Noé entra donc dans l'arche, et ses fils, sa femme, et les femmes de ses fils avec lui, à cause des eaux du déluge.
8 Jozi ya wanyama walio safi na walio najisi, ndege na viumbe vitambaavyo,
Des animaux purs et des animaux qui ne sont pas purs, et des oiseaux, et de tout ce qui rampe sur la terre,
9 wa kiume na wa kike, walikuja kwa Noa wakaingia katika safina kama Mungu alivyomwamuru Noa.
Deux par deux, mâle et femelle, entrèrent vers Noé dans l'arche, comme Dieu l'avait commandé à Noé.
10 Baada ya siku saba, maji ya gharika yakaja juu ya dunia.
Et il arriva, au bout des sept jours, que les eaux du déluge furent sur la terre.
11 Katika siku ya kumi na saba ya mwezi wa pili mwaka wa 600 wa kuishi kwake Noa, siku hiyo ndipo chemchemi zote hata zilizo chini sana ya ardhi zilibubujika kwa nguvu, na malango ya mafuriko ya mbinguni yakafunguliwa.
En l'an six cent de la vie de Noé, au second mois, au dix-septième jour du mois, en ce jour-là, toutes les sources du grand abîme éclatèrent, et les bondes des cieux s'ouvrirent.
12 Mvua ikanyesha juu ya nchi siku arobaini usiku na mchana.
Et la pluie tomba sur la terre quarante jours et quarante nuits.
13 Siku hiyo Noa, na mkewe, na wanawe Shemu, Hamu na Yafethi pamoja na wake zao wakaingia katika ile safina.
En ce même jour-là, Noé, Sem, Cham et Japhet, fils de Noé, et la femme de Noé, et les trois femmes de ses fils avec eux, entrèrent dans l'arche,
14 Nao walikuwa pamoja na kila mnyama wa mwituni kufuatana na aina yake, wanyama wote wafugwao kufuatana na aina zao, kila kiumbe kitambaacho juu ya ardhi kwa aina yake, na kila ndege kufuatana na aina yake, naam kila kiumbe chenye mabawa.
Eux, et tous les animaux selon leur espèce, et tout le bétail selon son espèce, et tous les reptiles qui rampent sur la terre selon leur espèce, et tous les oiseaux selon leur espèce, tout petit oiseau, tout ce qui a des ailes;
15 Viumbe vyote vyenye pumzi ya uhai ndani yake vikaja kwa Noa viwili viwili, vikaingia katika safina.
Ils entrèrent donc vers Noé dans l'arche; deux par deux, de toute chair qui a souffle de vie.
16 Wanyama walioingia katika safina walikuwa wa kiume na wa kike, wa kila kiumbe chenye uhai kama Mungu alivyomwamuru Noa, ndipo Bwana akamfungia ndani.
Et ceux qui vinrent, vinrent mâle et femelle de toute chair, comme Dieu le lui avait commandé; et l'Éternel ferma l'arche sur lui.
17 Kwa siku arobaini mafuriko yaliendelea kujaa duniani na maji yalivyozidi kuongezeka, yaliinua safina juu sana kutoka kwenye uso wa nchi.
Et le déluge fut quarante jours sur la terre; et les eaux crûrent, et soulevèrent l'arche, et elle s'éleva de dessus la terre.
18 Maji yakajaa na kuongezeka sana juu ya nchi, na safina ikaelea juu ya uso wa maji.
Et les eaux grossirent et crûrent fort sur la terre; et l'arche flottait à la surface des eaux.
19 Maji yakazidi kujaa juu ya nchi, yakaifunika milima yote mirefu chini ya mbingu yote.
Et les eaux grossirent prodigieusement sur la terre; et toutes les hautes montagnes qui sont sous tous les cieux, furent couvertes.
20 Maji yakaendelea kujaa yakaifunika milima kwa kina cha zaidi ya dhiraa kumi na tano.
Les eaux s'élevèrent de quinze coudées au-dessus; et les montagnes furent couvertes.
21 Kila kiumbe hai kitambaacho juu ya nchi kikaangamia: Ndege, wanyama wa kufugwa, wanyama pori, viumbe vyote juu ya nchi na wanadamu wote.
Et toute chair qui se mouvait sur la terre, expira, tant des oiseaux que du bétail, des animaux et de tous les reptiles qui se traînent sur la terre, et tous les hommes.
22 Kila kiumbe juu ya nchi kavu chenye pumzi ya uhai kikafa.
Tout ce qui avait souffle de vie dans ses narines, et tout ce qui était sur la terre ferme, mourut.
23 Kila kitu chenye uhai juu ya uso wa nchi kilifutiliwa mbali, watu, wanyama, viumbe vitambaavyo na ndege warukao angani wakafutiliwa mbali toka duniani. Waliobaki ni Noa peke yake na wale waliokuwa pamoja naye ndani ya safina.
Tous les êtres qui étaient sur la face de la terre furent exterminés, depuis les hommes jusqu'aux bêtes, jusqu'aux reptiles, et jusqu'aux oiseaux des cieux, et ils furent exterminés de dessus la terre. Il ne resta que Noé, et ce qui était avec lui dans l'arche.
24 Maji yakaifunika dunia kwa siku 150.
Et les eaux furent grosses sur la terre pendant cent cinquante jours.