< Mwanzo 7 >

1 Ndipo Bwana akamwambia Noa, “Ingia katika safina wewe na jamaa yako yote, kwa sababu katika kizazi hiki nimeona ya kuwa wewe ni mwenye haki.
Yahvé dit à Noé: « Entre dans le navire avec toute ta famille, car j'ai vu ta justice devant moi, dans cette génération.
2 Uchukue wanyama saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, na wanyama wawili wawili wa kila aina walio najisi wa kiume na wa kike.
Tu prendras avec toi sept couples de chaque animal pur, le mâle et sa femelle. Des animaux qui ne sont pas purs, tu en prendras deux, le mâle et sa femelle.
3 Pia uchukue ndege saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, ili kuhifadhi aina zao mbalimbali katika dunia yote.
Et aussi des oiseaux du ciel, sept et sept, mâle et femelle, pour faire vivre la semence sur la surface de toute la terre.
4 Siku saba kuanzia sasa nitaleta mvua juu ya nchi kwa siku arobaini usiku na mchana, nami nitafutilia mbali kutoka uso wa nchi kila kiumbe hai nilichokiumba.”
En sept jours, je ferai pleuvoir sur la terre pendant quarante jours et quarante nuits. Je détruirai tout être vivant que j'ai créé à la surface de la terre. »
5 Noa akafanya yote kama Bwana alivyomwamuru.
Noé fit tout ce que Yahvé lui avait ordonné.
6 Noa alikuwa na miaka 600 gharika ilipokuja juu ya dunia.
Noé avait six cents ans lorsque le déluge d'eaux vint sur la terre.
7 Noa na mkewe na wanawe na wake zao wakaingia katika safina ili waepuke ile gharika.
Noé monta dans le bateau avec ses fils, sa femme et les femmes de ses fils, à cause du déluge.
8 Jozi ya wanyama walio safi na walio najisi, ndege na viumbe vitambaavyo,
Les animaux purs, les animaux impurs, les oiseaux et tout ce qui rampe sur le sol
9 wa kiume na wa kike, walikuja kwa Noa wakaingia katika safina kama Mungu alivyomwamuru Noa.
allèrent par paires vers Noé dans le bateau, mâle et femelle, comme Dieu l'avait ordonné à Noé.
10 Baada ya siku saba, maji ya gharika yakaja juu ya dunia.
Après les sept jours, les eaux du déluge arrivèrent sur la terre.
11 Katika siku ya kumi na saba ya mwezi wa pili mwaka wa 600 wa kuishi kwake Noa, siku hiyo ndipo chemchemi zote hata zilizo chini sana ya ardhi zilibubujika kwa nguvu, na malango ya mafuriko ya mbinguni yakafunguliwa.
La six centième année de la vie de Noé, au deuxième mois, le dix-septième jour du mois, en ce jour, toutes les sources du grand abîme éclatèrent, et les fenêtres du ciel s'ouvrirent.
12 Mvua ikanyesha juu ya nchi siku arobaini usiku na mchana.
Il pleuvait sur la terre quarante jours et quarante nuits.
13 Siku hiyo Noa, na mkewe, na wanawe Shemu, Hamu na Yafethi pamoja na wake zao wakaingia katika ile safina.
Ce même jour, Noé, Sem, Cham et Japhet, les fils de Noé, ainsi que la femme de Noé et les trois femmes de ses fils avec eux, montèrent dans le navire,
14 Nao walikuwa pamoja na kila mnyama wa mwituni kufuatana na aina yake, wanyama wote wafugwao kufuatana na aina zao, kila kiumbe kitambaacho juu ya ardhi kwa aina yake, na kila ndege kufuatana na aina yake, naam kila kiumbe chenye mabawa.
eux et tous les animaux selon leur espèce, tout le bétail selon son espèce, tous les reptiles qui rampent sur la terre selon leur espèce, et tous les oiseaux selon leur espèce, tous les oiseaux de toute espèce.
15 Viumbe vyote vyenye pumzi ya uhai ndani yake vikaja kwa Noa viwili viwili, vikaingia katika safina.
Des couples de toute chair ayant en eux une haleine de vie montèrent dans le bateau vers Noé.
16 Wanyama walioingia katika safina walikuwa wa kiume na wa kike, wa kila kiumbe chenye uhai kama Mungu alivyomwamuru Noa, ndipo Bwana akamfungia ndani.
Ceux qui entrèrent, entrèrent mâle et femelle de toute chair, comme Dieu l'avait ordonné; puis Yahvé l'enferma.
17 Kwa siku arobaini mafuriko yaliendelea kujaa duniani na maji yalivyozidi kuongezeka, yaliinua safina juu sana kutoka kwenye uso wa nchi.
Le déluge fut quarante jours sur la terre. Les eaux grossirent et soulevèrent le navire, qui s'éleva au-dessus de la terre.
18 Maji yakajaa na kuongezeka sana juu ya nchi, na safina ikaelea juu ya uso wa maji.
Les eaux montèrent et s'élevèrent très haut sur la terre, et le navire flotta à la surface des eaux.
19 Maji yakazidi kujaa juu ya nchi, yakaifunika milima yote mirefu chini ya mbingu yote.
Les eaux s'élevèrent très haut sur la terre. Toutes les hautes montagnes qui étaient sous tout le ciel furent couvertes.
20 Maji yakaendelea kujaa yakaifunika milima kwa kina cha zaidi ya dhiraa kumi na tano.
Les eaux s'élevèrent de quinze coudées, et les montagnes furent couvertes.
21 Kila kiumbe hai kitambaacho juu ya nchi kikaangamia: Ndege, wanyama wa kufugwa, wanyama pori, viumbe vyote juu ya nchi na wanadamu wote.
Toute chair qui se mouvait sur la terre mourut, les oiseaux, le bétail, les animaux, tous les reptiles qui rampent sur la terre, et tous les hommes.
22 Kila kiumbe juu ya nchi kavu chenye pumzi ya uhai kikafa.
Tout ce qui était sur la terre ferme, dans les narines duquel se trouvait le souffle de l'esprit de vie, mourut.
23 Kila kitu chenye uhai juu ya uso wa nchi kilifutiliwa mbali, watu, wanyama, viumbe vitambaavyo na ndege warukao angani wakafutiliwa mbali toka duniani. Waliobaki ni Noa peke yake na wale waliokuwa pamoja naye ndani ya safina.
Tout être vivant qui était à la surface de la terre fut détruit, y compris l'homme, le bétail, les reptiles et les oiseaux du ciel. Ils furent détruits de la terre. Il ne resta que Noé et ceux qui étaient avec lui dans le bateau.
24 Maji yakaifunika dunia kwa siku 150.
Les eaux inondèrent la terre pendant cent cinquante jours.

< Mwanzo 7 >

The Great Flood
The Great Flood