< Mwanzo 7 >

1 Ndipo Bwana akamwambia Noa, “Ingia katika safina wewe na jamaa yako yote, kwa sababu katika kizazi hiki nimeona ya kuwa wewe ni mwenye haki.
Also the Lord seide to Noe, Entre thou and al thin hous in to the schip, for Y seiy thee iust bifore me in this generacioun.
2 Uchukue wanyama saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, na wanyama wawili wawili wa kila aina walio najisi wa kiume na wa kike.
Of alle clene lyuynge beestis thou schalt take bi seuene and bi seuene, male and female; forsothe of vnclene lyuynge beestis thou schalt take bi tweyne and bi tweyne, male and female;
3 Pia uchukue ndege saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, ili kuhifadhi aina zao mbalimbali katika dunia yote.
but also of volatils of heuene thou schalt take, bi seuene and bi seuene, male and female, that her seed be saued on the face of al erthe.
4 Siku saba kuanzia sasa nitaleta mvua juu ya nchi kwa siku arobaini usiku na mchana, nami nitafutilia mbali kutoka uso wa nchi kila kiumbe hai nilichokiumba.”
For yit and aftir seuene daies Y schal reyne on erthe fourti daies and fourti nyytis, and Y schal do awey al substaunce which Y made, fro the face of erthe.
5 Noa akafanya yote kama Bwana alivyomwamuru.
Therfor Noe dide alle thingis whiche the Lord comaundide to hym.
6 Noa alikuwa na miaka 600 gharika ilipokuja juu ya dunia.
And he was of sixe hundrid yeer, whanne the watris of the greet flood flowiden on erthe.
7 Noa na mkewe na wanawe na wake zao wakaingia katika safina ili waepuke ile gharika.
And Noe entride in to the schip, and hise sones, and hise wijf, and the wyues of his sones, entriden with him for the watris of the greet flood.
8 Jozi ya wanyama walio safi na walio najisi, ndege na viumbe vitambaavyo,
And of lyuynge beestis clene and vnclene, and of briddis of heuene, and of ech beeste which is moued on erthe,
9 wa kiume na wa kike, walikuja kwa Noa wakaingia katika safina kama Mungu alivyomwamuru Noa.
bi tweyne and bi tweyne, male and female entriden to Noe in to the schip, as the Lord comaundide to Noe.
10 Baada ya siku saba, maji ya gharika yakaja juu ya dunia.
And whanne seuene daies hadden passid, the watris of the greet flood flowiden on erthe.
11 Katika siku ya kumi na saba ya mwezi wa pili mwaka wa 600 wa kuishi kwake Noa, siku hiyo ndipo chemchemi zote hata zilizo chini sana ya ardhi zilibubujika kwa nguvu, na malango ya mafuriko ya mbinguni yakafunguliwa.
In the sixe hundrid yeer of the lijf of Noe, in the secunde moneth, in the seuententhe dai of the moneth, alle the wellis of the greet see weren brokun, and the wyndowis of heuene weren opened,
12 Mvua ikanyesha juu ya nchi siku arobaini usiku na mchana.
and reyn was maad on erthe fourti daies and fourti nyytis.
13 Siku hiyo Noa, na mkewe, na wanawe Shemu, Hamu na Yafethi pamoja na wake zao wakaingia katika ile safina.
In the ende of that dai Noe entride, and Sem, Cham, and Japheth, hise sones, his wijf, and the wyues of hise sones, entriden with hem into the schip.
14 Nao walikuwa pamoja na kila mnyama wa mwituni kufuatana na aina yake, wanyama wote wafugwao kufuatana na aina zao, kila kiumbe kitambaacho juu ya ardhi kwa aina yake, na kila ndege kufuatana na aina yake, naam kila kiumbe chenye mabawa.
Thei entriden, and ech beeste bi his kynde, and alle werk beestis in her kynde, and ech beeste which is moued on erthe in his kynde, and ech volatil bi his kynde; alle briddis and alle volatils entriden to Noe in to the schip,
15 Viumbe vyote vyenye pumzi ya uhai ndani yake vikaja kwa Noa viwili viwili, vikaingia katika safina.
bi tweyne and bi tweyne of ech fleisch in whiche the spirit of lijf was.
16 Wanyama walioingia katika safina walikuwa wa kiume na wa kike, wa kila kiumbe chenye uhai kama Mungu alivyomwamuru Noa, ndipo Bwana akamfungia ndani.
And tho that entriden, entriden male and female of ech fleisch, as God comaundide to hym. And the Lord encloside hym fro with out-forth.
17 Kwa siku arobaini mafuriko yaliendelea kujaa duniani na maji yalivyozidi kuongezeka, yaliinua safina juu sana kutoka kwenye uso wa nchi.
And the greet flood was maad fourti daies and fourti niytis on erthe, and the watris weren multiplied, and reiseden the schip on hiy fro erthe.
18 Maji yakajaa na kuongezeka sana juu ya nchi, na safina ikaelea juu ya uso wa maji.
The watris flowiden greetli, and filliden alle thingis in the face of erthe. Forsothe the schip was borun on the watris.
19 Maji yakazidi kujaa juu ya nchi, yakaifunika milima yote mirefu chini ya mbingu yote.
And the watris hadden maistrie greetli on erthe, and alle hiye hillis vndur alle heuene weren hilid;
20 Maji yakaendelea kujaa yakaifunika milima kwa kina cha zaidi ya dhiraa kumi na tano.
the watyr was hiyere bi fiftene cubitis ouer the hilis whiche it hilide.
21 Kila kiumbe hai kitambaacho juu ya nchi kikaangamia: Ndege, wanyama wa kufugwa, wanyama pori, viumbe vyote juu ya nchi na wanadamu wote.
And ech fleisch was wastid that was moued on erthe, of briddis, of lyuynge beestis, of vnresonable beestis, and of alle `reptilis that crepen on erthe.
22 Kila kiumbe juu ya nchi kavu chenye pumzi ya uhai kikafa.
Alle men, and alle thingis in whiche the brething of lijf was in erthe, weren deed.
23 Kila kitu chenye uhai juu ya uso wa nchi kilifutiliwa mbali, watu, wanyama, viumbe vitambaavyo na ndege warukao angani wakafutiliwa mbali toka duniani. Waliobaki ni Noa peke yake na wale waliokuwa pamoja naye ndani ya safina.
And God dide awei al substaunce that was on erthe, fro man til to beeste, as wel a crepynge beeste as the briddis of heuene; and tho weren doon awei fro erthe. Forsothe Noe dwellide aloone, and thei that weren with hym in the schip.
24 Maji yakaifunika dunia kwa siku 150.
And the watris of the greet flood ouereyeden the erthe an hundrid and fifti daies.

< Mwanzo 7 >

The Great Flood
The Great Flood