< Mwanzo 7 >

1 Ndipo Bwana akamwambia Noa, “Ingia katika safina wewe na jamaa yako yote, kwa sababu katika kizazi hiki nimeona ya kuwa wewe ni mwenye haki.
And the LORde sayd vnto Noe: goo in to the arcke both thou and all thy houssold. For the haue I sene rightuous before me in thys generacion.
2 Uchukue wanyama saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, na wanyama wawili wawili wa kila aina walio najisi wa kiume na wa kike.
Of all clene beastes take vnto the. vij. of every kynde the male and hys female And of vnclene beastes a payre the male and hys female:
3 Pia uchukue ndege saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, ili kuhifadhi aina zao mbalimbali katika dunia yote.
lykewyse of the byrdes of the ayre vij. of every kynde male and female to save seed vppon all the erth.
4 Siku saba kuanzia sasa nitaleta mvua juu ya nchi kwa siku arobaini usiku na mchana, nami nitafutilia mbali kutoka uso wa nchi kila kiumbe hai nilichokiumba.”
For. vij. dayes hence wyll I send rayne vppo the erth. xl. dayes and. xl. nyghtes and wyll dystroy all maner of thynges that I haue made from of the face of the erth.
5 Noa akafanya yote kama Bwana alivyomwamuru.
And Noe dyd acordynge to all yt the lorde comaunded hym:
6 Noa alikuwa na miaka 600 gharika ilipokuja juu ya dunia.
and Noe was. vi. hundred yere olde when the floud of water came vppon the erth:
7 Noa na mkewe na wanawe na wake zao wakaingia katika safina ili waepuke ile gharika.
and Noe went and his sonnes and his wyfe and his sonnes wyves wyth hym in to the arke from the waters of the floud.
8 Jozi ya wanyama walio safi na walio najisi, ndege na viumbe vitambaavyo,
And of clene beastes and of beastes that ware vnclene and of byrdes and of all that crepeth vppo the erth
9 wa kiume na wa kike, walikuja kwa Noa wakaingia katika safina kama Mungu alivyomwamuru Noa.
came in by cooples of every kynde vnto Noe in to the arke: a male and a female: even as God commaunded Noe.
10 Baada ya siku saba, maji ya gharika yakaja juu ya dunia.
And the seventh daye the waters of the floud came vppon the erth.
11 Katika siku ya kumi na saba ya mwezi wa pili mwaka wa 600 wa kuishi kwake Noa, siku hiyo ndipo chemchemi zote hata zilizo chini sana ya ardhi zilibubujika kwa nguvu, na malango ya mafuriko ya mbinguni yakafunguliwa.
In the. vi. hundred yere of Noes lyfe in the secode moneth in the. xvij daye of the moneth yt same daye were all the founteynes of the grete depe broken vp and the wyndowes of heave were opened
12 Mvua ikanyesha juu ya nchi siku arobaini usiku na mchana.
ad there fell a rayne vpon the erth. xl. dayes and. xl. nyghtes.
13 Siku hiyo Noa, na mkewe, na wanawe Shemu, Hamu na Yafethi pamoja na wake zao wakaingia katika ile safina.
And the selfe same daye went Noe Sem Ham and Iapheth Noes sonnes and Noes wyfe and the. iij. wyues of his sonnes wyth them in to the arke:
14 Nao walikuwa pamoja na kila mnyama wa mwituni kufuatana na aina yake, wanyama wote wafugwao kufuatana na aina zao, kila kiumbe kitambaacho juu ya ardhi kwa aina yake, na kila ndege kufuatana na aina yake, naam kila kiumbe chenye mabawa.
both they and all maner of beastes in their kide and all maner of catell in their kynde and all maner of wormes that crepe vppon the erth in their kynde and all maner of byrdes in there kynde. and all maner off foules what soever had feders.
15 Viumbe vyote vyenye pumzi ya uhai ndani yake vikaja kwa Noa viwili viwili, vikaingia katika safina.
And they came vnto Noe in to the arke by cooples of all flesh yt had breth of lyfe in it.
16 Wanyama walioingia katika safina walikuwa wa kiume na wa kike, wa kila kiumbe chenye uhai kama Mungu alivyomwamuru Noa, ndipo Bwana akamfungia ndani.
And they that came came male ad female of every flesh acordige as God comaunded hym: and ye LORde shytt the dore vppo him
17 Kwa siku arobaini mafuriko yaliendelea kujaa duniani na maji yalivyozidi kuongezeka, yaliinua safina juu sana kutoka kwenye uso wa nchi.
And the floud came. xl. dayes and. xl. nyghtes vppon the erth and the water increased and bare vp the arcke ad it was lifte vp from of the erth
18 Maji yakajaa na kuongezeka sana juu ya nchi, na safina ikaelea juu ya uso wa maji.
And the water prevayled and increased exceadingly vppon the erth: and the arke went vppo he toppe of the waters.
19 Maji yakazidi kujaa juu ya nchi, yakaifunika milima yote mirefu chini ya mbingu yote.
And the waters prevayled excedingly above mesure vppo the erth so that all the hye hylles which are vnder all the partes of heaven were covered:
20 Maji yakaendelea kujaa yakaifunika milima kwa kina cha zaidi ya dhiraa kumi na tano.
eve. xv. cubytes hye prevayled the waters so that the hylles were covered.
21 Kila kiumbe hai kitambaacho juu ya nchi kikaangamia: Ndege, wanyama wa kufugwa, wanyama pori, viumbe vyote juu ya nchi na wanadamu wote.
And all fleshe that moved on the erth bothe birdes catell and beastes perisshed with al that crepte on the erth and all men:
22 Kila kiumbe juu ya nchi kavu chenye pumzi ya uhai kikafa.
so that all that had the breth of liffe in the nostrels of it thorow out all that was on drye lond dyed.
23 Kila kitu chenye uhai juu ya uso wa nchi kilifutiliwa mbali, watu, wanyama, viumbe vitambaavyo na ndege warukao angani wakafutiliwa mbali toka duniani. Waliobaki ni Noa peke yake na wale waliokuwa pamoja naye ndani ya safina.
Thus was destroyed all that was vppo the erth both man beastes wormes and foules of the ayre so that they were destroyed from the erth: save Noe was reserved only and they that were wyth hym in the arke.
24 Maji yakaifunika dunia kwa siku 150.
And the waters prevayled vppon the erth an hundred and fyftye dayes.

< Mwanzo 7 >

The Great Flood
The Great Flood