< Mwanzo 7 >

1 Ndipo Bwana akamwambia Noa, “Ingia katika safina wewe na jamaa yako yote, kwa sababu katika kizazi hiki nimeona ya kuwa wewe ni mwenye haki.
And God said to Noah, "Come with all of your household into the ship, for I have seen your righteousness before me in this generation.
2 Uchukue wanyama saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, na wanyama wawili wawili wa kila aina walio najisi wa kiume na wa kike.
You shall take seven pairs of every clean animal with you, the male and his female. Of the animals that are not clean, take two, the male and his female.
3 Pia uchukue ndege saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, ili kuhifadhi aina zao mbalimbali katika dunia yote.
Also of the clean flying creatures of the sky, seven pairs, a male and a female, and of all the unclean flying creatures, one pair, a male and a female, to preserve their offspring on the surface of all the earth.
4 Siku saba kuanzia sasa nitaleta mvua juu ya nchi kwa siku arobaini usiku na mchana, nami nitafutilia mbali kutoka uso wa nchi kila kiumbe hai nilichokiumba.”
In seven days, I will cause it to rain on the earth for forty days and forty nights. Every living thing that I have made, I will destroy from the surface of the ground."
5 Noa akafanya yote kama Bwana alivyomwamuru.
Noah did everything that God commanded him.
6 Noa alikuwa na miaka 600 gharika ilipokuja juu ya dunia.
Noah was six hundred years old when the flood of waters came on the earth.
7 Noa na mkewe na wanawe na wake zao wakaingia katika safina ili waepuke ile gharika.
Noah went into the ship with his sons, his wife, and his sons' wives, because of the waters of the flood.
8 Jozi ya wanyama walio safi na walio najisi, ndege na viumbe vitambaavyo,
Clean animals, animals that are not clean, flying creatures, and everything that crawls on the ground
9 wa kiume na wa kike, walikuja kwa Noa wakaingia katika safina kama Mungu alivyomwamuru Noa.
went by pairs to Noah into the ship, male and female, as God commanded Noah.
10 Baada ya siku saba, maji ya gharika yakaja juu ya dunia.
It happened after the seven days, that the waters of the flood came on the earth.
11 Katika siku ya kumi na saba ya mwezi wa pili mwaka wa 600 wa kuishi kwake Noa, siku hiyo ndipo chemchemi zote hata zilizo chini sana ya ardhi zilibubujika kwa nguvu, na malango ya mafuriko ya mbinguni yakafunguliwa.
In the six hundredth year of Noah's life, in the second month, on the seventeenth day of the month, on the same day all the fountains of the great deep were burst open, and the floodgates of the sky were opened.
12 Mvua ikanyesha juu ya nchi siku arobaini usiku na mchana.
The rain was on the earth forty days and forty nights.
13 Siku hiyo Noa, na mkewe, na wanawe Shemu, Hamu na Yafethi pamoja na wake zao wakaingia katika ile safina.
In the same day Noah, and Shem, Ham, and Japheth, the sons of Noah, and Noah's wife, and the three wives of his sons with them, entered into the ship;
14 Nao walikuwa pamoja na kila mnyama wa mwituni kufuatana na aina yake, wanyama wote wafugwao kufuatana na aina zao, kila kiumbe kitambaacho juu ya ardhi kwa aina yake, na kila ndege kufuatana na aina yake, naam kila kiumbe chenye mabawa.
they, and every wild animal after its kind, and every tame animal after their kind, every creature that crawls on the earth after its kind, and every flying creature after its kind, everything with wings.
15 Viumbe vyote vyenye pumzi ya uhai ndani yake vikaja kwa Noa viwili viwili, vikaingia katika safina.
They went to Noah into the ship, by pairs of all flesh with the breath of life in them.
16 Wanyama walioingia katika safina walikuwa wa kiume na wa kike, wa kila kiumbe chenye uhai kama Mungu alivyomwamuru Noa, ndipo Bwana akamfungia ndani.
Those who went in, went in male and female of all flesh, as God commanded him; and God shut him in.
17 Kwa siku arobaini mafuriko yaliendelea kujaa duniani na maji yalivyozidi kuongezeka, yaliinua safina juu sana kutoka kwenye uso wa nchi.
The flood was forty days on the earth. The waters increased, and lifted up the ship, and it was lifted up above the earth.
18 Maji yakajaa na kuongezeka sana juu ya nchi, na safina ikaelea juu ya uso wa maji.
The waters prevailed, and increased greatly on the earth; and the ship floated on the surface of the waters.
19 Maji yakazidi kujaa juu ya nchi, yakaifunika milima yote mirefu chini ya mbingu yote.
And the waters rose very high on the earth. And all the high mountains that were under the whole sky were covered.
20 Maji yakaendelea kujaa yakaifunika milima kwa kina cha zaidi ya dhiraa kumi na tano.
The waters rose and covered the highest mountains to a depth of more than twenty-six feet.
21 Kila kiumbe hai kitambaacho juu ya nchi kikaangamia: Ndege, wanyama wa kufugwa, wanyama pori, viumbe vyote juu ya nchi na wanadamu wote.
And all flesh died that moved on the earth, flying creatures, and tame animals, and wild animals, and every creature that crawls on the earth, and all humankind.
22 Kila kiumbe juu ya nchi kavu chenye pumzi ya uhai kikafa.
All in whose nostrils breathed the breath of life, of all that was on the dry land, died.
23 Kila kitu chenye uhai juu ya uso wa nchi kilifutiliwa mbali, watu, wanyama, viumbe vitambaavyo na ndege warukao angani wakafutiliwa mbali toka duniani. Waliobaki ni Noa peke yake na wale waliokuwa pamoja naye ndani ya safina.
Every living thing was destroyed that was on the surface of the ground, including people, animals, crawling creatures, and flying creatures of the sky. They were destroyed from the earth. Only Noah was left, and those who were with him in the ship.
24 Maji yakaifunika dunia kwa siku 150.
The waters prevailed on the earth one hundred fifty days.

< Mwanzo 7 >

The Great Flood
The Great Flood