< Mwanzo 7 >
1 Ndipo Bwana akamwambia Noa, “Ingia katika safina wewe na jamaa yako yote, kwa sababu katika kizazi hiki nimeona ya kuwa wewe ni mwenye haki.
And Jehovah said to Noah, Go into the ark, thou and all thy house; for thee have I seen righteous before me in this generation.
2 Uchukue wanyama saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, na wanyama wawili wawili wa kila aina walio najisi wa kiume na wa kike.
Of all clean beasts thou shalt take to thee by sevens, a male and its female; but of the beasts that are not clean two, a male and its female.
3 Pia uchukue ndege saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, ili kuhifadhi aina zao mbalimbali katika dunia yote.
Also of the fowl of the heavens by sevens, male and female; to keep seed alive on the face of all the earth.
4 Siku saba kuanzia sasa nitaleta mvua juu ya nchi kwa siku arobaini usiku na mchana, nami nitafutilia mbali kutoka uso wa nchi kila kiumbe hai nilichokiumba.”
For in yet seven days I will cause it to rain on the earth forty days and forty nights; and every living being which I have made will I destroy from the ground.
5 Noa akafanya yote kama Bwana alivyomwamuru.
And Noah did according to all that Jehovah had commanded him.
6 Noa alikuwa na miaka 600 gharika ilipokuja juu ya dunia.
And Noah was six hundred years old when the flood of waters was on the earth.
7 Noa na mkewe na wanawe na wake zao wakaingia katika safina ili waepuke ile gharika.
And Noah went in, and his sons, and his wife, and his sons' wives with him, into the ark, because of the waters of the flood.
8 Jozi ya wanyama walio safi na walio najisi, ndege na viumbe vitambaavyo,
Of clean beasts, and of beasts that are not clean, and of fowl, and of everything that creeps on the ground,
9 wa kiume na wa kike, walikuja kwa Noa wakaingia katika safina kama Mungu alivyomwamuru Noa.
there came two and two unto Noah into the ark, male and female, as God had commanded Noah.
10 Baada ya siku saba, maji ya gharika yakaja juu ya dunia.
And it came to pass after seven days that the waters of the flood were on the earth.
11 Katika siku ya kumi na saba ya mwezi wa pili mwaka wa 600 wa kuishi kwake Noa, siku hiyo ndipo chemchemi zote hata zilizo chini sana ya ardhi zilibubujika kwa nguvu, na malango ya mafuriko ya mbinguni yakafunguliwa.
In the six hundredth year of Noah's life, in the second month, on the seventeenth day of the month, on that same day all the fountains of the great deep were broken up, and the windows of heaven were opened.
12 Mvua ikanyesha juu ya nchi siku arobaini usiku na mchana.
And the pour of rain was on the earth forty days and forty nights.
13 Siku hiyo Noa, na mkewe, na wanawe Shemu, Hamu na Yafethi pamoja na wake zao wakaingia katika ile safina.
On the same day went Noah, and Shem and Ham and Japheth, the sons of Noah, and Noah's wife, and the three wives of his sons with them, into the ark;
14 Nao walikuwa pamoja na kila mnyama wa mwituni kufuatana na aina yake, wanyama wote wafugwao kufuatana na aina zao, kila kiumbe kitambaacho juu ya ardhi kwa aina yake, na kila ndege kufuatana na aina yake, naam kila kiumbe chenye mabawa.
they, and every beast after its kind, and all the cattle after their kind, and every creeping thing that creeps on the earth after its kind, and all fowl after its kind — every bird of every wing.
15 Viumbe vyote vyenye pumzi ya uhai ndani yake vikaja kwa Noa viwili viwili, vikaingia katika safina.
And they went to Noah, into the ark, two and two of all flesh, in which was the breath of life.
16 Wanyama walioingia katika safina walikuwa wa kiume na wa kike, wa kila kiumbe chenye uhai kama Mungu alivyomwamuru Noa, ndipo Bwana akamfungia ndani.
And they that came, came male and female of all flesh, as God had commanded him. And Jehovah shut him in.
17 Kwa siku arobaini mafuriko yaliendelea kujaa duniani na maji yalivyozidi kuongezeka, yaliinua safina juu sana kutoka kwenye uso wa nchi.
And the flood was forty days on the earth. And the waters increased, and bore up the ark; and it was lifted up above the earth.
18 Maji yakajaa na kuongezeka sana juu ya nchi, na safina ikaelea juu ya uso wa maji.
And the waters prevailed and increased greatly on the earth; and the ark went on the face of the waters.
19 Maji yakazidi kujaa juu ya nchi, yakaifunika milima yote mirefu chini ya mbingu yote.
And the waters prevailed exceedingly on the earth; and all the high mountains that are under all the heavens were covered.
20 Maji yakaendelea kujaa yakaifunika milima kwa kina cha zaidi ya dhiraa kumi na tano.
Fifteen cubits upward the waters prevailed; and the mountains were covered.
21 Kila kiumbe hai kitambaacho juu ya nchi kikaangamia: Ndege, wanyama wa kufugwa, wanyama pori, viumbe vyote juu ya nchi na wanadamu wote.
And all flesh that moved on the earth expired, fowl as well as cattle, and beasts, and all crawling things which crawl on the earth, and all mankind:
22 Kila kiumbe juu ya nchi kavu chenye pumzi ya uhai kikafa.
everything which had in its nostrils the breath of life, of all that was on the dry [land], died.
23 Kila kitu chenye uhai juu ya uso wa nchi kilifutiliwa mbali, watu, wanyama, viumbe vitambaavyo na ndege warukao angani wakafutiliwa mbali toka duniani. Waliobaki ni Noa peke yake na wale waliokuwa pamoja naye ndani ya safina.
And every living being was destroyed that was on the ground, both man, and cattle, and creeping things, and fowl of the heavens; and they were destroyed from the earth. And Noah alone remained, and what was with him in the ark.
24 Maji yakaifunika dunia kwa siku 150.
And the waters prevailed on the earth a hundred and fifty days.