< Mwanzo 7 >
1 Ndipo Bwana akamwambia Noa, “Ingia katika safina wewe na jamaa yako yote, kwa sababu katika kizazi hiki nimeona ya kuwa wewe ni mwenye haki.
And the Lord said to him: “Enter the ark, you and all your house. For I have seen you to be just in my sight, within this generation.
2 Uchukue wanyama saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, na wanyama wawili wawili wa kila aina walio najisi wa kiume na wa kike.
From all the clean animals, take seven and seven, the male and the female. Yet truly, from animals that are unclean, take two and two, the male and the female.
3 Pia uchukue ndege saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, ili kuhifadhi aina zao mbalimbali katika dunia yote.
But also from the birds of the air, take seven and seven, the male and the female, so that offspring may be saved upon the face of the whole earth.
4 Siku saba kuanzia sasa nitaleta mvua juu ya nchi kwa siku arobaini usiku na mchana, nami nitafutilia mbali kutoka uso wa nchi kila kiumbe hai nilichokiumba.”
For from that point, and after seven days, I will rain upon the earth for forty days and forty nights. And I will wipe away every substance that I have made, from the surface of the earth.”
5 Noa akafanya yote kama Bwana alivyomwamuru.
Therefore, Noah did all things just as the Lord had commanded him.
6 Noa alikuwa na miaka 600 gharika ilipokuja juu ya dunia.
And he was six hundred years old when the waters of the great flood inundated the earth.
7 Noa na mkewe na wanawe na wake zao wakaingia katika safina ili waepuke ile gharika.
And Noah entered into the ark, and his sons, his wife, and the wives of his sons with him, because of the waters of the great flood.
8 Jozi ya wanyama walio safi na walio najisi, ndege na viumbe vitambaavyo,
And from the animals both clean and unclean, and from the birds, and from everything that moves upon the earth,
9 wa kiume na wa kike, walikuja kwa Noa wakaingia katika safina kama Mungu alivyomwamuru Noa.
two by two they were brought into the ark to Noah, male and female, just as the Lord had instructed Noah.
10 Baada ya siku saba, maji ya gharika yakaja juu ya dunia.
And when seven days had passed, the waters of the great flood inundated the earth.
11 Katika siku ya kumi na saba ya mwezi wa pili mwaka wa 600 wa kuishi kwake Noa, siku hiyo ndipo chemchemi zote hata zilizo chini sana ya ardhi zilibubujika kwa nguvu, na malango ya mafuriko ya mbinguni yakafunguliwa.
In the six hundredth year of the life of Noah, in the second month, on the seventeenth day of the month, all the fountains of the great abyss were released, and the floodgates of heaven were opened.
12 Mvua ikanyesha juu ya nchi siku arobaini usiku na mchana.
And rain came upon the earth for forty days and forty nights.
13 Siku hiyo Noa, na mkewe, na wanawe Shemu, Hamu na Yafethi pamoja na wake zao wakaingia katika ile safina.
On the very same day, Noah and his sons, Shem, Ham, and Japheth, and his wife and the three wives of his sons with them, entered the ark.
14 Nao walikuwa pamoja na kila mnyama wa mwituni kufuatana na aina yake, wanyama wote wafugwao kufuatana na aina zao, kila kiumbe kitambaacho juu ya ardhi kwa aina yake, na kila ndege kufuatana na aina yake, naam kila kiumbe chenye mabawa.
They and every animal according to its kind, and all the cattle in their kind, and everything that moves upon the earth in their kind, and every flying thing according to its kind, all the birds and all that can fly,
15 Viumbe vyote vyenye pumzi ya uhai ndani yake vikaja kwa Noa viwili viwili, vikaingia katika safina.
entered the ark to Noah, two by two out of all that is flesh, in which there was the breath of life.
16 Wanyama walioingia katika safina walikuwa wa kiume na wa kike, wa kila kiumbe chenye uhai kama Mungu alivyomwamuru Noa, ndipo Bwana akamfungia ndani.
And those that entered went in male and female, from all that is flesh, just as God had instructed him. And then the Lord closed him in from the outside.
17 Kwa siku arobaini mafuriko yaliendelea kujaa duniani na maji yalivyozidi kuongezeka, yaliinua safina juu sana kutoka kwenye uso wa nchi.
And the great flood occurred for forty days upon the earth. And the waters were increased, and they lifted the ark high above the land.
18 Maji yakajaa na kuongezeka sana juu ya nchi, na safina ikaelea juu ya uso wa maji.
For they overflowed greatly, and they filled everything on the surface of the earth. And then the ark was carried across the waters.
19 Maji yakazidi kujaa juu ya nchi, yakaifunika milima yote mirefu chini ya mbingu yote.
And the waters prevailed beyond measure across the earth. And all the lofty mountains under the whole heaven were covered.
20 Maji yakaendelea kujaa yakaifunika milima kwa kina cha zaidi ya dhiraa kumi na tano.
The water was fifteen cubits higher than the mountains which it covered.
21 Kila kiumbe hai kitambaacho juu ya nchi kikaangamia: Ndege, wanyama wa kufugwa, wanyama pori, viumbe vyote juu ya nchi na wanadamu wote.
And all flesh was consumed which moved upon the earth: flying things, animals, wild beasts, and all moving things that crawl upon the ground. And all men,
22 Kila kiumbe juu ya nchi kavu chenye pumzi ya uhai kikafa.
and everything in which there is the breath of life on earth, died.
23 Kila kitu chenye uhai juu ya uso wa nchi kilifutiliwa mbali, watu, wanyama, viumbe vitambaavyo na ndege warukao angani wakafutiliwa mbali toka duniani. Waliobaki ni Noa peke yake na wale waliokuwa pamoja naye ndani ya safina.
And he wiped away all substance that was upon the earth, from man to animal, the crawling things just as much as the flying things of the air. And they were wiped away from the earth. But only Noah remained, and those who were with him in the ark.
24 Maji yakaifunika dunia kwa siku 150.
And the waters possessed the earth for one hundred and fifty days.