< Mwanzo 6 >

1 Watu walipoanza kuongezeka idadi katika uso wa dunia na watoto wa kike wakazaliwa kwao,
Lorsque les hommes commencèrent à se multiplier sur la surface de la terre et que des filles leur naquirent,
2 wana wa Mungu wakawaona kuwa hao binti za wanadamu walikuwa wazuri wa sura, wakaoa yeyote miongoni mwao waliyemchagua.
les fils de Dieu virent que les filles des hommes étaient belles, et ils prirent pour femmes toutes celles qu'ils voulurent.
3 Ndipo Bwana akasema, “Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye ni wa kufa, siku zake zitakuwa miaka 120.”
Yahvé dit: « Mon Esprit ne luttera pas toujours avec l'homme, car lui aussi est chair; aussi ses jours seront-ils de cent vingt ans. »
4 Wanefili walikuwako duniani siku hizo, na baadaye, hao wana wa Mungu walipoingia kwa binti za wanadamu na kuzaa nao. Wanefili walikuwa mashujaa na watu waliojulikana wa zamani hizo.
Les Nephilim étaient sur la terre en ces jours-là, et aussi après, lorsque les fils de Dieu s'approchèrent des filles des hommes et eurent des enfants avec elles. Ce sont les hommes puissants d'autrefois, les hommes de renom.
5 Bwana akaona jinsi uovu wa mwanadamu ulivyokuwa mkubwa duniani, na ya kuwa kila mwelekeo wa mawazo ya moyo wake wakati wote ulikuwa mbaya tu.
L'Éternel vit que la méchanceté de l'homme était grande sur la terre, et que toutes les imaginations des pensées du cœur de l'homme étaient continuellement mauvaises.
6 Bwana akasikitika kwamba alimuumba mwanadamu duniani, moyo wa Mungu ukajaa masikitiko.
L'Éternel se désolait d'avoir créé l'homme sur la terre, et cela lui faisait de la peine dans son cœur.
7 Kwa hiyo Bwana akasema, “Nitamfutilia mbali mwanadamu niliyemuumba kutoka kwenye uso wa dunia, wanadamu na wanyama, pamoja na viumbe vitambaavyo na ndege wa angani. Kwa maana nasikitika kuwaumba.”
Yahvé dit: « Je vais détruire l'homme que j'ai créé sur la surface de la terre, l'homme, les animaux, les reptiles et les oiseaux du ciel, car je suis désolé de les avoir créés. »
8 Lakini Noa akapata kibali machoni pa Bwana.
Mais Noé trouva grâce aux yeux de Yahvé.
9 Hivi ndivyo vizazi vya Noa. Noa alikuwa mtu wa haki, na mkamilifu miongoni mwa watu wa wakati wake, tena alitembea na Mungu.
Voici l'histoire des générations de Noé: Noé était un homme juste, irréprochable parmi les gens de son temps. Noé marchait avec Dieu.
10 Noa alikuwa na wana watatu: Shemu, Hamu na Yafethi.
Noé est devenu le père de trois fils: Sem, Cham et Japhet.
11 Wakati huu dunia ilikuwa imejaa uharibifu na ukatili machoni pa Mungu.
La terre était corrompue devant Dieu, et la terre était remplie de violence.
12 Mungu akaona jinsi dunia ilivyoharibika, kwa maana watu wote duniani walikuwa wameharibu njia zao.
Dieu regarda la terre et vit qu'elle était corrompue, car toute chair avait corrompu sa voie sur la terre.
13 Kwa hiyo Mungu akamwambia Noa, “Nitawaangamiza watu wote, kwa kuwa dunia imejaa ukatili kwa sababu yao. Hakika mimi nitaangamiza watu pamoja na dunia.
Dieu dit à Noé: « Je vais faire disparaître toute chair, car la terre est remplie de violence par elle. Voici que je vais les détruire, eux et la terre.
14 Kwa hiyo jitengenezee safina kubwa kwa mbao za mvinje, tengeneza vyumba ndani yake na uipake lami ndani na nje.
Fais un navire en bois de gopher. Tu feras des chambres dans le navire, et tu le scelleras de poix à l'intérieur et à l'extérieur.
15 Hivi ndivyo utakavyoitengeneza: Safina iwe na urefu wa dhiraa 300, upana wake dhiraa hamsini na kimo chake dhiraa thelathini.
Voici comment tu le feras. La longueur du navire sera de trois cents coudées, sa largeur de cinquante coudées et sa hauteur de trente coudées.
16 Itengenezee paa na umalizie safina kwa kuacha nafasi ya dhiraa moja juu. Weka mlango ubavuni mwa safina, na uifanye ya ghorofa ya chini, ya kati na ya juu.
Tu feras un toit dans le navire, et tu l'achèveras jusqu'à une coudée en haut. Tu placeras la porte du navire sur son côté. Tu le feras avec un premier, un deuxième et un troisième étage.
17 Nitaleta gharika ya maji juu ya nchi ili kuangamiza uhai wote chini ya mbingu, kila kiumbe chenye pumzi ya uhai ndani yake. Kila kitu juu ya nchi kitaangamia.
Moi, je ferai venir le déluge d'eau sur cette terre, pour détruire toute chair ayant souffle de vie sous le ciel. Tout ce qui est sur la terre mourra.
18 Lakini Mimi nitaweka Agano langu na wewe, nawe utaingia ndani ya Safina, wewe pamoja na mke wako, wanao na wake zao.
Mais j'établirai mon alliance avec vous. Vous monterez dans le navire, toi, tes fils, ta femme et les femmes de tes fils avec toi.
19 Utaingiza ndani ya Safina kila aina ya kiumbe hai wawili wawili, wa kiume na wa kike, ili kuwahifadhi hai pamoja na wewe.
De tous les êtres vivants de toute chair, tu en feras entrer deux dans le navire, pour les garder en vie avec toi. Ils seront mâle et femelle.
20 Wawili wa kila aina ya ndege, wa kila aina ya mnyama na wa kila aina ya kitambaacho ardhini watakuja kwako ili wahifadhiwe hai.
Des oiseaux selon leur espèce, du bétail selon son espèce, de tout reptile du sol selon son espèce, deux de chaque espèce viendront à toi, pour les garder en vie.
21 Utachukua kila aina ya chakula kitakacholiwa, na ukiweke akiba kama chakula kwa ajili yako na yao.”
Prends avec toi une partie de tout ce qui se mange, et ramasse-le pour toi; cela te servira de nourriture, à toi et à eux. »
22 Noa akafanya kila kitu kama vile Mungu alivyomwamuru.
Noé fit ainsi. Il fit tout ce que Dieu lui avait ordonné.

< Mwanzo 6 >

The World is Destroyed by Water
The World is Destroyed by Water