< Mwanzo 6 >
1 Watu walipoanza kuongezeka idadi katika uso wa dunia na watoto wa kike wakazaliwa kwao,
And it cometh to pass that mankind have begun to multiply on the face of the ground, and daughters have been born to them,
2 wana wa Mungu wakawaona kuwa hao binti za wanadamu walikuwa wazuri wa sura, wakaoa yeyote miongoni mwao waliyemchagua.
and sons of God see the daughters of men that they [are] fair, and they take to themselves women of all whom they have chosen.
3 Ndipo Bwana akasema, “Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye ni wa kufa, siku zake zitakuwa miaka 120.”
And Jehovah saith, 'My Spirit doth not strive in man — to the age; in their erring they [are] flesh:' and his days have been an hundred and twenty years.
4 Wanefili walikuwako duniani siku hizo, na baadaye, hao wana wa Mungu walipoingia kwa binti za wanadamu na kuzaa nao. Wanefili walikuwa mashujaa na watu waliojulikana wa zamani hizo.
The fallen ones were in the earth in those days, and even afterwards when sons of God come in unto daughters of men, and they have borne to them — they [are] the heroes, who, from of old, [are] the men of name.
5 Bwana akaona jinsi uovu wa mwanadamu ulivyokuwa mkubwa duniani, na ya kuwa kila mwelekeo wa mawazo ya moyo wake wakati wote ulikuwa mbaya tu.
And Jehovah seeth that abundant [is] the wickedness of man in the earth, and every imagination of the thoughts of his heart only evil all the day;
6 Bwana akasikitika kwamba alimuumba mwanadamu duniani, moyo wa Mungu ukajaa masikitiko.
and Jehovah repenteth that He hath made man in the earth, and He grieveth Himself — unto His heart.
7 Kwa hiyo Bwana akasema, “Nitamfutilia mbali mwanadamu niliyemuumba kutoka kwenye uso wa dunia, wanadamu na wanyama, pamoja na viumbe vitambaavyo na ndege wa angani. Kwa maana nasikitika kuwaumba.”
And Jehovah saith, 'I wipe away man whom I have prepared from off the face of the ground, from man unto beast, unto creeping thing, and unto fowl of the heavens, for I have repented that I have made them.'
8 Lakini Noa akapata kibali machoni pa Bwana.
And Noah found grace in the eyes of Jehovah.
9 Hivi ndivyo vizazi vya Noa. Noa alikuwa mtu wa haki, na mkamilifu miongoni mwa watu wa wakati wake, tena alitembea na Mungu.
These [are] births of Noah: Noah [is] a righteous man; perfect he hath been among his generations; with God hath Noah walked habitually.
10 Noa alikuwa na wana watatu: Shemu, Hamu na Yafethi.
And Noah begetteth three sons, Shem, Ham, and Japheth.
11 Wakati huu dunia ilikuwa imejaa uharibifu na ukatili machoni pa Mungu.
And the earth is corrupt before God, and the earth is filled [with] violence.
12 Mungu akaona jinsi dunia ilivyoharibika, kwa maana watu wote duniani walikuwa wameharibu njia zao.
And God seeth the earth, and lo, it hath been corrupted, for all flesh hath corrupted its way on the earth.
13 Kwa hiyo Mungu akamwambia Noa, “Nitawaangamiza watu wote, kwa kuwa dunia imejaa ukatili kwa sababu yao. Hakika mimi nitaangamiza watu pamoja na dunia.
And God said to Noah, 'An end of all flesh hath come before Me, for the earth hath been full of violence from their presence; and lo, I am destroying them with the earth.
14 Kwa hiyo jitengenezee safina kubwa kwa mbao za mvinje, tengeneza vyumba ndani yake na uipake lami ndani na nje.
'Make for thyself an ark of gopher-wood; rooms dost thou make with the ark, and thou hast covered it within and without with cypress;
15 Hivi ndivyo utakavyoitengeneza: Safina iwe na urefu wa dhiraa 300, upana wake dhiraa hamsini na kimo chake dhiraa thelathini.
and this [is] that which thou dost with it: three hundred cubits [is] the length of the ark, fifty cubits its breadth, and thirty cubits its height;
16 Itengenezee paa na umalizie safina kwa kuacha nafasi ya dhiraa moja juu. Weka mlango ubavuni mwa safina, na uifanye ya ghorofa ya chini, ya kati na ya juu.
a window dost thou make for the ark, and unto a cubit thou dost restrain it from above; and the opening of the ark thou dost put in its side, — lower, second, and third [stories] dost thou make it.
17 Nitaleta gharika ya maji juu ya nchi ili kuangamiza uhai wote chini ya mbingu, kila kiumbe chenye pumzi ya uhai ndani yake. Kila kitu juu ya nchi kitaangamia.
'And I, lo, I am bringing in the deluge of waters on the earth to destroy all flesh, in which [is] a living spirit, from under the heavens; all that [is] in the earth doth expire.
18 Lakini Mimi nitaweka Agano langu na wewe, nawe utaingia ndani ya Safina, wewe pamoja na mke wako, wanao na wake zao.
'And I have established My covenant with thee, and thou hast come in unto the ark, thou, and thy sons, and thy wife, and thy son's wives with thee;
19 Utaingiza ndani ya Safina kila aina ya kiumbe hai wawili wawili, wa kiume na wa kike, ili kuwahifadhi hai pamoja na wewe.
and of all that liveth, of all flesh, two of every [sort] thou dost bring in unto the ark, to keep alive with thee; male and female are they.
20 Wawili wa kila aina ya ndege, wa kila aina ya mnyama na wa kila aina ya kitambaacho ardhini watakuja kwako ili wahifadhiwe hai.
Of the fowl after its kind, and of the cattle after their kind, of every creeping thing of the ground after its kind, two of every [sort] they come in unto thee, to keep alive.
21 Utachukua kila aina ya chakula kitakacholiwa, na ukiweke akiba kama chakula kwa ajili yako na yao.”
'And thou, take to thyself of all food that is eaten; and thou hast gathered unto thyself, and it hath been to thee and to them for food.'
22 Noa akafanya kila kitu kama vile Mungu alivyomwamuru.
And Noah doth according to all that God hath commanded him; so hath he done.