< Mwanzo 6 >

1 Watu walipoanza kuongezeka idadi katika uso wa dunia na watoto wa kike wakazaliwa kwao,
It came about when mankind began to multiply on the earth and daughters were born to them,
2 wana wa Mungu wakawaona kuwa hao binti za wanadamu walikuwa wazuri wa sura, wakaoa yeyote miongoni mwao waliyemchagua.
that the sons of God saw that the daughters of mankind were attractive. They took for themselves wives, any of them that they chose.
3 Ndipo Bwana akasema, “Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye ni wa kufa, siku zake zitakuwa miaka 120.”
Yahweh said, “My spirit will not remain in mankind forever, for they are flesh. They will live 120 years.”
4 Wanefili walikuwako duniani siku hizo, na baadaye, hao wana wa Mungu walipoingia kwa binti za wanadamu na kuzaa nao. Wanefili walikuwa mashujaa na watu waliojulikana wa zamani hizo.
Giants were on the earth in those days, and also afterward. This happened when the sons of God married daughters of men, and they had children with them. These were the mighty men of old, men of renown.
5 Bwana akaona jinsi uovu wa mwanadamu ulivyokuwa mkubwa duniani, na ya kuwa kila mwelekeo wa mawazo ya moyo wake wakati wote ulikuwa mbaya tu.
Yahweh saw that the wickedness of mankind was great in the earth, and that every inclination of the thoughts of their hearts was only evil continually.
6 Bwana akasikitika kwamba alimuumba mwanadamu duniani, moyo wa Mungu ukajaa masikitiko.
Yahweh regretted that he had made mankind on the earth, and it grieved him to his heart.
7 Kwa hiyo Bwana akasema, “Nitamfutilia mbali mwanadamu niliyemuumba kutoka kwenye uso wa dunia, wanadamu na wanyama, pamoja na viumbe vitambaavyo na ndege wa angani. Kwa maana nasikitika kuwaumba.”
So Yahweh said, “I will wipe away mankind whom I have created from the surface of the earth; both mankind and the larger animals, and creeping things and birds of the heavens, for I am sorry that I have made them.”
8 Lakini Noa akapata kibali machoni pa Bwana.
But Noah found favor in the eyes of Yahweh.
9 Hivi ndivyo vizazi vya Noa. Noa alikuwa mtu wa haki, na mkamilifu miongoni mwa watu wa wakati wake, tena alitembea na Mungu.
These were the events concerning Noah. Noah was a righteous man, and blameless among the people of his time. Noah walked with God.
10 Noa alikuwa na wana watatu: Shemu, Hamu na Yafethi.
Noah became the father of three sons: Shem, Ham, and Japheth.
11 Wakati huu dunia ilikuwa imejaa uharibifu na ukatili machoni pa Mungu.
The earth was corrupt before God, and it was filled with violence.
12 Mungu akaona jinsi dunia ilivyoharibika, kwa maana watu wote duniani walikuwa wameharibu njia zao.
God saw the earth; behold, it was corrupt, for all flesh had corrupted their way upon the earth.
13 Kwa hiyo Mungu akamwambia Noa, “Nitawaangamiza watu wote, kwa kuwa dunia imejaa ukatili kwa sababu yao. Hakika mimi nitaangamiza watu pamoja na dunia.
God said to Noah, “I can see that it is time to put an end to all flesh, for the earth is filled with violence through them. Indeed, I will destroy them with the earth.
14 Kwa hiyo jitengenezee safina kubwa kwa mbao za mvinje, tengeneza vyumba ndani yake na uipake lami ndani na nje.
Make for yourself an ark of cypress wood. Make rooms in the ark, and cover it with pitch within and without.
15 Hivi ndivyo utakavyoitengeneza: Safina iwe na urefu wa dhiraa 300, upana wake dhiraa hamsini na kimo chake dhiraa thelathini.
This is how you will make it: The length of the ark is to be three hundred cubits; the breadth of it is to be fifty cubits, and the height of it is to be thirty cubits.
16 Itengenezee paa na umalizie safina kwa kuacha nafasi ya dhiraa moja juu. Weka mlango ubavuni mwa safina, na uifanye ya ghorofa ya chini, ya kati na ya juu.
Make a roof for the ark, and finish it at a cubit from the top of the side. Place a door in the side of the ark and make a lower, a second, and a third deck.
17 Nitaleta gharika ya maji juu ya nchi ili kuangamiza uhai wote chini ya mbingu, kila kiumbe chenye pumzi ya uhai ndani yake. Kila kitu juu ya nchi kitaangamia.
Listen, I am about to bring the flood of waters upon the earth, to destroy all flesh that has in it the breath of life from under heaven. Everything that is on the earth will die.
18 Lakini Mimi nitaweka Agano langu na wewe, nawe utaingia ndani ya Safina, wewe pamoja na mke wako, wanao na wake zao.
But I will establish my covenant with you. You will come into the ark, you, and your sons, and your wife, and your sons' wives with you.
19 Utaingiza ndani ya Safina kila aina ya kiumbe hai wawili wawili, wa kiume na wa kike, ili kuwahifadhi hai pamoja na wewe.
Of every living creature of all flesh, two of every kind you must bring into the ark, to keep them alive with you, both male and female.
20 Wawili wa kila aina ya ndege, wa kila aina ya mnyama na wa kila aina ya kitambaacho ardhini watakuja kwako ili wahifadhiwe hai.
Of the birds after their kind, and of the larger animals after their kind, of every creeping thing of the ground after its kind, two of every sort will come to you, to keep them alive.
21 Utachukua kila aina ya chakula kitakacholiwa, na ukiweke akiba kama chakula kwa ajili yako na yao.”
Gather for yourself every kind of food that is eaten and store it, so that it will be food for you and for them.”
22 Noa akafanya kila kitu kama vile Mungu alivyomwamuru.
So Noah did this. According to all that God commanded him, so he did.

< Mwanzo 6 >

The World is Destroyed by Water
The World is Destroyed by Water