< Mwanzo 6 >
1 Watu walipoanza kuongezeka idadi katika uso wa dunia na watoto wa kike wakazaliwa kwao,
And it was that began humankind to become numerous on [the] surface of the ground and daughters they were born to them.
2 wana wa Mungu wakawaona kuwa hao binti za wanadamu walikuwa wazuri wa sura, wakaoa yeyote miongoni mwao waliyemchagua.
And they saw [the] sons of God [the] daughters of humankind that [were] good they and they took for themselves wives from all whom they chose.
3 Ndipo Bwana akasema, “Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye ni wa kufa, siku zake zitakuwa miaka 120.”
And he said Yahweh not will remain spirit my in humankind for ever in that also he [is] flesh and they will be days his one hundred and twenty year[s].
4 Wanefili walikuwako duniani siku hizo, na baadaye, hao wana wa Mungu walipoingia kwa binti za wanadamu na kuzaa nao. Wanefili walikuwa mashujaa na watu waliojulikana wa zamani hizo.
The Nephilim they were on the earth in the days those and also after thus when they went [the] sons of God into [the] daughters of humankind and they bore children to them they [were] the mighty [men] who [were] from long ago [the] men of name.
5 Bwana akaona jinsi uovu wa mwanadamu ulivyokuwa mkubwa duniani, na ya kuwa kila mwelekeo wa mawazo ya moyo wake wakati wote ulikuwa mbaya tu.
And he saw Yahweh that [was] great [the] evil of humankind on the earth and every inclination of [the] thoughts of heart his only [was] evil every day.
6 Bwana akasikitika kwamba alimuumba mwanadamu duniani, moyo wa Mungu ukajaa masikitiko.
And he regretted Yahweh that he had made humankind on the earth and he was pained to heart his.
7 Kwa hiyo Bwana akasema, “Nitamfutilia mbali mwanadamu niliyemuumba kutoka kwenye uso wa dunia, wanadamu na wanyama, pamoja na viumbe vitambaavyo na ndege wa angani. Kwa maana nasikitika kuwaumba.”
And he said Yahweh I will wipe humankind which I created from on [the] surface of the ground from humankind unto animal[s] unto creeping thing[s] and unto [the] bird[s] of the heavens for I regret that I have made them.
8 Lakini Noa akapata kibali machoni pa Bwana.
And Noah he found favor in [the] eyes of Yahweh.
9 Hivi ndivyo vizazi vya Noa. Noa alikuwa mtu wa haki, na mkamilifu miongoni mwa watu wa wakati wake, tena alitembea na Mungu.
These [are] [the] accounts of Noah Noah [was] a man righteous blameless he was in generations his with God he walked about Noah.
10 Noa alikuwa na wana watatu: Shemu, Hamu na Yafethi.
And he fathered Noah three sons Shem Ham and Japheth.
11 Wakati huu dunia ilikuwa imejaa uharibifu na ukatili machoni pa Mungu.
And was corrupt the earth before God and was filled the earth violence.
12 Mungu akaona jinsi dunia ilivyoharibika, kwa maana watu wote duniani walikuwa wameharibu njia zao.
And he saw God the earth and there! it was corrupt for had corrupted all flesh way its on the earth.
13 Kwa hiyo Mungu akamwambia Noa, “Nitawaangamiza watu wote, kwa kuwa dunia imejaa ukatili kwa sababu yao. Hakika mimi nitaangamiza watu pamoja na dunia.
And he said God to Noah [the] end of all flesh [is] coming before me for is full the earth violence because of them and here [am] I about to destroy them with the earth.
14 Kwa hiyo jitengenezee safina kubwa kwa mbao za mvinje, tengeneza vyumba ndani yake na uipake lami ndani na nje.
Make for yourself an ark of wood of gopher nests you will make the ark and you will cover it from inside and from outside with pitch.
15 Hivi ndivyo utakavyoitengeneza: Safina iwe na urefu wa dhiraa 300, upana wake dhiraa hamsini na kimo chake dhiraa thelathini.
And this [is] how you will make it [will be] three hundred cubit[s] [the] length of the ark [will be] fifty cubit[s] breadth its and [will be] thirty cubit[s] height its.
16 Itengenezee paa na umalizie safina kwa kuacha nafasi ya dhiraa moja juu. Weka mlango ubavuni mwa safina, na uifanye ya ghorofa ya chini, ya kati na ya juu.
A roof - you will make for the ark and to a cubit you will finish it from to above and [the] entrance of the ark in side its you will put lower [decks] second [decks] and third [decks] you will make it.
17 Nitaleta gharika ya maji juu ya nchi ili kuangamiza uhai wote chini ya mbingu, kila kiumbe chenye pumzi ya uhai ndani yake. Kila kitu juu ya nchi kitaangamia.
And I here I [am] about to bring the flood water on the earth to destroy all flesh which [is] in it [the] breath of life from under the heavens all that [is] on the earth will die.
18 Lakini Mimi nitaweka Agano langu na wewe, nawe utaingia ndani ya Safina, wewe pamoja na mke wako, wanao na wake zao.
And I will establish covenant my with you and you will go into the ark you and sons your and wife your and [the] wives of sons your with you.
19 Utaingiza ndani ya Safina kila aina ya kiumbe hai wawili wawili, wa kiume na wa kike, ili kuwahifadhi hai pamoja na wewe.
And of every living [thing] of all flesh two of everything you will bring into the ark to preserve alive with you male and female they will be.
20 Wawili wa kila aina ya ndege, wa kila aina ya mnyama na wa kila aina ya kitambaacho ardhini watakuja kwako ili wahifadhiwe hai.
Of the bird[s] to kind its and of the animal[s] to kind its from every creeping thing of the ground to kind its two of everything they will come to you to preserve alive.
21 Utachukua kila aina ya chakula kitakacholiwa, na ukiweke akiba kama chakula kwa ajili yako na yao.”
And you take for yourself some of all food which is eaten and you will gather [it] to yourself and it will become for you and for them food.
22 Noa akafanya kila kitu kama vile Mungu alivyomwamuru.
And he did Noah according to all that he commanded him God so he did.