< Mwanzo 6 >

1 Watu walipoanza kuongezeka idadi katika uso wa dunia na watoto wa kike wakazaliwa kwao,
People started to increase in number and spread out across the earth. Daughters were born to them,
2 wana wa Mungu wakawaona kuwa hao binti za wanadamu walikuwa wazuri wa sura, wakaoa yeyote miongoni mwao waliyemchagua.
and the sons of God saw that these women were beautiful, and they took whichever ones they wanted.
3 Ndipo Bwana akasema, “Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye ni wa kufa, siku zake zitakuwa miaka 120.”
Then the Lord said, “My life-giving Spirit will not remain in these people forever, because they are only mortal. The time they have left will be 120 years.”
4 Wanefili walikuwako duniani siku hizo, na baadaye, hao wana wa Mungu walipoingia kwa binti za wanadamu na kuzaa nao. Wanefili walikuwa mashujaa na watu waliojulikana wa zamani hizo.
There were giants on earth in those days, and also later on. They were born after the sons of God slept with the daughters of these people. Their sons became the great warriors and famous men of ancient times.
5 Bwana akaona jinsi uovu wa mwanadamu ulivyokuwa mkubwa duniani, na ya kuwa kila mwelekeo wa mawazo ya moyo wake wakati wote ulikuwa mbaya tu.
The Lord saw how terribly evil people on earth had become—every single thought in their minds was evil all the time!
6 Bwana akasikitika kwamba alimuumba mwanadamu duniani, moyo wa Mungu ukajaa masikitiko.
The Lord was sorry he'd made human beings to live on the earth; it made him very sad to think about it.
7 Kwa hiyo Bwana akasema, “Nitamfutilia mbali mwanadamu niliyemuumba kutoka kwenye uso wa dunia, wanadamu na wanyama, pamoja na viumbe vitambaavyo na ndege wa angani. Kwa maana nasikitika kuwaumba.”
So the Lord said, “I'm going to wipe out these people I created from the earth, and not only them but also the animals, the creatures that run along the ground, and the birds, because I'm sorry I made them.”
8 Lakini Noa akapata kibali machoni pa Bwana.
But the Lord was pleased with Noah.
9 Hivi ndivyo vizazi vya Noa. Noa alikuwa mtu wa haki, na mkamilifu miongoni mwa watu wa wakati wake, tena alitembea na Mungu.
This is the story of Noah and his family. Noah was a man of integrity, living a moral life among the people of his time. He had a close relationship with God.
10 Noa alikuwa na wana watatu: Shemu, Hamu na Yafethi.
Noah had three sons: Shem, Ham, and Japheth.
11 Wakati huu dunia ilikuwa imejaa uharibifu na ukatili machoni pa Mungu.
God saw how corrupt the whole world had become, full of violent and lawless people.
12 Mungu akaona jinsi dunia ilivyoharibika, kwa maana watu wote duniani walikuwa wameharibu njia zao.
God recognized that the corruption in the world was due to everyone on earth living corrupt lives.
13 Kwa hiyo Mungu akamwambia Noa, “Nitawaangamiza watu wote, kwa kuwa dunia imejaa ukatili kwa sababu yao. Hakika mimi nitaangamiza watu pamoja na dunia.
So God told Noah, “I have decided to put an end to all people on earth because they are all violent and lawless. I myself am going to destroy all of them, along with the earth.
14 Kwa hiyo jitengenezee safina kubwa kwa mbao za mvinje, tengeneza vyumba ndani yake na uipake lami ndani na nje.
Build an ark out of cypress wood. Make rooms inside the ark, and coat it with tar, both inside and out.
15 Hivi ndivyo utakavyoitengeneza: Safina iwe na urefu wa dhiraa 300, upana wake dhiraa hamsini na kimo chake dhiraa thelathini.
This is how to build it: the ark is to measure 300 cubits long, 50 cubits wide, and 30 cubits high.
16 Itengenezee paa na umalizie safina kwa kuacha nafasi ya dhiraa moja juu. Weka mlango ubavuni mwa safina, na uifanye ya ghorofa ya chini, ya kati na ya juu.
Make a roof for the ark, leaving a cubit-wide opening between the roof and the top of the sides. Put a door in the side of the ark, and construct three decks inside.
17 Nitaleta gharika ya maji juu ya nchi ili kuangamiza uhai wote chini ya mbingu, kila kiumbe chenye pumzi ya uhai ndani yake. Kila kitu juu ya nchi kitaangamia.
I myself am going to flood the earth with water that will destroy everything that breathes, Every living thing everywhere on earth will die.
18 Lakini Mimi nitaweka Agano langu na wewe, nawe utaingia ndani ya Safina, wewe pamoja na mke wako, wanao na wake zao.
But I will keep my agreement with you. You are to go into the ark, taking with you your wife and your sons and their wives.
19 Utaingiza ndani ya Safina kila aina ya kiumbe hai wawili wawili, wa kiume na wa kike, ili kuwahifadhi hai pamoja na wewe.
Take a pair, male and female, of every kind of animal into the ark and make sure you keep them alive.
20 Wawili wa kila aina ya ndege, wa kila aina ya mnyama na wa kila aina ya kitambaacho ardhini watakuja kwako ili wahifadhiwe hai.
The same applies to every kind of bird, livestock, and the creatures that run along the ground—a pair of every kind will come to you so they can be kept alive.
21 Utachukua kila aina ya chakula kitakacholiwa, na ukiweke akiba kama chakula kwa ajili yako na yao.”
Take all kinds of food with you too. Store it so you and the animals will have enough to eat.”
22 Noa akafanya kila kitu kama vile Mungu alivyomwamuru.
Noah did exactly what God ordered him to do.

< Mwanzo 6 >

The World is Destroyed by Water
The World is Destroyed by Water