< Mwanzo 6 >

1 Watu walipoanza kuongezeka idadi katika uso wa dunia na watoto wa kike wakazaliwa kwao,
Da nu Menneskene begyndte at blive talrige på Jorden og der fødtes dem Døtre,
2 wana wa Mungu wakawaona kuwa hao binti za wanadamu walikuwa wazuri wa sura, wakaoa yeyote miongoni mwao waliyemchagua.
fik Gudssønnerne Øje på Menneskedøtrenes Skønhed, og de tog: så mange af dem, som de lystede, til Hustruer.
3 Ndipo Bwana akasema, “Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye ni wa kufa, siku zake zitakuwa miaka 120.”
Da sagde HERREN: "Min Ånd: skal ikke for evigt blive i Menneskene, eftersom de jo dog er Kød; deres Dage skal være 120 År."
4 Wanefili walikuwako duniani siku hizo, na baadaye, hao wana wa Mungu walipoingia kwa binti za wanadamu na kuzaa nao. Wanefili walikuwa mashujaa na watu waliojulikana wa zamani hizo.
I hine Dage, da Gudssønnerne gik ind til Menneskedøtrene og disse fødte dem Børn men også senere hen i Tiden - levede Kæmperne på Jorden. Det er Heltene, hvis Ry når tilbage til Fortids Dage.
5 Bwana akaona jinsi uovu wa mwanadamu ulivyokuwa mkubwa duniani, na ya kuwa kila mwelekeo wa mawazo ya moyo wake wakati wote ulikuwa mbaya tu.
Men HERREN så, at Menneskenes, Ondskab tog til på Jorden, og at deres Hjerters Higen og Tragten kun var ond Dagen lang.
6 Bwana akasikitika kwamba alimuumba mwanadamu duniani, moyo wa Mungu ukajaa masikitiko.
Da angrede HERREN, at han havde gjort Menneskene på Jorden, og det. skar ham i Hjertet.
7 Kwa hiyo Bwana akasema, “Nitamfutilia mbali mwanadamu niliyemuumba kutoka kwenye uso wa dunia, wanadamu na wanyama, pamoja na viumbe vitambaavyo na ndege wa angani. Kwa maana nasikitika kuwaumba.”
Og HERREN sagde: "Jeg vil udslette Menneskene, som jeg har skabt, af Jordens Flade, både Mennesker, Kvæg, Kryb og Himmelens, Fugle, thi jeg angrer, at jeg gjorde dem!"
8 Lakini Noa akapata kibali machoni pa Bwana.
Men Noa fandt Nåde for HERRENs Øjne
9 Hivi ndivyo vizazi vya Noa. Noa alikuwa mtu wa haki, na mkamilifu miongoni mwa watu wa wakati wake, tena alitembea na Mungu.
Dette er Noas Slægtebog. Noa var en retfærdig, ustraffelig Mand blandt sine samtidige; Noa vandrede med Gud.
10 Noa alikuwa na wana watatu: Shemu, Hamu na Yafethi.
Noa avlede tre Sønner: Sem, Kam og Jafet.
11 Wakati huu dunia ilikuwa imejaa uharibifu na ukatili machoni pa Mungu.
Men Jorden fordærvedes for Guds Øjne, og Jorden blev fuld af Uret;
12 Mungu akaona jinsi dunia ilivyoharibika, kwa maana watu wote duniani walikuwa wameharibu njia zao.
og Gud så til Jorden, og se, den var fordærvet, thi alt Kød havde fordærvet sin Vej på Jorden.
13 Kwa hiyo Mungu akamwambia Noa, “Nitawaangamiza watu wote, kwa kuwa dunia imejaa ukatili kwa sababu yao. Hakika mimi nitaangamiza watu pamoja na dunia.
Da sagde Gud til Noa: "Jeg har besluttet at gøre Ende på alt Kød, fordi Jorden ved deres Skyld et fuld af Uret; derfor vil jeg nu udrydde dem af Jorden.
14 Kwa hiyo jitengenezee safina kubwa kwa mbao za mvinje, tengeneza vyumba ndani yake na uipake lami ndani na nje.
Men du skal gøre dig en Ark af Gofertræ og indrette den med Rum ved Rum og overstryge den med Beg både indvendig og udvendig;
15 Hivi ndivyo utakavyoitengeneza: Safina iwe na urefu wa dhiraa 300, upana wake dhiraa hamsini na kimo chake dhiraa thelathini.
og således skal du bygge Arken: Den skal være 300 Alen lang, 50 Alen bred og 30 Alen høj;
16 Itengenezee paa na umalizie safina kwa kuacha nafasi ya dhiraa moja juu. Weka mlango ubavuni mwa safina, na uifanye ya ghorofa ya chini, ya kati na ya juu.
du skal anbringe Taget på Arken, og det skal ikke rage længer ud end een Alen fra oven; på Arkens Side skal du sætte Døren, og du skal indrette den med et nederste, et mellemste og et øverste Stokværk.
17 Nitaleta gharika ya maji juu ya nchi ili kuangamiza uhai wote chini ya mbingu, kila kiumbe chenye pumzi ya uhai ndani yake. Kila kitu juu ya nchi kitaangamia.
Se, jeg bringer nu Vandfloden over Jorden for at udrydde alt Kød under Himmelen, som har Livsånde; alt, hvad der er på Jorden, skal forgå.
18 Lakini Mimi nitaweka Agano langu na wewe, nawe utaingia ndani ya Safina, wewe pamoja na mke wako, wanao na wake zao.
Men jeg vil oprette min Pagt med dig. Du skal gå ind i Arken med dine Sønner, din Hustru og dine Sønnekoner:
19 Utaingiza ndani ya Safina kila aina ya kiumbe hai wawili wawili, wa kiume na wa kike, ili kuwahifadhi hai pamoja na wewe.
og af alle Dyr, af alt Kød skal du bringe et Par af hver Slags ind i Arken for at holde dem i Live hos dig. Han og Hundyr skal det være,
20 Wawili wa kila aina ya ndege, wa kila aina ya mnyama na wa kila aina ya kitambaacho ardhini watakuja kwako ili wahifadhiwe hai.
af Fuglene efter deres Arter, af Kvæget efter dets Arter og af alt Jordens Kryb efter dets Arter; Par for Par skal de gå ind til dig for at holdes i Live.
21 Utachukua kila aina ya chakula kitakacholiwa, na ukiweke akiba kama chakula kwa ajili yako na yao.”
Og du skal indsamle et Forråd af alle Slags Levnedsmidler, for at det kan tjene dig og dem til Føde."
22 Noa akafanya kila kitu kama vile Mungu alivyomwamuru.
Og Noa gjorde ganske som Gud havde pålagt ham; således gjorde han.

< Mwanzo 6 >

The World is Destroyed by Water
The World is Destroyed by Water