< Mwanzo 50 >

1 Basi Yosefu akamwangukia baba yake, akalilia juu yake na akambusu.
Yusuf kendini babasının üzerine attı, ağlayarak onu öptü.
2 Ndipo Yosefu akawaagiza matabibu waliokuwa wakimhudumia, wamtie baba yake Israeli dawa ili asioze. Hivyo matabibu wakamtia dawa asioze,
Babasının cesedini mumyalamaları için özel hekimlerine buyruk verdi. Hekimler İsrail'i mumyaladılar.
3 wakatumia siku arobaini, kwa maana ndio muda uliotakiwa wa kutia dawa ili asioze. Nao Wamisri wakamwombolezea Yakobo kwa siku sabini.
Bu iş kırk gün sürdü. Mumyalama için bu süre gerekliydi. Mısırlılar İsrail için yetmiş gün yas tuttu.
4 Siku za kumwombolezea zilipokwisha, Yosefu akawaambia washauri wa Farao, “Kama nimepata kibali machoni penu semeni na Farao kwa ajili yangu. Mwambieni,
Yas günleri geçince, Yusuf firavunun ev halkına, “Eğer benden hoşnut kaldınızsa, lütfen firavunla konuşun” dedi,
5 ‘Baba yangu aliniapisha na kuniambia, “Mimi niko karibu kufa; unizike katika kaburi lile nililochimba kwa ajili yangu mwenyewe katika nchi ya Kanaani.” Sasa nakuomba uniruhusu niende kumzika baba yangu, nami nitarudi.’”
“Babam bana ant içirdi: ‘Ölmek üzereyim. Beni Kenan ülkesinde kendim için kazdırdığım mezara gömeceksin’ dedi. Şimdi lütfen firavuna bildirin, izin versin gideyim, babamı gömüp geleyim.”
6 Farao akasema, “Panda, uende kumzika baba yako, kama alivyokuapiza kufanya.”
Firavun, “Git, babanı göm, andını yerine getir” dedi.
7 Hivyo Yosefu akapanda kwenda kumzika baba yake. Maafisa wote wa Farao wakaenda pamoja naye, watu mashuhuri wa baraza lake na watu mashuhuri wote wa Misri.
Böylece Yusuf babasını gömmeye gitti. Firavunun bütün görevlileri, sarayın ve Mısır'ın ileri gelenleri ona eşlik etti.
8 Hawa ni mbali na watu wote wa nyumbani kwa Yosefu, na ndugu zake, na wale wote wa nyumbani mwa baba yake. Ni watoto wao, makundi yao ya kondoo, mbuzi na ngʼombe tu waliobakia katika nchi ya Gosheni.
Yusuf'un bütün ailesi, kardeşleri, babasının ev halkı da onunla birlikteydi. Yalnız çocukları, davarlarla sığırları Goşen'de bıraktılar.
9 Magari makubwa na wapanda farasi pia walipanda pamoja naye. Likawa kundi kubwa sana.
Arabalarla atlılar da onları izledi. Büyük bir alay oluşturdular.
10 Walipofika kwenye sakafu ya kupuria nafaka ya Atadi, karibu na Yordani, wakalia kwa sauti na kwa uchungu; Yosefu akapumzika huko kwa siku saba kumwombolezea baba yake.
Şeria Irmağı'nın doğusunda Atat Harmanı'na varınca, yüksek sesle, acı acı ağıt yaktılar. Yusuf babası için yedi gün yas tuttu.
11 Wakanaani walioishi huko walipoona maombolezo yaliyofanyika katika sakafu ile ya kupuria ya Atadi, wakasema, “Wamisri wanafanya maombolezo makubwa.” Kwa hiyo mahali pale karibu na Yordani pakaitwa Abel-Mizraimu.
O bölgede yaşayan Kenanlılar, Atat Harmanı'ndaki yası görünce, “Mısırlılar ne kadar hüzünlü yas tutuyor!” dediler. Bu yüzden, Şeria Irmağı'nın doğusundaki bu yere Avel-Misrayim adı verildi.
12 Hivyo wana wa Yakobo wakafanya kama baba yao alivyowaagiza:
Yakup'un oğulları, babalarının vermiş olduğu buyruğu tam tamına yerine getirdiler.
13 Wakamchukua mpaka nchi ya Kanaani, wakamzika kwenye pango katika shamba la Makpela, karibu na Mamre, ambalo Abrahamu alilinunua kutoka kwa Efroni, Mhiti, pamoja na shamba liwe mahali pa kuzikia.
Onu Kenan ülkesine götürüp Mamre yakınlarında Makpela Tarlası'ndaki mağaraya gömdüler. O mağarayı mezar yapmak üzere tarlayla birlikte Hititli Efron'dan İbrahim satın almıştı.
14 Baada ya Yosefu kumzika baba yake, akarudi Misri pamoja na ndugu zake na wale wote waliokuwa wamekwenda naye kumzika baba yake.
Yusuf babasını gömdükten sonra, kendisi, kardeşleri ve onunla birlikte babasını gömmeye gelenlerin hepsi Mısır'a döndüler.
15 Ndugu zake Yosefu walipoona kwamba baba yao amekufa, wakasema, “Itakuwaje kama Yosefu ataweka kinyongo dhidi yetu na kutulipa mabaya yote tuliyomtendea?”
Babalarının ölümünden sonra Yusuf'un kardeşleri, “Belki Yusuf bize kin besliyordur” dediler, “Ya ona yaptığımız kötülüğe karşılık bizden öç almaya kalkarsa?”
16 Kwa hiyo wakampelekea Yosefu ujumbe, wakasema, “Kabla baba yako hajafa aliacha maagizo haya:
Böylece Yusuf'a haber gönderdiler: “Babamız ölmeden önce Yusuf'a şöyle deyin diye buyurmuştu: ‘Kardeşlerin sana kötülük yaptılar, lütfen onların suçunu, günahını bağışla.’ Ne olur şimdi günahımızı bağışla. Biz babanın Tanrısı'nın kullarıyız.” Yusuf bu haberi alınca ağladı.
17 ‘Hili ndilo mtakalomwambia Yosefu: Ninakuomba uwasamehe ndugu zako dhambi na mabaya kwa vile walivyokutenda vibaya.’ Sasa tafadhali samehe dhambi za watumishi wa Mungu wa baba yako.” Ujumbe huu ulipomfikia, Yosefu akalia.
18 Ndipo ndugu zake wakaja na kujitupa chini mbele yake. Wakasema, “Sisi ni watumwa wako.”
Bunun üzerine kardeşleri gidip onun önünde yere kapanarak, “Senin köleniz” dediler.
19 Lakini Yosefu akawaambia, “Msiogope. Je, mimi ni badala ya Mungu?
Yusuf, “Korkmayın” dedi, “Ben Tanrı mıyım?
20 Mlikusudia kunidhuru, lakini Mungu alikusudia mema, ili litimie hili linalofanyika sasa, kuokoa maisha ya watu wengi.
Siz bana kötülük düşündünüz, ama Tanrı bugün olduğu gibi birçok halkın yaşamını korumak için o kötülüğü iyiliğe çevirdi.
21 Hivyo basi, msiogope. Mimi nitawatunza ninyi nyote pamoja na watoto wenu.” Akawahakikishia na kusema nao kwa wema.
Korkmanıza gerek yok, size de çocuklarınıza da bakacağım.” Yüreklerine dokunacak güzel sözlerle onlara güven verdi.
22 Yosefu akakaa katika nchi ya Misri, yeye pamoja na jamaa yote ya baba yake. Akaishi miaka 110,
Yusuf'la babasının ev halkı Mısır'a yerleştiler. Yusuf yüz on yıl yaşadı.
23 naye akaona kizazi cha tatu cha watoto wa Efraimu. Pia akaona watoto wa Makiri mwana wa Manase, wakawekwa magotini mwa Yosefu walipozaliwa.
Efrayim'in üç göbek çocuklarını gördü. Manaşşe'nin oğlu Makir'in çocukları onun elinde doğdu.
24 Ndipo Yosefu akawaambia ndugu zake, “Mimi ninakaribia kufa. Lakini kwa hakika Mungu atawasaidia na kuwachukueni kutoka nchi hii na kuwapeleka katika nchi aliyomwahidi kwa kiapo Abrahamu, Isaki na Yakobo.”
Yusuf yakınlarına, “Ben ölmek üzereyim” dedi, “Ama Tanrı kesinlikle size yardım edecek; sizi İbrahim'e, İshak'a, Yakup'a ant içerek söz verdiği topraklara götürecek.”
25 Naye Yosefu akawaapisha wana wa Israeli na kuwaambia, “Hakika Mungu atawasaidia, nanyi ni lazima mhakikishe mmepandisha mifupa yangu kutoka mahali hapa.”
Sonra onlara ant içirerek, “Tanrı kesinlikle size yardım edecek” dedi, “O zaman kemiklerimi buradan götürürsünüz.”
26 Kwa hiyo Yosefu akafa akiwa na umri wa miaka 110. Baada ya kumtia dawa ili asioze, akawekwa kwenye jeneza huko Misri.
Yusuf yüz on yaşında öldü. Onu mumyalayıp Mısır'da bir tabuta koydular.

< Mwanzo 50 >