< Mwanzo 5 >

1 Hii ni orodha iliyoandikwa ya vizazi vya Adamu. Wakati Mungu alipomuumba Adamu, alimfanya kwa sura ya Mungu.
این است شرح پیدایش آدم و نسل او. هنگامی که خدا خواست انسان را بیافریند، او را شبیه خود آفرید.
2 Aliwaumba mwanaume na mwanamke, akawabariki. Walipokwisha kuumbwa, akawaita “mwanadamu.”
او آنها را مرد و زن خلق فرموده، برکت داد و از همان آغاز خلقت، ایشان را انسان نامید.
3 Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, alikuwa na mwana aliyekuwa na sura yake, mwenye kufanana naye. Akamwita Sethi.
آدم: وقتی آدم ۱۳۰ ساله بود، پسرش شیث به دنیا آمد. او شبیه پدرش آدم بود. بعد از تولد شیث، آدم ۸۰۰ سال دیگر عمر کرد و صاحب پسران و دختران شد. آدم در سن ۹۳۰ سالگی مرد.
4 Baada ya Sethi kuzaliwa, Adamu aliishi miaka 800, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
5 Adamu aliishi jumla ya miaka 930, ndipo akafa.
6 Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
شیث: وقتی شیث ۱۰۵ ساله بود، پسرش انوش به دنیا آمد. بعد از تولد انوش، شیث ۸۰۷ سال دیگر عمر کرد و صاحب پسران و دختران شد. شیث در سن ۹۱۲ سالگی مرد.
7 Baada ya kumzaa Enoshi, Sethi aliishi miaka 807, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
8 Sethi aliishi jumla ya miaka 912, ndipo akafa.
9 Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
انوش: وقتی انوش نود ساله بود، پسرش قینان به دنیا آمد. بعد از تولد قینان، انوش ۸۱۵ سال دیگر عمر کرد و صاحب پسران و دختران شد. انوش در سن ۹۰۵ سالگی مرد.
10 Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815, naye alikuwa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
11 Enoshi aliishi jumla ya miaka 905, ndipo akafa.
12 Kenani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
قینان: وقتی قینان هفتاد ساله بود، پسرش مهلل‌ئیل به دنیا آمد. بعد از تولد مهلل‌ئیل، قینان ۸۴۰ سال دیگر عمر کرد و صاحب پسران و دختران شد. او در سن ۹۱۰ سالگی مرد.
13 Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
14 Kenani aliishi jumla ya miaka 910, ndipo akafa.
15 Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Yaredi.
مهلل‌ئیل: وقتی مهلل‌ئیل شصت و پنج ساله بود، پسرش یارد به دنیا آمد. پس از تولد یارد، مهلل‌ئیل ۸۳۰ سال دیگر عمر کرد و صاحب پسران و دختران شد. او در سن ۸۹۵ سالگی مرد.
16 Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
17 Mahalaleli aliishi jumla ya miaka 895, ndipo akafa.
18 Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, akamzaa Enoki.
یارد: وقتی یارد ۱۶۲ ساله بود، پسرش خنوخ به دنیا آمد. بعد از تولد خنوخ، یارد ۸۰۰ سال دیگر عمر کرد و صاحب پسران و دختران شد. یارد در سن ۹۶۲ سالگی مرد.
19 Baada ya kumzaa Enoki, Yaredi aliishi miaka 800, naye akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
20 Yaredi aliishi jumla ya miaka 962, ndipo akafa.
21 Enoki alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela.
خنوخ: وقتی خنوخ شصت و پنج ساله بود، پسرش متوشالح به دنیا آمد. بعد از تولد متوشالح، خنوخ ۳۰۰ سال دیگر با خدا زیست. او صاحب پسران و دخترانی شد و ۳۶۵ سال زندگی کرد. خنوخ با خدا می‌زیست و خدا او را به حضور خود به بالا برد و دیگر کسی او را ندید.
22 Baada ya kumzaa Methusela, Enoki alitembea na Mungu miaka 300, na akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
23 Enoki aliishi jumla ya miaka 365.
24 Enoki akatembea na Mungu, kisha akatoweka, kwa sababu Mungu alimchukua.
25 Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, akamzaa Lameki.
متوشالح: وقتی متوشالح ۱۸۷ ساله بود، پسرش لمک به دنیا آمد. بعد از تولد لمک، متوشالح ۷۸۲ سال دیگر زندگی کرد و صاحب پسران و دختران شد. متوشالح در سن ۹۶۹ سالگی مرد.
26 Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
27 Methusela aliishi jumla ya miaka 969, ndipo akafa.
28 Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.
لمک: وقتی لمک ۱۸۲ ساله بود، پسرش نوح به دنیا آمد. لمک گفت: «این پسر، ما را از کار سختِ زراعت که در اثر لعنت خداوند بر زمین، دامنگیر ما شده، آسوده خواهد کرد.» پس لمک اسم او را نوح (یعنی «آسودگی») گذاشت. بعد از تولد نوح، لمک ۵۹۵ سال دیگر عمر کرد و صاحب پسران و دختران شد. او در سن ۷۷۷ سالگی مرد.
29 Akamwita jina lake Noa, akasema, “Yeye ndiye atakayetufariji katika kazi na maumivu makali ya mikono yetu yaliyosababishwa na ardhi iliyolaaniwa na Bwana.”
30 Baada ya Noa kuzaliwa, Lameki aliishi miaka 595, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
31 Lameki aliishi jumla ya miaka 777, ndipo akafa.
32 Baada ya Noa kuishi miaka 500, aliwazaa Shemu, Hamu na Yafethi.
نوح: نوح در سن ۵۰۰ سالگی صاحب سه پسر به نامهای سام، حام و یافث بود.

< Mwanzo 5 >