< Mwanzo 5 >

1 Hii ni orodha iliyoandikwa ya vizazi vya Adamu. Wakati Mungu alipomuumba Adamu, alimfanya kwa sura ya Mungu.
Hic est liber generationis Adam. In die, qua creavit Deus hominem, ad similitudinem Dei fecit illum.
2 Aliwaumba mwanaume na mwanamke, akawabariki. Walipokwisha kuumbwa, akawaita “mwanadamu.”
Masculum et feminam creavit eos, et benedixit illis: et vocavit nomen eorum Adam, in die quo creati sunt.
3 Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, alikuwa na mwana aliyekuwa na sura yake, mwenye kufanana naye. Akamwita Sethi.
Vixit autem Adam centum triginta annis: et genuit ad imaginem et similitudinem suam, vocavitque nomen eius Seth.
4 Baada ya Sethi kuzaliwa, Adamu aliishi miaka 800, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Et facti sunt dies Adam, postquam genuit Seth, octingenti anni: genuitque filios et filias.
5 Adamu aliishi jumla ya miaka 930, ndipo akafa.
Et factum est omne tempus quod vixit Adam, anni nongenti triginta, et mortuus est.
6 Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
Vixit quoque Seth centum quinque annis, et genuit Enos.
7 Baada ya kumzaa Enoshi, Sethi aliishi miaka 807, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Vixitque Seth postquam genuit Enos, octingentis septem annis, genuitque filios et filias.
8 Sethi aliishi jumla ya miaka 912, ndipo akafa.
Et facti sunt omnes dies Seth nongentorum duodecim annorum, et mortuus est.
9 Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
Vixit vero Enos nonaginta annis, et genuit Cainan.
10 Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815, naye alikuwa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Post cuius ortum vixit octingentis quindecim annis, et genuit filios, et filias.
11 Enoshi aliishi jumla ya miaka 905, ndipo akafa.
Factique sunt omnes dies Enos nongenti quinque anni, et mortuus est.
12 Kenani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
Vixit quoque Cainan septuaginta annis, et genuit Malaleel.
13 Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Et vixit Cainan, postquam genuit Malaleel, octingentis quadraginta annis, genuitque filios et filias.
14 Kenani aliishi jumla ya miaka 910, ndipo akafa.
Et facti sunt omnes dies Cainan nongenti decem anni, et mortuus est.
15 Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Yaredi.
Vixit autem Malaleel sexaginta quinque annis, et genuit Iared.
16 Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Et vixit Malaleel postquam genuit Iared, octingentis triginta annis: et genuit filios et filias.
17 Mahalaleli aliishi jumla ya miaka 895, ndipo akafa.
Et facti sunt omnes dies Malaleel octingenti nonaginta quinque anni, et mortuus est.
18 Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, akamzaa Enoki.
Vixitque Iared centum sexaginta duobus annis, et genuit Henoch.
19 Baada ya kumzaa Enoki, Yaredi aliishi miaka 800, naye akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Et vixit Iared, postquam genuit Henoch, octingentis annis, et genuit filios et filias.
20 Yaredi aliishi jumla ya miaka 962, ndipo akafa.
Et facti sunt omnes dies Iared nongenti sexaginta duo anni, et mortuus est.
21 Enoki alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela.
Porro Henoch vixit sexaginta quinque annis, et genuit Mathusalam.
22 Baada ya kumzaa Methusela, Enoki alitembea na Mungu miaka 300, na akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Et ambulavit Henoch cum Deo: et vixit, postquam genuit Mathusalam, trecentis annis, et genuit filios et filias.
23 Enoki aliishi jumla ya miaka 365.
Et facti sunt omnes dies Henoch trecenti sexaginta quinque anni.
24 Enoki akatembea na Mungu, kisha akatoweka, kwa sababu Mungu alimchukua.
Ambulavitque cum Deo, et non apparuit: quia tulit eum Deus.
25 Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, akamzaa Lameki.
Vixit quoque Mathusala centum octoginta septem annis, et genuit Lamech.
26 Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Et vixit Mathusala, postquam genuit Lamech, septingentis octoginta duobus annis, et genuit filios et filias.
27 Methusela aliishi jumla ya miaka 969, ndipo akafa.
Et facti sunt omnes dies Mathusala nongenti sexaginta novem anni, et mortuus est.
28 Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.
Vixit autem Lamech centum octoginta duobus annis, et genuit filium:
29 Akamwita jina lake Noa, akasema, “Yeye ndiye atakayetufariji katika kazi na maumivu makali ya mikono yetu yaliyosababishwa na ardhi iliyolaaniwa na Bwana.”
vocavitque nomen eius Noe, dicens: Iste consolabitur nos ab operibus et laboribus manuum nostrarum in terra, cui maledixit Dominus.
30 Baada ya Noa kuzaliwa, Lameki aliishi miaka 595, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Vixitque Lamech, postquam genuit Noe, quingentis nonaginta quinque annis, et genuit filios et filias.
31 Lameki aliishi jumla ya miaka 777, ndipo akafa.
Et facti sunt omnes dies Lamech, septingenti septuaginta septem anni, et mortuus est.
32 Baada ya Noa kuishi miaka 500, aliwazaa Shemu, Hamu na Yafethi.
Noe vero cum quingentorum esset annorum, genuit Sem, Cham, et Iapheth.

< Mwanzo 5 >