< Mwanzo 5 >
1 Hii ni orodha iliyoandikwa ya vizazi vya Adamu. Wakati Mungu alipomuumba Adamu, alimfanya kwa sura ya Mungu.
यह आदम के वंशजों का प्रलेख है: जब परमेश्वर ने मनुष्य की सृष्टि की, तो उन्होंने मनुष्य को अपने ही रूप में बनाया.
2 Aliwaumba mwanaume na mwanamke, akawabariki. Walipokwisha kuumbwa, akawaita “mwanadamu.”
परमेश्वर ने मनुष्य को नर तथा नारी कहकर उन्हें आशीष दी और परमेश्वर ने उनका नाम आदम रखा.
3 Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, alikuwa na mwana aliyekuwa na sura yake, mwenye kufanana naye. Akamwita Sethi.
जब आदम 130 वर्ष के हुए, तब एक पुत्र पैदा हुआ, जिनका रूप स्वयं उन्हीं के समान था; उनका शेत नाम रखा गया.
4 Baada ya Sethi kuzaliwa, Adamu aliishi miaka 800, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
शेत के जन्म के बाद आदम 800 वर्ष के हुए, उनके और पुत्र-पुत्रियां भी पैदा हुए.
5 Adamu aliishi jumla ya miaka 930, ndipo akafa.
इस प्रकार आदम कुल 930 साल जीवित रहे, फिर उनकी मृत्यु हो गई.
6 Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
जब शेत 105 वर्ष के थे, तब एनोश का जन्म हुआ.
7 Baada ya kumzaa Enoshi, Sethi aliishi miaka 807, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
एनोश के बाद उनके और पुत्र-पुत्रियां भी पैदा हुए तथा शेत 807 वर्ष और जीवित रहे.
8 Sethi aliishi jumla ya miaka 912, ndipo akafa.
जब शेत कुल 912 साल जीवित रहे, तब उनकी मृत्यु हो गई.
9 Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
जब एनोश 90 वर्ष के हुए, तब केनान का जन्म हुआ.
10 Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815, naye alikuwa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
केनान के जन्म के बाद एनोश 815 वर्ष और जीवित रहे तथा उनके और पुत्र-पुत्रियां भी पैदा हुए.
11 Enoshi aliishi jumla ya miaka 905, ndipo akafa.
जब एनोश कुल 905 साल जीवित रहे, तब उनकी मृत्यु हो गई.
12 Kenani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
जब केनान 70 वर्ष के हुए, तब माहालालेल का जन्म हुआ.
13 Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
माहालालेल के जन्म के बाद, केनान 840 वर्ष और जीवित रहे तथा उनके और पुत्र-पुत्रियां भी पैदा हुए.
14 Kenani aliishi jumla ya miaka 910, ndipo akafa.
इस प्रकार केनान कुल 910 वर्ष के हुए, और उनकी मृत्यु हो गई.
15 Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Yaredi.
जब माहालालेल 65 वर्ष के हुए, तब यारेद का जन्म हुआ.
16 Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
यारेद के जन्म के बाद, माहालालेल 830 वर्ष और जीवित रहे तथा उनके और पुत्र-पुत्रियां भी पैदा हुए.
17 Mahalaleli aliishi jumla ya miaka 895, ndipo akafa.
जब माहालालेल 895 वर्ष के थे, तब उनकी मृत्यु हो गई.
18 Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, akamzaa Enoki.
जब यारेद 162 वर्ष के हुए, तब हनोख का जन्म हुआ.
19 Baada ya kumzaa Enoki, Yaredi aliishi miaka 800, naye akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
हनोख के जन्म के बाद, यारेद 800 वर्ष और जीवित रहे तथा उनके और पुत्र-पुत्रियां भी पैदा हुईं.
20 Yaredi aliishi jumla ya miaka 962, ndipo akafa.
जब यारेद कुल 962 साल जीवित रहे, तब उनकी मृत्यु हो गई.
21 Enoki alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela.
जब हनोख 65 वर्ष के हुए, तब मेथुसेलाह का जन्म हुआ.
22 Baada ya kumzaa Methusela, Enoki alitembea na Mungu miaka 300, na akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
मेथुसेलाह के जन्म के बाद हनोख 300 वर्ष तक परमेश्वर के साथ साथ चलते रहे. उसके अन्य पुत्र-पुत्रियां भी पैदा हुए.
23 Enoki aliishi jumla ya miaka 365.
हनोख कुल 265 साल जीवित रहे.
24 Enoki akatembea na Mungu, kisha akatoweka, kwa sababu Mungu alimchukua.
हनोख परमेश्वर के साथ साथ चलते रहे. और वे नहीं रहे, क्योंकि परमेश्वर ने उन्हें अपने पास उठा लिया.
25 Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, akamzaa Lameki.
जब मेथुसेलाह 187 वर्ष के हुए, तब लामेख का जन्म हुआ.
26 Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
लामेख के जन्म के बाद, मेथुसेलाह 782 वर्ष और जीवित रहे तथा उनके और पुत्र-पुत्रियां भी पैदा हुए.
27 Methusela aliishi jumla ya miaka 969, ndipo akafa.
जब मेथुसेलाह कुल 969 साल जीवित रहे, तब उनकी मृत्यु हो गई.
28 Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.
जब लामेख 182 वर्ष के हुए, तब एक पुत्र का जन्म हुआ,
29 Akamwita jina lake Noa, akasema, “Yeye ndiye atakayetufariji katika kazi na maumivu makali ya mikono yetu yaliyosababishwa na ardhi iliyolaaniwa na Bwana.”
जिनका नाम उन्होंने नोहा यह कहकर रखा, “यह बालक हमें हमारे कामों से तथा मेहनत से, और इस शापित भूमि से शांति देगा.”
30 Baada ya Noa kuzaliwa, Lameki aliishi miaka 595, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
नोहा के जन्म के बाद लामेख 595 वर्ष और जीवित रहे, तथा उनके और पुत्र-पुत्रियां पैदा हुए.
31 Lameki aliishi jumla ya miaka 777, ndipo akafa.
जब लामेख कुल 777 साल जीवित रहे, तब उनकी मृत्यु हुई.
32 Baada ya Noa kuishi miaka 500, aliwazaa Shemu, Hamu na Yafethi.
नोहा के 500 वर्ष की आयु में शेम, हाम तथा याफेत का जन्म हुआ.