< Mwanzo 5 >

1 Hii ni orodha iliyoandikwa ya vizazi vya Adamu. Wakati Mungu alipomuumba Adamu, alimfanya kwa sura ya Mungu.
C’est ici le livre des générations d’Adam. Au jour où Dieu créa Adam, il le fit à la ressemblance de Dieu.
2 Aliwaumba mwanaume na mwanamke, akawabariki. Walipokwisha kuumbwa, akawaita “mwanadamu.”
Il les créa mâle et femelle, et les bénit; et il appela leur nom Adam, au jour où ils furent créés.
3 Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, alikuwa na mwana aliyekuwa na sura yake, mwenye kufanana naye. Akamwita Sethi.
Et Adam vécut 130 ans, et engendra [un fils] à sa ressemblance, selon son image, et appela son nom Seth.
4 Baada ya Sethi kuzaliwa, Adamu aliishi miaka 800, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Et les jours d’Adam, après qu’il eut engendré Seth, furent 800 ans; et il engendra des fils et des filles.
5 Adamu aliishi jumla ya miaka 930, ndipo akafa.
Et tous les jours qu’Adam vécut furent 930 ans; et il mourut.
6 Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
Et Seth vécut 105 ans, et engendra Énosh.
7 Baada ya kumzaa Enoshi, Sethi aliishi miaka 807, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Et Seth, après qu’il eut engendré Énosh, vécut 807 ans; et il engendra des fils et des filles.
8 Sethi aliishi jumla ya miaka 912, ndipo akafa.
Et tous les jours de Seth furent 912 ans; et il mourut.
9 Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
Et Énosh vécut 90 ans, et engendra Kénan.
10 Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815, naye alikuwa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Et Énosh, après qu’il eut engendré Kénan, vécut 815 ans; et il engendra des fils et des filles.
11 Enoshi aliishi jumla ya miaka 905, ndipo akafa.
Et tous les jours d’Énosh furent 905 ans; et il mourut.
12 Kenani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
Et Kénan vécut 70 ans, et engendra Mahalaleël.
13 Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Et Kénan, après qu’il eut engendré Mahalaleël, vécut 840 ans; et il engendra des fils et des filles.
14 Kenani aliishi jumla ya miaka 910, ndipo akafa.
Et tous les jours de Kénan furent 910 ans; et il mourut.
15 Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Yaredi.
Et Mahalaleël vécut 65 ans, et engendra Jéred.
16 Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Et Mahalaleël, après qu’il eut engendré Jéred, vécut 830 ans; et il engendra des fils et des filles.
17 Mahalaleli aliishi jumla ya miaka 895, ndipo akafa.
Et tous les jours de Mahalaleël furent 895 ans; et il mourut.
18 Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, akamzaa Enoki.
Et Jéred vécut 162 ans, et engendra Hénoc.
19 Baada ya kumzaa Enoki, Yaredi aliishi miaka 800, naye akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Et Jéred, après qu’il eut engendré Hénoc, vécut 800 ans; et il engendra des fils et des filles.
20 Yaredi aliishi jumla ya miaka 962, ndipo akafa.
Et tous les jours de Jéred furent 962 ans; et il mourut.
21 Enoki alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela.
Et Hénoc vécut 65 ans, et engendra Methushélah.
22 Baada ya kumzaa Methusela, Enoki alitembea na Mungu miaka 300, na akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Et Hénoc, après qu’il eut engendré Methushélah, marcha avec Dieu 300 ans; et il engendra des fils et des filles.
23 Enoki aliishi jumla ya miaka 365.
Et tous les jours de Hénoc furent 365 ans.
24 Enoki akatembea na Mungu, kisha akatoweka, kwa sababu Mungu alimchukua.
Et Hénoc marcha avec Dieu; et il ne fut plus, car Dieu le prit.
25 Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, akamzaa Lameki.
Et Methushélah vécut 187 ans, et engendra Lémec.
26 Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Et Methushélah, après qu’il eut engendré Lémec, vécut 782 ans; et il engendra des fils et des filles.
27 Methusela aliishi jumla ya miaka 969, ndipo akafa.
Et tous les jours de Methushélah furent 969 ans; et il mourut.
28 Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.
Et Lémec vécut 182 ans, et engendra un fils;
29 Akamwita jina lake Noa, akasema, “Yeye ndiye atakayetufariji katika kazi na maumivu makali ya mikono yetu yaliyosababishwa na ardhi iliyolaaniwa na Bwana.”
et il appela son nom Noé, disant: Celui-ci nous consolera à l’égard de notre ouvrage et du travail de nos mains, à cause du sol que l’Éternel a maudit.
30 Baada ya Noa kuzaliwa, Lameki aliishi miaka 595, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Et Lémec, après qu’il eut engendré Noé, vécut 595 ans; et il engendra des fils et des filles.
31 Lameki aliishi jumla ya miaka 777, ndipo akafa.
Et tous les jours de Lémec furent 777 ans; et il mourut.
32 Baada ya Noa kuishi miaka 500, aliwazaa Shemu, Hamu na Yafethi.
Et Noé était âgé de 500 ans, et Noé engendra Sem, Cham, et Japheth.

< Mwanzo 5 >