< Mwanzo 5 >

1 Hii ni orodha iliyoandikwa ya vizazi vya Adamu. Wakati Mungu alipomuumba Adamu, alimfanya kwa sura ya Mungu.
This is the book of the generations of Adam. In the day that God created man, he made him in God’s likeness.
2 Aliwaumba mwanaume na mwanamke, akawabariki. Walipokwisha kuumbwa, akawaita “mwanadamu.”
He created them male and female, and blessed them. On the day they were created, he named them Adam.
3 Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, alikuwa na mwana aliyekuwa na sura yake, mwenye kufanana naye. Akamwita Sethi.
Adam lived one hundred thirty years, and became the father of a son in his own likeness, after his image, and named him Seth.
4 Baada ya Sethi kuzaliwa, Adamu aliishi miaka 800, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
The days of Adam after he became the father of Seth were eight hundred years, and he became the father of other sons and daughters.
5 Adamu aliishi jumla ya miaka 930, ndipo akafa.
All the days that Adam lived were nine hundred thirty years, then he died.
6 Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
Seth lived one hundred five years, then became the father of Enosh.
7 Baada ya kumzaa Enoshi, Sethi aliishi miaka 807, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Seth lived after he became the father of Enosh eight hundred seven years, and became the father of other sons and daughters.
8 Sethi aliishi jumla ya miaka 912, ndipo akafa.
All of the days of Seth were nine hundred twelve years, then he died.
9 Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
Enosh lived ninety years, and became the father of Kenan.
10 Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815, naye alikuwa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Enosh lived after he became the father of Kenan eight hundred fifteen years, and became the father of other sons and daughters.
11 Enoshi aliishi jumla ya miaka 905, ndipo akafa.
All of the days of Enosh were nine hundred five years, then he died.
12 Kenani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
Kenan lived seventy years, then became the father of Mahalalel.
13 Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Kenan lived after he became the father of Mahalalel eight hundred forty years, and became the father of other sons and daughters
14 Kenani aliishi jumla ya miaka 910, ndipo akafa.
and all of the days of Kenan were nine hundred ten years, then he died.
15 Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Yaredi.
Mahalalel lived sixty-five years, then became the father of Jared.
16 Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Mahalalel lived after he became the father of Jared eight hundred thirty years, and became the father of other sons and daughters.
17 Mahalaleli aliishi jumla ya miaka 895, ndipo akafa.
All of the days of Mahalalel were eight hundred ninety-five years, then he died.
18 Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, akamzaa Enoki.
Jared lived one hundred sixty-two years, then became the father of Enoch.
19 Baada ya kumzaa Enoki, Yaredi aliishi miaka 800, naye akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Jared lived after he became the father of Enoch eight hundred years, and became the father of other sons and daughters.
20 Yaredi aliishi jumla ya miaka 962, ndipo akafa.
All of the days of Jared were nine hundred sixty-two years, then he died.
21 Enoki alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela.
Enoch lived sixty-five years, then became the father of Methuselah.
22 Baada ya kumzaa Methusela, Enoki alitembea na Mungu miaka 300, na akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
After Methuselah’s birth, Enoch walked with God for three hundred years, and became the father of more sons and daughters.
23 Enoki aliishi jumla ya miaka 365.
All the days of Enoch were three hundred sixty-five years.
24 Enoki akatembea na Mungu, kisha akatoweka, kwa sababu Mungu alimchukua.
Enoch walked with God, and he was not found, for God took him.
25 Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, akamzaa Lameki.
Methuselah lived one hundred eighty-seven years, then became the father of Lamech.
26 Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Methuselah lived after he became the father of Lamech seven hundred eighty-two years, and became the father of other sons and daughters.
27 Methusela aliishi jumla ya miaka 969, ndipo akafa.
All the days of Methuselah were nine hundred sixty-nine years, then he died.
28 Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.
Lamech lived one hundred eighty-two years, then became the father of a son.
29 Akamwita jina lake Noa, akasema, “Yeye ndiye atakayetufariji katika kazi na maumivu makali ya mikono yetu yaliyosababishwa na ardhi iliyolaaniwa na Bwana.”
He named him Noah, saying, “This one will comfort us in our work and in the toil of our hands, caused by the ground which Yahweh has cursed.”
30 Baada ya Noa kuzaliwa, Lameki aliishi miaka 595, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
Lamech lived after he became the father of Noah five hundred ninety-five years, and became the father of other sons and daughters.
31 Lameki aliishi jumla ya miaka 777, ndipo akafa.
All the days of Lamech were seven hundred seventy-seven years, then he died.
32 Baada ya Noa kuishi miaka 500, aliwazaa Shemu, Hamu na Yafethi.
Noah was five hundred years old, then Noah became the father of Shem, Ham, and Japheth.

< Mwanzo 5 >