< Mwanzo 5 >
1 Hii ni orodha iliyoandikwa ya vizazi vya Adamu. Wakati Mungu alipomuumba Adamu, alimfanya kwa sura ya Mungu.
this scroll: book generation Adam in/on/with day to create God man in/on/with likeness God to make [obj] him
2 Aliwaumba mwanaume na mwanamke, akawabariki. Walipokwisha kuumbwa, akawaita “mwanadamu.”
male and female to create them and to bless [obj] them and to call: call by [obj] name their man in/on/with day to create they
3 Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, alikuwa na mwana aliyekuwa na sura yake, mwenye kufanana naye. Akamwita Sethi.
and to live Adam thirty and hundred year and to beget in/on/with likeness his like/as image his and to call: call by [obj] name his Seth
4 Baada ya Sethi kuzaliwa, Adamu aliishi miaka 800, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
and to be day Adam after to beget he [obj] Seth eight hundred year and to beget son: child and daughter
5 Adamu aliishi jumla ya miaka 930, ndipo akafa.
and to be all day Adam which to live nine hundred year and thirty year and to die
6 Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
and to live Seth five year and hundred year and to beget [obj] Enosh
7 Baada ya kumzaa Enoshi, Sethi aliishi miaka 807, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
and to live Seth after to beget he [obj] Enosh seven year and eight hundred year and to beget son: child and daughter
8 Sethi aliishi jumla ya miaka 912, ndipo akafa.
and to be all day Seth two ten year and nine hundred year and to die
9 Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
and to live Enosh ninety year and to beget [obj] Kenan
10 Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815, naye alikuwa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
and to live Enosh after to beget he [obj] Kenan five ten year and eight hundred year and to beget son: child and daughter
11 Enoshi aliishi jumla ya miaka 905, ndipo akafa.
and to be all day Enosh five year and nine hundred year and to die
12 Kenani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
and to live Kenan seventy year and to beget [obj] Mahalalel
13 Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
and to live Kenan after to beget he [obj] Mahalalel forty year and eight hundred year and to beget son: child and daughter
14 Kenani aliishi jumla ya miaka 910, ndipo akafa.
and to be all day Kenan ten year and nine hundred year and to die
15 Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Yaredi.
and to live Mahalalel five year and sixty year and to beget [obj] Jared
16 Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
and to live Mahalalel after to beget he [obj] Jared thirty year and eight hundred year and to beget son: child and daughter
17 Mahalaleli aliishi jumla ya miaka 895, ndipo akafa.
and to be all day Mahalalel five and ninety year and eight hundred year and to die
18 Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, akamzaa Enoki.
and to live Jared two and sixty year and hundred year and to beget [obj] Enoch
19 Baada ya kumzaa Enoki, Yaredi aliishi miaka 800, naye akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
and to live Jared after to beget he [obj] Enoch eight hundred year and to beget son: child and daughter
20 Yaredi aliishi jumla ya miaka 962, ndipo akafa.
and to be all day Jared two and sixty year and nine hundred year and to die
21 Enoki alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela.
and to live Enoch five and sixty year and to beget [obj] Methuselah
22 Baada ya kumzaa Methusela, Enoki alitembea na Mungu miaka 300, na akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
and to go: walk Enoch with [the] God after to beget he [obj] Methuselah three hundred year and to beget son: child and daughter
23 Enoki aliishi jumla ya miaka 365.
and to be all day Enoch five and sixty year and three hundred year
24 Enoki akatembea na Mungu, kisha akatoweka, kwa sababu Mungu alimchukua.
and to go: walk Enoch with [the] God and nothing he for to take: take [obj] him God
25 Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, akamzaa Lameki.
and to live Methuselah seven and eighty year and hundred year and to beget [obj] Lamech
26 Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
and to live Methuselah after to beget he [obj] Lamech two and eighty year and seven hundred year and to beget son: child and daughter
27 Methusela aliishi jumla ya miaka 969, ndipo akafa.
and to be all day Methuselah nine and sixty year and nine hundred year and to die
28 Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.
and to live Lamech two and eighty year and hundred year and to beget son: child
29 Akamwita jina lake Noa, akasema, “Yeye ndiye atakayetufariji katika kazi na maumivu makali ya mikono yetu yaliyosababishwa na ardhi iliyolaaniwa na Bwana.”
and to call: call by [obj] name his Noah to/for to say this to be sorry: comfort us from deed: work our and from toil hand our from [the] land: soil which to curse her LORD
30 Baada ya Noa kuzaliwa, Lameki aliishi miaka 595, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
and to live Lamech after to beget he [obj] Noah five and ninety year and five hundred year and to beget son: child and daughter
31 Lameki aliishi jumla ya miaka 777, ndipo akafa.
and to be all day Lamech seven and seventy year and seven hundred year and to die
32 Baada ya Noa kuishi miaka 500, aliwazaa Shemu, Hamu na Yafethi.
and to be Noah son: aged five hundred year and to beget Noah [obj] Shem [obj] Ham and [obj] Japheth