< Mwanzo 5 >
1 Hii ni orodha iliyoandikwa ya vizazi vya Adamu. Wakati Mungu alipomuumba Adamu, alimfanya kwa sura ya Mungu.
This [is] the genealogy of men in the day in which God made Adam; in the image of God he made him:
2 Aliwaumba mwanaume na mwanamke, akawabariki. Walipokwisha kuumbwa, akawaita “mwanadamu.”
male and female he made them, and blessed them; and he called his name Adam, in the day in which he made them.
3 Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, alikuwa na mwana aliyekuwa na sura yake, mwenye kufanana naye. Akamwita Sethi.
And Adam lived two hundred and thirty years, and begot [a son] after his [own] form, and after his [own] image, and he called his name Seth.
4 Baada ya Sethi kuzaliwa, Adamu aliishi miaka 800, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
And the days of Adam, which he lived after his begetting Seth, were seven hundred years; and he begot sons and daughters.
5 Adamu aliishi jumla ya miaka 930, ndipo akafa.
And all the days of Adam which he lived were nine hundred and thirty years, and he died.
6 Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
Now Seth lived two hundred and five years, and begot Enos.
7 Baada ya kumzaa Enoshi, Sethi aliishi miaka 807, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
And Seth lived after his begetting Enos, seven hundred and seven years, and he begot sons and daughters.
8 Sethi aliishi jumla ya miaka 912, ndipo akafa.
And all the days of Seth were nine hundred and twelve years, and he died.
9 Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
And Enos lived an hundred and ninety years, and begot Cainan.
10 Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815, naye alikuwa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
And Enos lived after his begetting Cainan, seven hundred and fifteen years, and he begot sons and daughters.
11 Enoshi aliishi jumla ya miaka 905, ndipo akafa.
And all the days of Enos were nine hundred and five years, and he died.
12 Kenani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
And Cainan lived an hundred and seventy years, and he begot Maleleel.
13 Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
And Cainan lived after his begetting Maleleel, seven hundred and forty years, and he begot sons and daughters.
14 Kenani aliishi jumla ya miaka 910, ndipo akafa.
And all the days of Cainan were nine hundred and ten years, and he died.
15 Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Yaredi.
And Maleleel lived an hundred and sixty and five years, and he begot Jared.
16 Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
And Maleleel lived after his begetting Jared, seven hundred and thirty years, and he begot sons and daughters.
17 Mahalaleli aliishi jumla ya miaka 895, ndipo akafa.
And all the days of Maleleel were eight hundred and ninety and five years, and he died.
18 Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, akamzaa Enoki.
And Jared lived an hundred and sixty and two years, and begot Enoch:
19 Baada ya kumzaa Enoki, Yaredi aliishi miaka 800, naye akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
and Jared lived after his begetting Enoch, eight hundred years, and he begot sons and daughters.
20 Yaredi aliishi jumla ya miaka 962, ndipo akafa.
And all the days of Jared were nine hundred and sixty and two years, and he died.
21 Enoki alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela.
And Enoch lived an hundred and sixty and five years, and became the father of Mathusala.
22 Baada ya kumzaa Methusela, Enoki alitembea na Mungu miaka 300, na akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
And Enoch was well-pleasing to God after his begetting Mathusala, two hundred years, and he begot sons and daughters.
23 Enoki aliishi jumla ya miaka 365.
And all the days of Enoch were three hundred and sixty and five years.
24 Enoki akatembea na Mungu, kisha akatoweka, kwa sababu Mungu alimchukua.
And Enoch was well-pleasing to God, and was not found, because God translated him.
25 Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, akamzaa Lameki.
And Mathusala lived an hundred and sixty and seven years, and begot Lamech.
26 Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
And Mathusala lived after his begetting Lamech eight hundred and two years, and begot sons and daughters.
27 Methusela aliishi jumla ya miaka 969, ndipo akafa.
And all the days of Mathusala which he lived, were nine hundred and sixty and nine years, and he died.
28 Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.
And Lamech lived an hundred and eighty and eight years, and begot a son.
29 Akamwita jina lake Noa, akasema, “Yeye ndiye atakayetufariji katika kazi na maumivu makali ya mikono yetu yaliyosababishwa na ardhi iliyolaaniwa na Bwana.”
And he called his name Noe, saying, This one will cause us to cease from our works, and from the toils of our hands, and from the earth, which the Lord God has cursed.
30 Baada ya Noa kuzaliwa, Lameki aliishi miaka 595, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
And Lamech lived after his begetting Noe, five hundred and sixty and five years, and begot sons and daughters.
31 Lameki aliishi jumla ya miaka 777, ndipo akafa.
And all the days of Lamech were seven hundred and fifty-three years, and he died.
32 Baada ya Noa kuishi miaka 500, aliwazaa Shemu, Hamu na Yafethi.