< Mwanzo 49 >

1 Ndipo Yakobo akawaita wanawe na kusema: “Kusanyikeni kunizunguka ili niweze kuwaambia lile litakalowatokea siku zijazo.
Jacob chamou seus filhos, e disse: “Reúnam-se, para que eu possa dizer-lhes o que lhes acontecerá nos próximos dias”.
2 “Kusanyikeni na msikilize, enyi wana wa Yakobo, msikilizeni baba yenu Israeli.
Reúnam-se, e ouçam, filhos de Jacob. Ouça Israel, seu pai.
3 “Reubeni, wewe ni mzaliwa wangu wa kwanza, nguvu zangu, tunda la kwanza la nguvu zangu, umepita kwa heshima, umepita kwa uwezo.
“Reuben, você é meu primogênito, minha força e o começo de minha força, Excesso de dignidade e excitação no poder.
4 Usiyezuiwa kama maji, basi hutakuwa mkuu tena, kwa kuwa ulipanda kwenye kitanda cha baba yako, kwenye kitanda changu na kukinajisi.
Boiling como a água, você não deve se sobressair, porque você foi para a cama do seu pai, depois a sujou. Ele foi até o meu sofá.
5 “Simeoni na Lawi ni wana ndugu: panga zao ni silaha za jeuri.
“Simeon e Levi são irmãos. Suas espadas são armas de violência.
6 Mimi na nisiingie katika baraza lao, nami nisiunganike katika kusanyiko lao, kwa kuwa wamewaua watu katika hasira yao, walikata mishipa ya miguu ya mafahali kama walivyopenda.
Minha alma, não venha ao conselho deles. Minha glória, não se unam à sua assembléia; pois em sua raiva mataram homens. Em sua vontade própria, eles manietaram o gado.
7 Hasira yao na ilaaniwe, kwa kuwa ni kali mno, nayo ghadhabu yao ni ya ukatili! Nitawatawanya katika Yakobo Na kuwasambaza katika Israeli.
Amaldiçoada seja a raiva deles, pois foi feroz; e sua ira, pois foi cruel. Vou dividi-los em Jacob, e os espalhe em Israel.
8 “Yuda, ndugu zako watakusifu; mkono wako utakuwa shingoni mwa adui zako; wana wa baba yako watakusujudia.
“Judah, seus irmãos o elogiarão. Sua mão estará sobre o pescoço de seus inimigos. Os filhos de seu pai se curvarão diante de você.
9 Ee Yuda, wewe ni mwana simba; unarudi toka mawindoni, mwanangu. Kama simba hunyemelea na kulala chini, kama simba jike: nani athubutuye kumwamsha?
Judah é uma cria de leão. Da presa, meu filho, você subiu. Ele abaixou-se, agachou-se como um leão, como uma leoa. Quem o despertará?
10 Fimbo ya ufalme haitaondoka kwa Yuda, wala fimbo ya mtawala kati ya miguu yake, hadi aje yeye ambaye milki ni yake, ambaye utii wa mataifa ni wake.
O ceptro não se afastará de Judá, nem o bastão do governante entre seus pés, até que ele venha a quem pertence. A obediência dos povos será para ele.
11 Atamfunga punda wake katika mzabibu, naye mwana-punda wake kwenye tawi lililo bora zaidi; atafua mavazi yake katika divai, majoho yake katika damu ya mizabibu.
Ligando seu potro à videira, o potro de seu burro para a videira escolhida, ele lavou suas peças de vestuário em vinho, suas vestes no sangue das uvas.
12 Macho yake yatakuwa mekundu kwa divai, meno yake yatakuwa meupe kwa maziwa.
Seus olhos ficarão vermelhos com vinho, seus dentes brancos com leite.
13 “Zabuloni ataishi pwani ya bahari na kuwa bandari za kuegesha meli; mpaka wake utapanuka kuelekea Sidoni.
“Zebulun habitará no paraíso do mar. Ele será para um refúgio de navios. Sua fronteira será em Sidon.
14 “Isakari ni punda mwenye nguvu ambaye amelala kati ya mizigo yake.
“Issachar é um burro forte, deitado entre os alforges.
15 Aonapo palivyo pazuri mahali pake pa kupumzika na jinsi nchi yake inavyopendeza, atainamisha bega lake kwenye mzigo na kujitolea kwa ajili ya kazi ngumu.
Ele viu um lugar de descanso, que era bom, a terra, que era agradável. Ele se curva ao peso do peso, e se torna um servo fazendo trabalhos forçados.
16 “Dani atahukumu watu wake kwa haki kama mmoja wa makabila ya Israeli.
“Dan irá julgar seu povo, como uma das tribos de Israel.
17 Dani atakuwa nyoka kando ya barabara, nyoka mwenye sumu kando ya njia, yule aumaye visigino vya farasi ili yule ampandaye aanguke chali.
Dan será uma serpente na trilha, uma víbora no caminho, que morde os calcanhares do cavalo, para que seu cavaleiro caia para trás.
18 “Ee Bwana, nautafuta wokovu wako.
Esperei por sua salvação, Yahweh.
19 “Gadi atashambuliwa ghafula na kundi la washambuliaji, lakini yeye atawageukia na kuwashinda kabisa.
“Uma tropa vai pressionar o Gad, mas ele vai pressionar o calcanhar deles.
20 “Chakula cha Asheri kitakuwa kinono, naye atatoa chakula kitamu kimfaacho mfalme.
“A comida do Asher será rica. Ele produzirá delicadezas reais.
21 “Naftali ni kulungu jike aliyeachiwa huru azaaye watoto wazuri.
“Naftali é uma corça libertada, que carrega belos peões.
22 “Yosefu ni mzabibu uzaao, mzabibu uzaao ulio kando ya chemchemi, ambao matawi yake hutanda ukutani.
“Joseph é uma videira frutífera, uma videira frutífera por uma fonte. Seus ramos correm sobre a parede.
23 Kwa uchungu wapiga mshale walimshambulia, wakampiga mshale kwa ukatili.
The os arqueiros o entristeceram gravemente, atirou nele, e o perseguiu:
24 Lakini upinde wake ulibaki imara, mikono yake ikatiwa nguvu, na mkono wa Mwenye Nguvu wa Yakobo, kwa sababu ya Mchungaji, Mwamba wa Israeli,
Mas seu arco permaneceu forte. Os braços de suas mãos foram tornados fortes, pelas mãos do Poderoso de Jacob, (de lá é o pastor, a pedra de Israel),
25 kwa sababu ya Mungu wa baba yako, anayekusaidia, kwa sababu ya Mwenyezi, yeye anayekubariki kwa baraka za mbinguni juu, baraka za kilindi kilichoko chini, baraka za matitini na za tumbo la uzazi.
mesmo pelo Deus de seu pai, que o ajudará, pelo Todo-Poderoso, que o abençoará, com as bênçãos do céu acima, bênçãos das profundezas que se encontram abaixo, bênçãos dos seios, e do útero.
26 Baraka za baba yako ni kubwa kuliko baraka za milima ya kale, nyingi kuliko vilima vya kale. Baraka hizo zote na zikae juu ya kichwa cha Yosefu, juu ya paji la yule mkuu miongoni mwa ndugu zake.
As bênçãos de seu pai prevaleceram sobre as bênçãos de meus antepassados, acima dos limites das colinas antigas. Eles ficarão na cabeça de José, sobre a coroa da cabeça daquele que está separado de seus irmãos.
27 “Benyamini ni mbwa mwitu mlafi mwenye njaa kuu; asubuhi hurarua mawindo yake, jioni hugawa nyara.”
“Benjamin é um lobo esfomeado. Pela manhã, ele devorará a presa. À noite, ele dividirá o saque”.
28 Haya yote ndiyo makabila kumi na mawili ya Israeli, na hivi ndivyo baba yao alivyowaambia alipowabariki, akimpa kila mmoja baraka inayomfaa.
Todas estas são as doze tribos de Israel, e foi isto que seu pai lhes falou, e os abençoou. Ele abençoou a todos de acordo com sua própria bênção.
29 Ndipo alipowapa maelekezo haya: “Mimi niko karibu kukusanywa kwa watu wangu. Mnizike pamoja na baba zangu kwenye pango katika shamba la Efroni, Mhiti,
Ele os instruiu e lhes disse: “Vou ser reunido ao meu povo”. Enterrem-me com meus pais na caverna que está no campo de Efron, o hitita,
30 pango lililoko katika shamba la Makpela, karibu na Mamre huko Kanaani, ambalo Abrahamu alinunua kwa ajili ya mahali pa kuzikia kutoka kwa Efroni, Mhiti, pamoja na shamba.
na caverna que está no campo de Machpelah, que está antes de Mamre, na terra de Canaã, que Abraão comprou com o campo de Efron, o hitita, como local de sepultamento.
31 Huko ndiko Abrahamu na Sara mkewe walikozikwa, huko akazikwa Isaki na Rebeka mkewe, na huko nilimzika Lea.
Ali enterraram Abraão e Sara, sua esposa. Ali enterraram Isaac e Rebekah, sua esposa, e ali enterrei Leah:
32 Shamba hilo na pango lililoko ndani yake lilinunuliwa kutoka kwa Wahiti.”
o campo e a caverna que lá se encontra, que foi comprada dos filhos de Heth”.
33 Baada ya Yakobo kumaliza kutoa maelekezo hayo kwa wanawe, akarudisha miguu yake kitandani, akapumua pumzi ya mwisho, na akakusanywa kwa watu wake.
Quando Jacó terminou de carregar seus filhos, ele levantou os pés na cama, deu seu último suspiro e foi reunido ao seu povo.

< Mwanzo 49 >