< Mwanzo 49 >

1 Ndipo Yakobo akawaita wanawe na kusema: “Kusanyikeni kunizunguka ili niweze kuwaambia lile litakalowatokea siku zijazo.
Or Jacob appela ses fils et leur dit: Assemblez-vous, afin que je vous annonce ce qui doit vous arriver dans les jours derniers.
2 “Kusanyikeni na msikilize, enyi wana wa Yakobo, msikilizeni baba yenu Israeli.
Assemblez-vous, et écoutez, fils de Jacob, écoutez Israël votre père:
3 “Reubeni, wewe ni mzaliwa wangu wa kwanza, nguvu zangu, tunda la kwanza la nguvu zangu, umepita kwa heshima, umepita kwa uwezo.
Ruben, mon premier-né, toi ma force et le principe de ma douleur; premier en dons, plus grand en puissance,
4 Usiyezuiwa kama maji, basi hutakuwa mkuu tena, kwa kuwa ulipanda kwenye kitanda cha baba yako, kwenye kitanda changu na kukinajisi.
Tu t’es répandu comme l’eau; tu ne croîtras pas, parce que tu es monté sur le lit de ton père, et que tu as souillé sa couche.
5 “Simeoni na Lawi ni wana ndugu: panga zao ni silaha za jeuri.
Siméon et Lévi sont frères, instruments d’iniquité dans le combat.
6 Mimi na nisiingie katika baraza lao, nami nisiunganike katika kusanyiko lao, kwa kuwa wamewaua watu katika hasira yao, walikata mishipa ya miguu ya mafahali kama walivyopenda.
Que dans leur conseil n’entre pas mon âme, et que dans leurs assemblées ne se trouve pas ma gloire, parce que dans leur fureur, ils ont tué un homme, et que dans leur résolution ils ont renversé un mur.
7 Hasira yao na ilaaniwe, kwa kuwa ni kali mno, nayo ghadhabu yao ni ya ukatili! Nitawatawanya katika Yakobo Na kuwasambaza katika Israeli.
Maudite leur fureur, parce qu’elle est opiniâtre, et leur indignation, parce qu’elle est implacable! je les diviserai dans Jacob, et je les disperserai dans Israël.
8 “Yuda, ndugu zako watakusifu; mkono wako utakuwa shingoni mwa adui zako; wana wa baba yako watakusujudia.
Juda, tes frères te loueront; ta main sera sur le cou de tes ennemis; les enfants de ton père se prosterneront devant toi.
9 Ee Yuda, wewe ni mwana simba; unarudi toka mawindoni, mwanangu. Kama simba hunyemelea na kulala chini, kama simba jike: nani athubutuye kumwamsha?
C’est le petit d’un lion, que Juda. Tu t’es élancé sur la proie, ô mon fils: te reposant, tu t’es couché comme le lion et comme la lionne; qui le provoquera?
10 Fimbo ya ufalme haitaondoka kwa Yuda, wala fimbo ya mtawala kati ya miguu yake, hadi aje yeye ambaye milki ni yake, ambaye utii wa mataifa ni wake.
Le sceptre ne sera pas ôté de Juda, ni le prince de sa postérité, jusqu’à ce que vienne celui qui doit être envoyé, et lui-même sera l’attente des nations.
11 Atamfunga punda wake katika mzabibu, naye mwana-punda wake kwenye tawi lililo bora zaidi; atafua mavazi yake katika divai, majoho yake katika damu ya mizabibu.
Il liera, ô mon fils, à la vigne son ânon, et au cep son ânesse. Il lavera dans le vin sa robe, et dans le sang du raisin son manteau.
12 Macho yake yatakuwa mekundu kwa divai, meno yake yatakuwa meupe kwa maziwa.
Ses yeux sont plus beaux que le vin, et ses dents plus blanches que le lait.
13 “Zabuloni ataishi pwani ya bahari na kuwa bandari za kuegesha meli; mpaka wake utapanuka kuelekea Sidoni.
Zabulon habitera sur le rivage de la mer, et près du port des navires, s’étendant jusqu’à Sidon.
14 “Isakari ni punda mwenye nguvu ambaye amelala kati ya mizigo yake.
Issachar, âne robuste, couché au milieu de son héritage.
15 Aonapo palivyo pazuri mahali pake pa kupumzika na jinsi nchi yake inavyopendeza, atainamisha bega lake kwenye mzigo na kujitolea kwa ajili ya kazi ngumu.
Il a vu que le repos était bon, et que sa terre était excellente; il a soumis son épaule aux fardeaux, et il s’est assujetti aux tributs.
16 “Dani atahukumu watu wake kwa haki kama mmoja wa makabila ya Israeli.
Dan jugera son peuple, aussi bien qu’une autre tribu en Israël.
17 Dani atakuwa nyoka kando ya barabara, nyoka mwenye sumu kando ya njia, yule aumaye visigino vya farasi ili yule ampandaye aanguke chali.
Que Dan devienne un serpent sur le chemin, un céraste dans le sentier, mordant le talon du cheval, afin que son cavalier tombe à la renverse.
18 “Ee Bwana, nautafuta wokovu wako.
C’est votre Salut que j’attendrai, Seigneur.
19 “Gadi atashambuliwa ghafula na kundi la washambuliaji, lakini yeye atawageukia na kuwashinda kabisa.
Gad tout armé combattra devant lui; et lui-même se revêtira de ses armes en arrière.
20 “Chakula cha Asheri kitakuwa kinono, naye atatoa chakula kitamu kimfaacho mfalme.
Aser, gras est son pain, et il fournira des délices aux rois
21 “Naftali ni kulungu jike aliyeachiwa huru azaaye watoto wazuri.
Nephthali, cerf échappé; il donne des paroles pleines de beauté.
22 “Yosefu ni mzabibu uzaao, mzabibu uzaao ulio kando ya chemchemi, ambao matawi yake hutanda ukutani.
Joseph, fils croissant, fils croissant et beau à voir: les jeunes filles ont couru sur la muraille.
23 Kwa uchungu wapiga mshale walimshambulia, wakampiga mshale kwa ukatili.
Mais ils l’ont irrité, ils l’ont querellé, et ils lui ont porté envie, ceux qui avaient des dards.
24 Lakini upinde wake ulibaki imara, mikono yake ikatiwa nguvu, na mkono wa Mwenye Nguvu wa Yakobo, kwa sababu ya Mchungaji, Mwamba wa Israeli,
Son arc s’est appuyé sur le fort; les liens de ses bras et de ses mains ont été brisés par les mains du puissant de Jacob; de là il est sorti pasteur, pierre d’Israël.
25 kwa sababu ya Mungu wa baba yako, anayekusaidia, kwa sababu ya Mwenyezi, yeye anayekubariki kwa baraka za mbinguni juu, baraka za kilindi kilichoko chini, baraka za matitini na za tumbo la uzazi.
Le Dieu de ton père sera ton soutien, et le Tout-Puissant te bénira des bénédictions célestes d’en haut, des bénédictions de l’abîme qui est en bas, des bénédictions de mamelles et de sein.
26 Baraka za baba yako ni kubwa kuliko baraka za milima ya kale, nyingi kuliko vilima vya kale. Baraka hizo zote na zikae juu ya kichwa cha Yosefu, juu ya paji la yule mkuu miongoni mwa ndugu zake.
Les bénédictions de ton père seront fortifiées par les bénédictions de ses pères jusqu’à ce que vienne le désir des collines éternelles; qu’elles se répandent sur la tête de Joseph et sur la tête de celui qui est Nazaréen entre ses frères.
27 “Benyamini ni mbwa mwitu mlafi mwenye njaa kuu; asubuhi hurarua mawindo yake, jioni hugawa nyara.”
Benjamin, loup ravissant: le matin, il dévorera la proie, et le soir, il partagera les dépouilles.
28 Haya yote ndiyo makabila kumi na mawili ya Israeli, na hivi ndivyo baba yao alivyowaambia alipowabariki, akimpa kila mmoja baraka inayomfaa.
Tous ceux-là sont les douze dans les tribus d’Israël: ainsi leur parla leur père, et il les bénit les uns après les autres des bénédictions propres à chacun deux.
29 Ndipo alipowapa maelekezo haya: “Mimi niko karibu kukusanywa kwa watu wangu. Mnizike pamoja na baba zangu kwenye pango katika shamba la Efroni, Mhiti,
Et il leur commanda, disant; Je vais être réuni à mon peuple: ensevelissez-moi avec mes pères dans la caverne double qui est dans le champ d’Ephron l’Hétéen,
30 pango lililoko katika shamba la Makpela, karibu na Mamre huko Kanaani, ambalo Abrahamu alinunua kwa ajili ya mahali pa kuzikia kutoka kwa Efroni, Mhiti, pamoja na shamba.
Vis-à-vis de Mambré dans la terre de Chanaan, et qu’Abraham acheta d’Ephron l’Hétéen, avec le champ, pour y posséder un sépulcre.
31 Huko ndiko Abrahamu na Sara mkewe walikozikwa, huko akazikwa Isaki na Rebeka mkewe, na huko nilimzika Lea.
C’est là qu’on l’a enseveli lui et Sara sa femme: là a été enseveli Isaac avec Rébecca sa femme: là aussi, ensevelie, repose Lia.
32 Shamba hilo na pango lililoko ndani yake lilinunuliwa kutoka kwa Wahiti.”
Les recommandations qu’il adressait à ses fils achevées, il retira ses pieds sur son lit, et mourut; et il fut réuni à son peuple.
33 Baada ya Yakobo kumaliza kutoa maelekezo hayo kwa wanawe, akarudisha miguu yake kitandani, akapumua pumzi ya mwisho, na akakusanywa kwa watu wake.

< Mwanzo 49 >