< Mwanzo 49 >
1 Ndipo Yakobo akawaita wanawe na kusema: “Kusanyikeni kunizunguka ili niweze kuwaambia lile litakalowatokea siku zijazo.
Et Jacob fit venir ses fils et dit: Rassemblez-vous, je vais vous découvrir ce qui vous arrivera dans les temps à venir!
2 “Kusanyikeni na msikilize, enyi wana wa Yakobo, msikilizeni baba yenu Israeli.
Réunissez-vous, et écoutez, fils de Jacob, écoutez Israël, votre père.
3 “Reubeni, wewe ni mzaliwa wangu wa kwanza, nguvu zangu, tunda la kwanza la nguvu zangu, umepita kwa heshima, umepita kwa uwezo.
Ruben, tu es mon premier-né, ma vigueur, et les prémices de ma virilité; tu as la prééminence du rang, la prééminence de la force.
4 Usiyezuiwa kama maji, basi hutakuwa mkuu tena, kwa kuwa ulipanda kwenye kitanda cha baba yako, kwenye kitanda changu na kukinajisi.
Toi qui bous comme les eaux, tu perdras ton rang! car tu es monté au lit de ton père, tu l'as profané!… c'est dans ma couche qu'il est monté!
5 “Simeoni na Lawi ni wana ndugu: panga zao ni silaha za jeuri.
Siméon et Lévi sont des frères; leurs glaives furent instruments de violence.
6 Mimi na nisiingie katika baraza lao, nami nisiunganike katika kusanyiko lao, kwa kuwa wamewaua watu katika hasira yao, walikata mishipa ya miguu ya mafahali kama walivyopenda.
Que mon âme n'entre point en leur conseil, que ma personne ne se joigne point à leur ligue! Dans leur courroux ils ont tué des hommes, et dans leur passion coupé les nerfs des taureaux.
7 Hasira yao na ilaaniwe, kwa kuwa ni kali mno, nayo ghadhabu yao ni ya ukatili! Nitawatawanya katika Yakobo Na kuwasambaza katika Israeli.
Maudit soit leur courroux, car il fut violent, et leur fureur, car elle fut cruelle! Je les distribuerai dans Jacob et les disséminerai dans Israël.
8 “Yuda, ndugu zako watakusifu; mkono wako utakuwa shingoni mwa adui zako; wana wa baba yako watakusujudia.
Juda, c'est toi que tes frères loueront; ta main saisit le col de tes ennemis, les fils de ton père s'inclineront devant toi.
9 Ee Yuda, wewe ni mwana simba; unarudi toka mawindoni, mwanangu. Kama simba hunyemelea na kulala chini, kama simba jike: nani athubutuye kumwamsha?
Juda est un jeune lion, après la capture, tu reviens, mon fils! il se replie, il se rase comme le lion, comme la lionne, qui le fera lever?
10 Fimbo ya ufalme haitaondoka kwa Yuda, wala fimbo ya mtawala kati ya miguu yake, hadi aje yeye ambaye milki ni yake, ambaye utii wa mataifa ni wake.
Le sceptre ne se retire point de Juda, ni le bâton de l'empire d'entre ses pieds, jusqu'à ce qu'il entre à Silo, et que les peuples lui rendent obéissance.
11 Atamfunga punda wake katika mzabibu, naye mwana-punda wake kwenye tawi lililo bora zaidi; atafua mavazi yake katika divai, majoho yake katika damu ya mizabibu.
Il attache son âne à la vigne, et au noble cep le poulain de son ânesse; il baigne son habit dans le vin, et son manteau dans le sang du raisin;
12 Macho yake yatakuwa mekundu kwa divai, meno yake yatakuwa meupe kwa maziwa.
le vin fait étinceler ses yeux, et le lait blanchit ses dents.
13 “Zabuloni ataishi pwani ya bahari na kuwa bandari za kuegesha meli; mpaka wake utapanuka kuelekea Sidoni.
Zabulon habite la plage de la mer, il habite la plage des navires, et ses confins atteignent à Sidon.
14 “Isakari ni punda mwenye nguvu ambaye amelala kati ya mizigo yake.
Issaschar, âne robuste, repose entre les parcs,
15 Aonapo palivyo pazuri mahali pake pa kupumzika na jinsi nchi yake inavyopendeza, atainamisha bega lake kwenye mzigo na kujitolea kwa ajili ya kazi ngumu.
et voyant la beauté de son lieu de son repos, et les agréments de la contrée, il présente son épaule au fardeau, et fait le service des corvées.
16 “Dani atahukumu watu wake kwa haki kama mmoja wa makabila ya Israeli.
Dan juge son peuple, comme chacune des tribus d'Israël.
17 Dani atakuwa nyoka kando ya barabara, nyoka mwenye sumu kando ya njia, yule aumaye visigino vya farasi ili yule ampandaye aanguke chali.
Dan est un serpent sur le chemin, un céraste sur le sentier, il mord les pâturons des chevaux, et le cavalier tombe à la renverse.
18 “Ee Bwana, nautafuta wokovu wako.
C'est ton salut que j'attends, Éternel!…
19 “Gadi atashambuliwa ghafula na kundi la washambuliaji, lakini yeye atawageukia na kuwashinda kabisa.
Gad est assailli par des escadrons, mais il assaille l'arrière-garde.
20 “Chakula cha Asheri kitakuwa kinono, naye atatoa chakula kitamu kimfaacho mfalme.
D'Asser sort le pain savoureux, il fournit les friandises des rois.
21 “Naftali ni kulungu jike aliyeachiwa huru azaaye watoto wazuri.
Nephthali est une biche élancée: il prononce des discours élégants.
22 “Yosefu ni mzabibu uzaao, mzabibu uzaao ulio kando ya chemchemi, ambao matawi yake hutanda ukutani.
Joseph est le rameau d'un arbre fécond, le rameau d'un arbre fécond près d'une source, ses jets franchissent la muraille.
23 Kwa uchungu wapiga mshale walimshambulia, wakampiga mshale kwa ukatili.
On le provoque, on tire, et les archers le poursuivent;
24 Lakini upinde wake ulibaki imara, mikono yake ikatiwa nguvu, na mkono wa Mwenye Nguvu wa Yakobo, kwa sababu ya Mchungaji, Mwamba wa Israeli,
mais son arc reste ferme et ses mains ont force et souplesse. Que la main du Héros de Jacob, du lieu où réside le Berger et le Rocher d'Israël,
25 kwa sababu ya Mungu wa baba yako, anayekusaidia, kwa sababu ya Mwenyezi, yeye anayekubariki kwa baraka za mbinguni juu, baraka za kilindi kilichoko chini, baraka za matitini na za tumbo la uzazi.
la main du Dieu de ton père, qui fut ton aide, du Tout-Puissant qui t'a béni, répande les bénédictions du ciel exhaussé, les bénédictions des ondes de la couche inférieure, les bénédictions des mamelles et de la maternité.
26 Baraka za baba yako ni kubwa kuliko baraka za milima ya kale, nyingi kuliko vilima vya kale. Baraka hizo zote na zikae juu ya kichwa cha Yosefu, juu ya paji la yule mkuu miongoni mwa ndugu zake.
La bénédiction de ton père est supérieure à la bénédiction des monts élevés, aux attraits des coteaux éternels: qu'elle repose sur la tête de Joseph, sur le front du prince de ses frères!
27 “Benyamini ni mbwa mwitu mlafi mwenye njaa kuu; asubuhi hurarua mawindo yake, jioni hugawa nyara.”
Benjamin est le loup qui déchire; le matin il dévore une proie, et le soir il partage le butin.
28 Haya yote ndiyo makabila kumi na mawili ya Israeli, na hivi ndivyo baba yao alivyowaambia alipowabariki, akimpa kila mmoja baraka inayomfaa.
Tels sont tous ceux qui forment les tribus d'Israël, douze en nombre, et telles sont les paroles que leur adressa leur père; et c'est ainsi qu'il les bénit, leur donnant à chacun une bénédiction particulière.
29 Ndipo alipowapa maelekezo haya: “Mimi niko karibu kukusanywa kwa watu wangu. Mnizike pamoja na baba zangu kwenye pango katika shamba la Efroni, Mhiti,
Et il leur laissa ses instructions en ces termes: Je vais être recueilli auprès de mon peuple; vous me donnerez la sépulture à côté de mes pères dans la grotte du champ de Ephron le Héthien,
30 pango lililoko katika shamba la Makpela, karibu na Mamre huko Kanaani, ambalo Abrahamu alinunua kwa ajili ya mahali pa kuzikia kutoka kwa Efroni, Mhiti, pamoja na shamba.
dans la grotte du champ de Macpéla à l'orient de Mamré au pays de Canaan, qu'Abraham a achetée de Ephron le Héthien, avec le champ comme propriété sépulcrale;
31 Huko ndiko Abrahamu na Sara mkewe walikozikwa, huko akazikwa Isaki na Rebeka mkewe, na huko nilimzika Lea.
c'est là qu'ont reçu la sépulture Abraham et Sarah, sa femme; c'est là qu'ont reçu la sépulture Isaac et Rebecca, sa femme, et c'est là que j'ai donné la sépulture à Léa,
32 Shamba hilo na pango lililoko ndani yake lilinunuliwa kutoka kwa Wahiti.”
dans le champ acheté des enfants de Heth, et dans la grotte qui s'y trouve.
33 Baada ya Yakobo kumaliza kutoa maelekezo hayo kwa wanawe, akarudisha miguu yake kitandani, akapumua pumzi ya mwisho, na akakusanywa kwa watu wake.
Et lorsque Jacob eut achevé de donner ses ordres à ses fils, il assembla ses pieds sur le lit, et il expira et fut recueilli auprès de ses pères.