< Mwanzo 49 >

1 Ndipo Yakobo akawaita wanawe na kusema: “Kusanyikeni kunizunguka ili niweze kuwaambia lile litakalowatokea siku zijazo.
Te phoeiah Jakob loh a ca rhoek te a khue tih, “Tun ngol uh lamtah, vuenvai ah nangmih taengah aka thoeng ham te nangmih taengah ka puen pawn ni,
2 “Kusanyikeni na msikilize, enyi wana wa Yakobo, msikilizeni baba yenu Israeli.
Jakob ca rhoek loh a yaak uh tih a coi uh thae vaengah, “Na pa Israel kah ol te ya uh van lah.
3 “Reubeni, wewe ni mzaliwa wangu wa kwanza, nguvu zangu, tunda la kwanza la nguvu zangu, umepita kwa heshima, umepita kwa uwezo.
Reuben nang he ka caming tih, ka thadueng neh, ka thahuem cuek, hlangrhuel boeimang, hlangtlung hlangrhuel la na om dae,
4 Usiyezuiwa kama maji, basi hutakuwa mkuu tena, kwa kuwa ulipanda kwenye kitanda cha baba yako, kwenye kitanda changu na kukinajisi.
Na pa kah tih thingkong sola na yoeng tih, ka rhaenghmuen te na poeih phoeiah, tui bangla na soetaenah dongah caknoi khaw na khueh mahpawh.
5 “Simeoni na Lawi ni wana ndugu: panga zao ni silaha za jeuri.
Simeon neh Levi boeina, amih rhoi kah tubael tah kuthlahnah tumca ni.
6 Mimi na nisiingie katika baraza lao, nami nisiunganike katika kusanyiko lao, kwa kuwa wamewaua watu katika hasira yao, walikata mishipa ya miguu ya mafahali kama walivyopenda.
Amih rhoi kah tingtunnah dongah ka hinglu naepkhap pawh. Amah rhoi kah thintoek dongah hlang a ngawn rhoi tih vaito kaprhui haih ham te amih rhoi kah kolonah la a om dongah, kai kah thangpomnah loh amih rhoi a hlangping te bulbo boel saeh.
7 Hasira yao na ilaaniwe, kwa kuwa ni kali mno, nayo ghadhabu yao ni ya ukatili! Nitawatawanya katika Yakobo Na kuwasambaza katika Israeli.
Amih rhoi kah a thinpom khaw a tlung dongah a thintoek te thae a phoei thil. Te dongah a mangkhak te Jakob taengah ka tael vetih Israel taengah khaw ka taekyak ni.
8 “Yuda, ndugu zako watakusifu; mkono wako utakuwa shingoni mwa adui zako; wana wa baba yako watakusujudia.
Judah nang he na manuca rhoek loh nang n'uem uh ni. Na kut te na thunkha a rhawn dongla cu ni. Na pacaboeina te nang taengah bakop uh ni.
9 Ee Yuda, wewe ni mwana simba; unarudi toka mawindoni, mwanangu. Kama simba hunyemelea na kulala chini, kama simba jike: nani athubutuye kumwamsha?
Judah he sathueng ca ni. Ka ca loh maeh kung lamkah na bal phoeiah, sathueng neh sathuengnu bangla aka yuel tih, aka kol te ulong anih a haeng eh.
10 Fimbo ya ufalme haitaondoka kwa Yuda, wala fimbo ya mtawala kati ya miguu yake, hadi aje yeye ambaye milki ni yake, ambaye utii wa mataifa ni wake.
Judah lamkah mancai tah nong boel lamtah, a kho laklo lamloh taem saeh. Shiloh a pha duela anih taengah, pilnam kah boengainah om saeh.
11 Atamfunga punda wake katika mzabibu, naye mwana-punda wake kwenye tawi lililo bora zaidi; atafua mavazi yake katika divai, majoho yake katika damu ya mizabibu.
A laaktal, laaktal te misur dongah, a laak ca te cangsawt misur dongah pael saeh. A pueinak te misurtui dongah, a hnipup, hnipup te misur thii dongah til saeh.
12 Macho yake yatakuwa mekundu kwa divai, meno yake yatakuwa meupe kwa maziwa.
Na mik khaw musurtui lakah ling vetih, na no te suktui lakah bok ni.
13 “Zabuloni ataishi pwani ya bahari na kuwa bandari za kuegesha meli; mpaka wake utapanuka kuelekea Sidoni.
Zebulun he tuitunli kah langkaeng ah khosa saeh lamtah, langkaeng kah sangpho rhoek bangla a bawtnah loh Sidon due pha saeh.
14 “Isakari ni punda mwenye nguvu ambaye amelala kati ya mizigo yake.
Issakhar he laak songrhuh bangla saelvong laklo ah na kol.
15 Aonapo palivyo pazuri mahali pake pa kupumzika na jinsi nchi yake inavyopendeza, atainamisha bega lake kwenye mzigo na kujitolea kwa ajili ya kazi ngumu.
Duemnah then neh khohmuen hlahmae te khaw a hmuh dae, phueih te a laengpang ah a thueng tih aka thotat saldong la om ni.
16 “Dani atahukumu watu wake kwa haki kama mmoja wa makabila ya Israeli.
Dan he Israel koca pakhat vanbangla a pilnam kah lai a thui pah ni.
17 Dani atakuwa nyoka kando ya barabara, nyoka mwenye sumu kando ya njia, yule aumaye visigino vya farasi ili yule ampandaye aanguke chali.
Dan he long taengkah rhul neh marhang dongkah aka ngol te a hnuk la bung saeh tila marhang khomik aka maeng tih, caehlong rhulthae bangla om ni.
18 “Ee Bwana, nautafuta wokovu wako.
BOEIPA nang kah khangnah ham ni ka lamtawn he.
19 “Gadi atashambuliwa ghafula na kundi la washambuliaji, lakini yeye atawageukia na kuwashinda kabisa.
Gad he caem loh tloek cakhaw anih loh a khomik a tloek pah ni.
20 “Chakula cha Asheri kitakuwa kinono, naye atatoa chakula kitamu kimfaacho mfalme.
Asher ham caak bae vetih, manghai buhmong a tael ni.
21 “Naftali ni kulungu jike aliyeachiwa huru azaaye watoto wazuri.
Naphtali tah sayukrhuinu bangla khocaeh dangka vetih, ol then a thui ni.
22 “Yosefu ni mzabibu uzaao, mzabibu uzaao ulio kando ya chemchemi, ambao matawi yake hutanda ukutani.
Joseph tah a ca loh thaihsu tih, a ca loh tuiphuet taengkah pungtai. Ngannu ngankhong loh pangbueng dongla luei.
23 Kwa uchungu wapiga mshale walimshambulia, wakampiga mshale kwa ukatili.
Thaltang boei rhoek a konaeh uh dongah, a phaep uh tih a kah uh.
24 Lakini upinde wake ulibaki imara, mikono yake ikatiwa nguvu, na mkono wa Mwenye Nguvu wa Yakobo, kwa sababu ya Mchungaji, Mwamba wa Israeli,
Tedae Jakob kah samrhang kut rhang neh, Israel aka dawn lungnu rhang neh,
25 kwa sababu ya Mungu wa baba yako, anayekusaidia, kwa sababu ya Mwenyezi, yeye anayekubariki kwa baraka za mbinguni juu, baraka za kilindi kilichoko chini, baraka za matitini na za tumbo la uzazi.
Na pa kah Pathen loh nang m'bom tih Tlungthang loh nang te vaan a sosang kah yoethennah, a laedil kah aka kol yoethennah nen khaw, a rhangsuk dongkah yoethennah nen khaw, a bung khuikah nen khaw yoethen m'paek dongah, a li khaw tangkuek la om tih, a kut bantha khaw caang.
26 Baraka za baba yako ni kubwa kuliko baraka za milima ya kale, nyingi kuliko vilima vya kale. Baraka hizo zote na zikae juu ya kichwa cha Yosefu, juu ya paji la yule mkuu miongoni mwa ndugu zake.
Na pa kah yoethennah he kai aka yom kah yoethennah lakah len. Khosuen som ah a saelongnah hil Joseph lu so neh a manuca hlangcoelh luki soah om saeh.
27 “Benyamini ni mbwa mwitu mlafi mwenye njaa kuu; asubuhi hurarua mawindo yake, jioni hugawa nyara.”
Benjamin, uithang laihat loh, mincang ah maeh a ngaeh, hlaem ah kutbuem a tael,” a ti nah.
28 Haya yote ndiyo makabila kumi na mawili ya Israeli, na hivi ndivyo baba yao alivyowaambia alipowabariki, akimpa kila mmoja baraka inayomfaa.
A pum boeih la Israel koca he hlai nit dongah a napa loh amih taengah a thui vaengah amah kah yoethennah neh amih te yoethen rhip a paek.
29 Ndipo alipowapa maelekezo haya: “Mimi niko karibu kukusanywa kwa watu wangu. Mnizike pamoja na baba zangu kwenye pango katika shamba la Efroni, Mhiti,
Te phoeiah amih te a uen tih, “Kai he ka pilnam taengla ka khum atah a pa rhoek neh Khitti Ephron lo kah lungko ah n'up uh.
30 pango lililoko katika shamba la Makpela, karibu na Mamre huko Kanaani, ambalo Abrahamu alinunua kwa ajili ya mahali pa kuzikia kutoka kwa Efroni, Mhiti, pamoja na shamba.
Kanaan kho Mamre hmai, Makpelah lo kah lungko te phuel khohut la Khitti Ephron taeng lamkah Abraham loh a lai khohmuen ni.
31 Huko ndiko Abrahamu na Sara mkewe walikozikwa, huko akazikwa Isaki na Rebeka mkewe, na huko nilimzika Lea.
Ti ah te Abraham neh a yuu Sarah a up uh tih Isaak neh a yuu Rebekah te pahoi a up uh coeng. Leah khaw pahoi ka up coeng.
32 Shamba hilo na pango lililoko ndani yake lilinunuliwa kutoka kwa Wahiti.”
Te dongah Kheth ca rhoek taeng lamkah te khohmuen boiva neh a khuikah lungko te,” a ti nah.
33 Baada ya Yakobo kumaliza kutoa maelekezo hayo kwa wanawe, akarudisha miguu yake kitandani, akapumua pumzi ya mwisho, na akakusanywa kwa watu wake.
Jakob loh a ca rhoek a uen te a khah phoeiah baiphaih dongla a kho a yueh. Te phoeiah pal tih a pilnam taengla khoem uh.

< Mwanzo 49 >