< Mwanzo 48 >

1 Baada ya muda Yosefu akaambiwa kwamba, “Baba yako ni mgonjwa.” Kwa hiyo akawachukua wanawe wawili Manase na Efraimu, pamoja naye.
Après ces choses, quelqu'un dit à Joseph: « Voici ton père qui est malade. » Il prit avec lui ses deux fils, Manassé et Éphraïm.
2 Yakobo alipoambiwa, “Mwanao Yosefu amekujia kukuona,” Israeli akakusanya nguvu zake, akaketi kitandani.
Quelqu'un en informa Jacob, et dit: « Voici ton fils Joseph qui vient vers toi. » Israël se fortifia, et s'assit sur le lit.
3 Yakobo akamwambia Yosefu, “Mungu Mwenyezi alinitokea huko Luzu katika nchi ya Kanaani, huko akanibariki,
Jacob dit à Joseph: « Le Dieu tout-puissant m'est apparu à Luz, au pays de Canaan, et il m'a béni.
4 naye akaniambia, ‘Nitakufanya ustawi na kuongezeka hesabu yako, nitakufanya kuwa jamii ya mataifa, nami nitakupa nchi hii uimiliki milele wewe na wazao wako baada yako.’
Il m'a dit: « Voici, je te rendrai fécond, je te multiplierai, je ferai de toi une multitude de peuples, et je donnerai ce pays à ta postérité après toi, comme possession éternelle.
5 “Sasa basi, wanao wawili waliozaliwa kwako huku Misri kabla sijaja hapa kwako watahesabiwa kuwa ni wangu; Efraimu na Manase watakuwa wangu, kama vile Reubeni na Simeoni walivyo wangu.
Or, tes deux fils, qui te sont nés au pays d'Égypte avant que je ne vienne vers toi en Égypte, sont à moi; Éphraïm et Manassé, comme Ruben et Siméon, seront à moi.
6 Lakini watoto utakaowazaa baada yao watakuwa wako. Katika nchi watakayoirithi, watatambuliwa kwa jina la ndugu zao.
Ta descendance, que tu auras engendrée après eux, sera à toi. Ils seront appelés du nom de leurs frères dans leur héritage.
7 Nilipokuwa ninarudi kutoka Padani, katika huzuni yangu Raheli alifariki katika nchi ya Kanaani tulipokuwa tungali tukisafiri, tukiwa karibu kufika Efrathi. Kwa hiyo nilimzika huko, kando ya njia iendayo Efrathi” (yaani Bethlehemu).
Quant à moi, quand je suis venu de Paddan, Rachel est morte près de moi au pays de Canaan, en chemin, alors qu'il y avait encore de la distance à parcourir jusqu'à Éphrata, et je l'ai enterrée là, sur le chemin d'Éphrata (appelée aussi Bethléem). »
8 Wakati Israeli alipowaona wana wa Yosefu, akauliza, “Hawa ni nani?”
Israël vit les fils de Joseph, et dit: « Qui sont ceux-ci? »
9 Yosefu akamjibu baba yake, “Hawa ni wana ambao Mungu amenipa nikiwa huku.” Ndipo Israeli akasema, “Walete kwangu ili niwabariki.”
Joseph dit à son père: « Ce sont mes fils, que Dieu m'a donnés ici. » Il dit: « Amène-les-moi, je te prie, et je les bénirai. »
10 Basi macho ya Israeli yalikuwa hayaoni vizuri kwa sababu ya uzee, naye aliona kwa shida. Kwa hiyo Yosefu akawaleta wanawe karibu na baba yake, Israeli akawabusu na akawakumbatia.
Or les yeux d'Israël s'étaient obscurcis à cause de l'âge, de sorte qu'il ne voyait pas bien. Joseph les fit approcher de lui; il les embrassa et les serra dans ses bras.
11 Israeli akamwambia Yosefu, “Kamwe sikutazamia kuuona uso wako tena, lakini sasa Mungu ameniruhusu kuwaona watoto wako pia.”
Israël dit à Joseph: « Je ne pensais pas voir ton visage, et voici que Dieu m'a permis de voir aussi ta descendance. »
12 Ndipo Yosefu akawaondoa wanawe magotini mwa Israeli naye akasujudu hadi nchi.
Joseph les fit sortir d'entre ses genoux, et il se prosterna, le visage tourné vers la terre.
13 Yosefu akachukua wale wana wawili, Efraimu kwenye mkono wake wa kuume akimwelekeza kwenye mkono wa kushoto wa Israeli, na Manase katika mkono wake wa kushoto akimwelekeza kwenye mkono wa kuume wa Israeli, akawaleta karibu na babu yao.
Joseph les prit tous deux, Éphraïm dans sa main droite vers la main gauche d`Israël, et Manassé dans sa main gauche vers la main droite d`Israël, et il les fit approcher de lui.
14 Lakini Israeli akaupeleka mkono wake wa kuume, akauweka juu ya kichwa cha Efraimu, ingawa alikuwa ndiye mdogo, na mkono wake wa kushoto akaukatisha, akauweka juu ya kichwa cha Manase, ingawa Manase alikuwa ndiye mzaliwa wa kwanza.
Israël étendit sa main droite et la posa sur la tête d'Ephraïm, qui était le plus jeune, et sa main gauche sur la tête de Manassé, guidant sciemment ses mains, car Manassé était le premier-né.
15 Ndipo akambariki Yosefu akisema, “Mungu ambaye baba zangu Abrahamu na Isaki walimtii, Mungu ambaye amekuwa mchungaji wa maisha yangu yote mpaka leo hii,
Il bénit Joseph, et dit, « Le Dieu devant lequel mes pères Abraham et Isaac ont marché, le Dieu qui m'a nourri toute ma vie jusqu'à aujourd'hui,
16 Malaika ambaye aliniokoa kutoka madhara yote, yeye na awabariki vijana hawa. Na waitwe kwa jina langu na kwa majina ya baba zangu Abrahamu na Isaki, wao na waongezeke kwa wingi katika dunia.”
l'ange qui m'a racheté de tout mal, bénis les gars, et que mon nom soit nommé sur eux, et le nom de mes pères, Abraham et Isaac. Qu'ils deviennent une multitude sur la terre. »
17 Yosefu alipoona baba yake akiweka mkono wa kuume juu ya kichwa cha Efraimu, hakupendezwa, kwa hiyo akauchukua mkono wa baba yake kutoka kichwa cha Efraimu na kuuweka juu ya kichwa cha Manase.
Lorsque Joseph vit que son père posait sa main droite sur la tête d'Ephraïm, cela lui déplut. Il leva la main de son père, pour la faire passer de la tête d'Ephraïm à celle de Manassé.
18 Yosefu akamwambia, “Hapana, baba yangu, huyu ndiye mzaliwa wa kwanza; uweke mkono wako wa kuume juu ya kichwa chake.”
Joseph dit à son père: « Pas ainsi, mon père, car c'est le premier-né. Pose ta main droite sur sa tête. »
19 Lakini baba yake akakataa, akasema, “Ninajua, mwanangu, ninajua. Yeye pia atakuwa taifa, naye pia atakuwa mkuu. Hata hivyo, ndugu yake mdogo atakuwa mkuu kuliko yeye, nao wazao wake watakuwa kundi la mataifa.”
Son père refusa, et dit: « Je le sais, mon fils, je le sais. Lui aussi deviendra un peuple, et lui aussi sera grand. Mais son jeune frère sera plus grand que lui, et sa descendance deviendra une multitude de nations. »
20 Akawabarikia siku ile na kusema, “Kwa jina lenu Israeli watatamka baraka hii: ‘Mungu na awafanye kama Efraimu na Manase.’” Kwa hiyo akamtanguliza Efraimu mbele ya Manase.
Il les bénit ce jour-là, en disant: « Israël bénira en vous, en disant: 'Que Dieu vous fasse comme Ephraïm et comme Manassé'" Il plaça Ephraïm devant Manassé.
21 Ndipo Israeli akamwambia Yosefu, “Mimi ninakaribia kufa, lakini Mungu atakuwa pamoja nanyi, na atawarudisha katika nchi ya baba zenu.
Israël dit à Joseph: « Voici, je meurs, mais Dieu sera avec toi, et il te ramènera dans le pays de tes pères.
22 Kwako wewe, kama aliye juu ya ndugu zako, ninakupa sehemu moja zaidi ya ndugu zako, lile eneo nililoteka kwa Waamori kwa upanga wangu na upinde wangu.”
De plus, je t'ai donné une part au-dessus de tes frères, que j'ai arrachée de la main de l'Amoréen avec mon épée et avec mon arc. »

< Mwanzo 48 >