< Mwanzo 48 >

1 Baada ya muda Yosefu akaambiwa kwamba, “Baba yako ni mgonjwa.” Kwa hiyo akawachukua wanawe wawili Manase na Efraimu, pamoja naye.
След това, известиха на Иосифа: Ето, баща ти е болен. и той поведе със себе си двата си сина, Манасия и Ефрема, да отидат при него.
2 Yakobo alipoambiwa, “Mwanao Yosefu amekujia kukuona,” Israeli akakusanya nguvu zake, akaketi kitandani.
И известиха на Якова, казвайки: Ето, син ти Иосиф иде при тебе. Тогава Израил събра силите си и седна на леглото.
3 Yakobo akamwambia Yosefu, “Mungu Mwenyezi alinitokea huko Luzu katika nchi ya Kanaani, huko akanibariki,
И Яков каза на Иосифа: Бог Всемогъщи ми се яви в Луз, в Ханаанската земя, и благослови ме, като ми каза:
4 naye akaniambia, ‘Nitakufanya ustawi na kuongezeka hesabu yako, nitakufanya kuwa jamii ya mataifa, nami nitakupa nchi hii uimiliki milele wewe na wazao wako baada yako.’
Ето, Аз ще те наплодя, ще те размножа, и ще направя да произлязат много народи от теб: и ще дам тая земя на потомството ти след теб за всегдашно притежание.
5 “Sasa basi, wanao wawili waliozaliwa kwako huku Misri kabla sijaja hapa kwako watahesabiwa kuwa ni wangu; Efraimu na Manase watakuwa wangu, kama vile Reubeni na Simeoni walivyo wangu.
И сега, двата ти сина, които ти се родиха в Египетската земя, преди да дойда аз при тебе в Египет, са мои; Ефрем и Манасия ще бъдат мои също, както Рувим и Симеон.
6 Lakini watoto utakaowazaa baada yao watakuwa wako. Katika nchi watakayoirithi, watatambuliwa kwa jina la ndugu zao.
А чадата, които родиш подир тях, ще бъдат твои, а колкото за наследството си, ще се наричат с името на тия свои братя.
7 Nilipokuwa ninarudi kutoka Padani, katika huzuni yangu Raheli alifariki katika nchi ya Kanaani tulipokuwa tungali tukisafiri, tukiwa karibu kufika Efrathi. Kwa hiyo nilimzika huko, kando ya njia iendayo Efrathi” (yaani Bethlehemu).
А когато се връщах от Падан, умря ми Рахил на пътя на Ханаанската земя, като оставаше едно малко разстояние да стигнем до Ефрата; и погребах я там, край пътя за Ефрата, (който е Витлеем).
8 Wakati Israeli alipowaona wana wa Yosefu, akauliza, “Hawa ni nani?”
И като съгледа Иосифовите синове, рече Израил: Кои са тия?
9 Yosefu akamjibu baba yake, “Hawa ni wana ambao Mungu amenipa nikiwa huku.” Ndipo Israeli akasema, “Walete kwangu ili niwabariki.”
А Иосиф каза на баща си: Тия са синовете, които Бог ми даде тука. А той рече: Моля, доведи ги при мене, за да ги благословя.
10 Basi macho ya Israeli yalikuwa hayaoni vizuri kwa sababu ya uzee, naye aliona kwa shida. Kwa hiyo Yosefu akawaleta wanawe karibu na baba yake, Israeli akawabusu na akawakumbatia.
А очите на Израиля бяха помрачени от старост, та не можеше да вижда. И тъй, Иосиф ги приближи при него; а той ги целуна и ги прегърна.
11 Israeli akamwambia Yosefu, “Kamwe sikutazamia kuuona uso wako tena, lakini sasa Mungu ameniruhusu kuwaona watoto wako pia.”
И рече Израил на Иосифа: Не се надявах да видя лицето ти; но, ето, Бог ми показа и потомството ти.
12 Ndipo Yosefu akawaondoa wanawe magotini mwa Israeli naye akasujudu hadi nchi.
И Иосиф, като ги махна от между колената си, поклони се с лицето до земята.
13 Yosefu akachukua wale wana wawili, Efraimu kwenye mkono wake wa kuume akimwelekeza kwenye mkono wa kushoto wa Israeli, na Manase katika mkono wake wa kushoto akimwelekeza kwenye mkono wa kuume wa Israeli, akawaleta karibu na babu yao.
После Иосиф ги взе двамата, Ефрема с дясната си ръка към лявата на Израил, а Манасия с лявата си ръка към дясната на Израил, та ги доведе при него.
14 Lakini Israeli akaupeleka mkono wake wa kuume, akauweka juu ya kichwa cha Efraimu, ingawa alikuwa ndiye mdogo, na mkono wake wa kushoto akaukatisha, akauweka juu ya kichwa cha Manase, ingawa Manase alikuwa ndiye mzaliwa wa kwanza.
А Израил простря дясната си ръка и я възложи на главата на Ефрема, който беше по-младият, а лявата ръка на Манасиевата глава, като нарочно кръстоса ръцете си; (защото Манасия беше първородният).
15 Ndipo akambariki Yosefu akisema, “Mungu ambaye baba zangu Abrahamu na Isaki walimtii, Mungu ambaye amekuwa mchungaji wa maisha yangu yote mpaka leo hii,
И като благослови Иосифа рече: Бог, пред Когото ходеха бащите ми Авраам и Исаак, Бог, Който ме е пасъл през целия ми живот до тоя ден;
16 Malaika ambaye aliniokoa kutoka madhara yote, yeye na awabariki vijana hawa. Na waitwe kwa jina langu na kwa majina ya baba zangu Abrahamu na Isaki, wao na waongezeke kwa wingi katika dunia.”
ангелът, който ме избавя от всяко зло, нека благослови момчетата; и нека се наричат с моето име и с името на бащите ми Авраама и Исаака; и нека нарастат в множество всред земята.
17 Yosefu alipoona baba yake akiweka mkono wa kuume juu ya kichwa cha Efraimu, hakupendezwa, kwa hiyo akauchukua mkono wa baba yake kutoka kichwa cha Efraimu na kuuweka juu ya kichwa cha Manase.
Но като видя Иосиф, че баща му възложи дясната си ръка на Ефремовата глава, не одобри; и дигна ръката на баща си, за да я премести от Ефремовата глава на Манасиевата глава.
18 Yosefu akamwambia, “Hapana, baba yangu, huyu ndiye mzaliwa wa kwanza; uweke mkono wako wa kuume juu ya kichwa chake.”
И Иосиф рече на баща си: Не така, тате, защото ето първородният, възложи дясната си ръка на неговата глава.
19 Lakini baba yake akakataa, akasema, “Ninajua, mwanangu, ninajua. Yeye pia atakuwa taifa, naye pia atakuwa mkuu. Hata hivyo, ndugu yake mdogo atakuwa mkuu kuliko yeye, nao wazao wake watakuwa kundi la mataifa.”
Но баща му отказа, като рече: Зная синко, зная; и той ще стане племе; и той ще бъде велик; но по-младият му брат ще бъде по-голям от него, и потомството му ще стане множество народи.
20 Akawabarikia siku ile na kusema, “Kwa jina lenu Israeli watatamka baraka hii: ‘Mungu na awafanye kama Efraimu na Manase.’” Kwa hiyo akamtanguliza Efraimu mbele ya Manase.
И тъй, в същия ден ги благослови, казвайки: С твоето име Израил ще благославя, като казва: Бог да те направи като Ефрема и като Манасия!- като постави Ефрема пред Манасия.
21 Ndipo Israeli akamwambia Yosefu, “Mimi ninakaribia kufa, lakini Mungu atakuwa pamoja nanyi, na atawarudisha katika nchi ya baba zenu.
След това Израил рече на Иосифа: Ето, аз умирам; но Бог ще бъде с вас, и ще ви върне пак в отечеството ви.
22 Kwako wewe, kama aliye juu ya ndugu zako, ninakupa sehemu moja zaidi ya ndugu zako, lile eneo nililoteka kwa Waamori kwa upanga wangu na upinde wangu.”
Впрочем, аз на тебе давам един дял повече отколкото на братята ти, който дял взех от ръцете на аморейците със сабята си и с лъка си.

< Mwanzo 48 >