< Mwanzo 47 >

1 Yosefu akaenda na kumwambia Farao, “Baba yangu na ndugu zangu wamekuja kutoka nchi ya Kanaani wakiwa na makundi yao ya kondoo, mbuzi na ngʼombe, pamoja na kila kitu walicho nacho, nao sasa wapo huko Gosheni.”
Et Joseph vint et fit savoir cela à Pharaon, et lui dit: Mon père et mes frères, avec leurs brebis et leurs bœufs, et tout ce qui est à eux, sont venus du pays de Canaan; et voici, ils sont dans le pays de Gossen.
2 Akachagua ndugu zake watano na kuwaonyesha kwa Farao.
Et il prit cinq hommes d'entre ses frères et les présenta à Pharaon.
3 Farao akawauliza hao ndugu zake, “Kazi yenu ni nini?” Wakamjibu, “Watumishi wako ni wachunga mifugo, kama vile baba zetu walivyokuwa.”
Et Pharaon dit à ses frères: Quel est votre métier? Et ils répondirent à Pharaon: Tes serviteurs sont bergers, comme l'ont été nos pères.
4 Pia wakamwambia Farao, “Tumekuja kukaa huku kwa muda mfupi, kwa sababu njaa ni kali huko Kanaani, na mifugo ya watumishi wako haina malisho. Kwa hiyo sasa, tafadhali uruhusu watumishi wako wakae huko Gosheni.”
Puis ils dirent à Pharaon: C'est pour séjourner dans le pays que nous sommes venus; car il n'y a plus de pâturage pour les troupeaux de tes serviteurs; car la famine est grande au pays de Canaan. Permets donc à tes serviteurs d'habiter au pays de Gossen.
5 Farao akamwambia Yosefu, “Baba yako na ndugu zako wamekuja kwako,
Et Pharaon parla ainsi à Joseph: Ton père et tes frères sont venus vers toi;
6 nayo nchi ya Misri ipo mbele yako, uwakalishe baba yako na ndugu zako katika sehemu iliyo bora kupita zote katika nchi. Na waishi Gosheni. Kama unamfahamu yeyote miongoni mwao mwenye uwezo maalum, waweke wawe wasimamizi wa mifugo yangu.”
Le pays d'Égypte est à ta disposition; fais habiter ton père et tes frères dans le meilleur endroit du pays; qu'ils demeurent dans le pays de Gossen. Et si tu connais qu'il y ait parmi eux des hommes capables, tu les établiras chefs de troupeaux sur ce qui m'appartient.
7 Ndipo Yosefu akamleta Yakobo baba yake na kumtambulisha mbele ya Farao. Baada ya Yakobo kumbariki Farao,
Alors Joseph amena Jacob son père, et le présenta à Pharaon. Et Jacob bénit Pharaon.
8 Farao akamuuliza, “Je una umri gani?”
Et Pharaon dit à Jacob: A combien s'élèvent les jours des années de ta vie?
9 Naye Yakobo akamwambia Farao, “Siku za miaka ya kusafiri kwangu ni miaka 130. Miaka yangu imekuwa michache na ya taabu, wala haikufikia miaka ya kusafiri ya baba zangu.”
Et Jacob répondit à Pharaon: Les jours des années de mes pèlerinages sont de cent trente ans; les jours des années de ma vie ont été courts et mauvais, et ils n'ont point atteint les jours des années de la vie de mes pères, du temps de leurs pèlerinages.
10 Kisha Yakobo akambariki Farao, naye akaondoka mbele ya uso wake.
Et Jacob bénit Pharaon, puis il sortit de devant Pharaon.
11 Ndipo Yosefu akawakalisha baba yake na ndugu zake katika nchi ya Misri na kuwapa milki katika sehemu bora sana ya nchi, wilaya ya Ramesesi, kama Farao alivyoelekeza.
Et Joseph assigna une demeure à son père et à ses frères, et il leur donna une possession au pays d'Égypte, dans le meilleur endroit du pays, dans le pays de Ramsès, comme l'avait ordonné Pharaon.
12 Pia Yosefu akampa baba yake, na ndugu zake na wote wa nyumbani mwa baba yake vyakula, kwa kulingana na hesabu ya watoto wao.
Et Joseph fournit de pain son père, ses frères, et toute la maison de son père, selon le nombre des enfants.
13 Hata hivyo, hapakuwepo chakula katika sehemu yote kwa kuwa njaa ilikuwa kali sana; Misri na Kanaani zote zikaharibiwa kwa sababu ya njaa.
Or, il n'y avait point de pain dans tout le pays, car la famine était très grande; et le pays d'Égypte et le pays de Canaan étaient épuisés par la famine.
14 Yosefu akakusanya fedha zote zilizopatikana kutoka mauzo ya nafaka huko Misri na Kanaani, akazileta kwenye jumba la kifalme la Farao.
Et Joseph amassa tout l'argent qui se trouvait dans le pays d'Égypte et dans le pays de Canaan, en échange du blé qu'on achetait; et Joseph fit entrer cet argent dans la maison de Pharaon.
15 Fedha za watu wa Misri na Kanaani zilipokwisha, Wamisri wote wakamjia Yosefu na kumwambia, “Tupatie chakula. Kwa nini tufe mbele ya macho yako? Fedha zetu zimekwisha.”
Et quand l'argent manqua au pays d'Égypte et au pays de Canaan, tous les Égyptiens vinrent à Joseph, en disant: Donne-nous du pain; et pourquoi mourrions-nous devant toi, parce qu'il n'y a plus d'argent?
16 Yosefu akawaambia, “Basi leteni mifugo yenu, nitawauzia chakula kwa kubadilisha na mifugo yenu, kwa kuwa fedha zenu zimekwisha.”
Et Joseph répondit: Donnez votre bétail, et je vous donnerai du pain en échange de votre bétail, s'il n'y a plus d'argent.
17 Kwa hiyo wakaleta mifugo yao kwa Yosefu, naye akawapa chakula kwa kubadilishana na farasi zao, kondoo na mbuzi zao, ngʼombe na punda zao. Katika mwaka huo wote Yosefu akawapa chakula kwa kubadilishana na mifugo yao yote.
Alors ils amenèrent leur bétail à Joseph, et Joseph leur donna du pain, en échange des chevaux, des troupeaux de brebis, des troupeaux de bœufs et des ânes. Il leur fournit du pain en échange de tous leurs troupeaux cette année-là.
18 Mwaka ule ulipokwisha, wakamjia mwaka uliofuata na kumwambia, “Hatuwezi kuficha ukweli mbele za bwana wetu kwamba, kwa kuwa fedha zetu zimekwisha na wanyama wetu ni mali yako, sasa hakuna chochote kilichosalia kwa ajili ya bwana wetu isipokuwa miili yetu na ardhi yetu.
Cette année écoulée, ils revinrent l'année suivante, et lui dirent: Nous ne cacherons point à mon seigneur que l'argent est épuisé, et que les troupeaux de bétail ont passé à mon seigneur; il ne reste rien devant mon seigneur que nos corps et nos terres.
19 Kwa nini tuangamie mbele ya macho yako, sisi pamoja na nchi yetu? Utununue sisi pamoja na ardhi yetu ili kubadilishana kwa chakula. Nasi pamoja na nchi yetu tutakuwa watumwa wa Farao. Tupe sisi mbegu ili tuweze kuishi wala tusife, nchi yetu isije ikawa ukiwa.”
Pourquoi péririons-nous sous tes yeux, nous et nos terres? Achète-nous, nous et nos terres, pour du pain, et nous serons, avec nos terres, esclaves de Pharaon. Et donne-nous de quoi semer, afin que nous vivions et ne mourions pas, et que le sol ne soit point désolé.
20 Kwa hiyo Yosefu akamnunulia Farao nchi yote ya Misri. Wamisri, mmoja baada ya mwingine, waliuza mashamba yao, kwa sababu njaa ilikuwa kali sana kwao. Nchi ikawa mali ya Farao,
Et Joseph acquit tout le sol de l'Égypte à Pharaon; car les Égyptiens vendirent chacun leur champ, parce que la famine les y força; et la terre fut à Pharaon.
21 naye Yosefu akawafanya watu watumike kama watumwa, kuanzia upande mmoja wa Misri hadi upande mwingine.
Quant au peuple, il le fit passer dans les villes, depuis une extrémité du territoire de l'Égypte jusqu'à l'autre.
22 Hata hivyo, hakununua nchi ya makuhani, kwa sababu walikuwa wanapata mgawo wao wa kawaida kutoka kwa Farao, nao walikuwa na chakula cha kuwatosha kutokana na mgawo waliopewa na Farao. Hii ndiyo sababu hawakuuza ardhi yao.
Les terres des prêtres furent les seules qu'il n'acquit point; car les prêtres recevaient de Pharaon une portion fixée, et ils mangeaient la portion que Pharaon leur avait donnée. C'est pourquoi, ils ne vendirent point leurs terres.
23 Yosefu akawaambia watu, “Kwa vile nimewanunua ninyi pamoja na nchi yenu leo kuwa mali ya Farao, hapa kuna mbegu kwa ajili yenu ili mweze kuziotesha.
Et Joseph dit au peuple: Je vous ai acquis aujourd'hui, vous et vos terres, à Pharaon. Voici pour vous de la semence, afin que vous ensemenciez le sol.
24 Lakini wakati mazao yatakapokuwa tayari, mpeni Farao sehemu ya tano. Sehemu hizo nne zitakazobaki mtaziweka kama mbegu kwa ajili ya mashamba na kwa ajili ya chakula chenu wenyewe na cha watu wa nyumbani mwenu na watoto wenu.”
Et au temps des récoltes, vous donnerez le cinquième à Pharaon, et les quatre autres parties seront à vous, pour semer les champs, et pour votre nourriture, et pour celle des gens qui sont dans vos maisons, et pour la nourriture de vos petits enfants.
25 Wakamwambia, “Umeokoa maisha yetu. Basi na tupate kibali mbele ya macho ya bwana wetu; tutakuwa watumwa wa Farao.”
Et ils dirent: Tu nous as sauvé la vie! Que nous trouvions grâce aux yeux de mon seigneur, et nous serons esclaves de Pharaon.
26 Basi Yosefu akaiweka iwe sheria kuhusu nchi ya Misri, ambayo inatumika mpaka leo, kwamba, sehemu ya tano ya mazao ni mali ya Farao. Ni nchi ya makuhani tu ambayo haikuwa ya Farao.
Et Joseph en fit une loi, qui dure jusqu'à ce jour, sur les terres d'Égypte: Le cinquième à Pharaon. Il n'y eut que les terres des prêtres qui ne furent point à Pharaon.
27 Basi Waisraeli wakaishi Misri katika nchi ya Gosheni. Wakapata mali huko wakastawi na kuongezeka kwa wingi sana.
Israël habita donc au pays d'Égypte, au pays de Gossen; et ils y acquirent des propriétés, et ils s'accrurent, et multiplièrent beaucoup.
28 Yakobo akaishi Misri miaka kumi na saba, nayo miaka ya maisha yake ilikuwa 147.
Et Jacob vécut au pays d'Égypte dix-sept ans. Et les jours de Jacob, les années de sa vie, furent de cent quarante-sept ans.
29 Wakati ulipokaribia wa Israeli kufa, akamwita mwanawe Yosefu na kumwambia, “Kama nimepata kibali machoni pake, weka mkono wako chini ya paja langu na uniahidi kuwa utanifanyia fadhili na uaminifu. Usinizike Misri,
Et quand le jour de la mort d'Israël approcha, il appela son fils Joseph, et lui dit: Si j'ai trouvé grâce à tes y eux, mets, je te prie, ta main sous ma cuisse, et use envers moi de bonté et de fidélité: je te prie, ne m'enterre point en Égypte.
30 lakini nitakapopumzika na baba zangu, unichukue kutoka Misri, ukanizike walipozikwa.” Yosefu akamwambia, “Nitafanya kama unavyosema.”
Quand je serai couché avec mes pères, emporte-moi d'Égypte, et enterre-moi dans leur tombeau. Et il répondit: Je ferai selon ta parole.
31 Akamwambia, “Niapie.” Ndipo Yosefu akamwapia, naye Israeli akaabudu, akiwa ameegemea juu ya kichwa cha fimbo yake.
Il dit: Jure-le-moi. Et il le lui jura. Et Israël se prosterna sur le chevet du lit.

< Mwanzo 47 >