< Mwanzo 47 >
1 Yosefu akaenda na kumwambia Farao, “Baba yangu na ndugu zangu wamekuja kutoka nchi ya Kanaani wakiwa na makundi yao ya kondoo, mbuzi na ngʼombe, pamoja na kila kitu walicho nacho, nao sasa wapo huko Gosheni.”
And Joseph came and told Pharaoh and said, My father and my brethren, and their sheep and their cattle, and all that they have, are come out of the land of Canaan; and behold, they are in the land of Goshen.
2 Akachagua ndugu zake watano na kuwaonyesha kwa Farao.
And he took from the whole number of his brethren, five men, and set them before Pharaoh.
3 Farao akawauliza hao ndugu zake, “Kazi yenu ni nini?” Wakamjibu, “Watumishi wako ni wachunga mifugo, kama vile baba zetu walivyokuwa.”
And Pharaoh said to his brethren, What is your occupation? And they said to Pharaoh, Thy servants are shepherds, both we and our fathers.
4 Pia wakamwambia Farao, “Tumekuja kukaa huku kwa muda mfupi, kwa sababu njaa ni kali huko Kanaani, na mifugo ya watumishi wako haina malisho. Kwa hiyo sasa, tafadhali uruhusu watumishi wako wakae huko Gosheni.”
And they said to Pharaoh, To sojourn in the land are we come; for there is no pasture for the sheep that thy servants have, for the famine is grievous in the land of Canaan; and now, we pray thee, let thy servants dwell in the land of Goshen.
5 Farao akamwambia Yosefu, “Baba yako na ndugu zako wamekuja kwako,
And Pharaoh spoke to Joseph, saying, Thy father and thy brethren are come to thee.
6 nayo nchi ya Misri ipo mbele yako, uwakalishe baba yako na ndugu zako katika sehemu iliyo bora kupita zote katika nchi. Na waishi Gosheni. Kama unamfahamu yeyote miongoni mwao mwenye uwezo maalum, waweke wawe wasimamizi wa mifugo yangu.”
The land of Egypt is before thee; in the best of the land settle thy father and thy brethren: let them dwell in the land of Goshen. And if thou knowest men of activity among them, then set them as overseers of cattle over what I have.
7 Ndipo Yosefu akamleta Yakobo baba yake na kumtambulisha mbele ya Farao. Baada ya Yakobo kumbariki Farao,
And Joseph brought Jacob his father, and set him before Pharaoh. And Jacob blessed Pharaoh.
8 Farao akamuuliza, “Je una umri gani?”
And Pharaoh said to Jacob, How many are the days of the years of thy life?
9 Naye Yakobo akamwambia Farao, “Siku za miaka ya kusafiri kwangu ni miaka 130. Miaka yangu imekuwa michache na ya taabu, wala haikufikia miaka ya kusafiri ya baba zangu.”
And Jacob said to Pharaoh, The days of the years of my sojourning are a hundred and thirty years. Few and evil have been the days of the years of my life, and they do not attain to the days of the years of the life of my fathers, in the days of their sojourning.
10 Kisha Yakobo akambariki Farao, naye akaondoka mbele ya uso wake.
And Jacob blessed Pharaoh, and went out from Pharaoh.
11 Ndipo Yosefu akawakalisha baba yake na ndugu zake katika nchi ya Misri na kuwapa milki katika sehemu bora sana ya nchi, wilaya ya Ramesesi, kama Farao alivyoelekeza.
And Joseph settled his father and his brethren, and gave them a possession in the land of Egypt, in the best of the land, in the land of Rameses, as Pharaoh had commanded.
12 Pia Yosefu akampa baba yake, na ndugu zake na wote wa nyumbani mwa baba yake vyakula, kwa kulingana na hesabu ya watoto wao.
And Joseph maintained his father, and his brethren, and all his father's household, with bread, according to the number of the little ones.
13 Hata hivyo, hapakuwepo chakula katika sehemu yote kwa kuwa njaa ilikuwa kali sana; Misri na Kanaani zote zikaharibiwa kwa sababu ya njaa.
And there was no bread in all the land; for the famine was very grievous; and the land of Egypt and the land of Canaan were exhausted through the famine.
14 Yosefu akakusanya fedha zote zilizopatikana kutoka mauzo ya nafaka huko Misri na Kanaani, akazileta kwenye jumba la kifalme la Farao.
And Joseph gathered up all the money that was found in the land of Egypt, and in the land of Canaan, for the grain which they bought; and Joseph brought the money into Pharaoh's house.
15 Fedha za watu wa Misri na Kanaani zilipokwisha, Wamisri wote wakamjia Yosefu na kumwambia, “Tupatie chakula. Kwa nini tufe mbele ya macho yako? Fedha zetu zimekwisha.”
And when money came to an end in the land of Egypt and in the land of Canaan, all the Egyptians came to Joseph, saying, Give us bread! for why should we die before thee? for [our] money is all gone.
16 Yosefu akawaambia, “Basi leteni mifugo yenu, nitawauzia chakula kwa kubadilisha na mifugo yenu, kwa kuwa fedha zenu zimekwisha.”
And Joseph said, Give your cattle, and I will give you for your cattle, if [your] money be all gone.
17 Kwa hiyo wakaleta mifugo yao kwa Yosefu, naye akawapa chakula kwa kubadilishana na farasi zao, kondoo na mbuzi zao, ngʼombe na punda zao. Katika mwaka huo wote Yosefu akawapa chakula kwa kubadilishana na mifugo yao yote.
And they brought their cattle to Joseph; and Joseph gave them bread for horses, and for flocks of sheep, and for herds of cattle, and for asses; and he fed them with bread for all their cattle that year.
18 Mwaka ule ulipokwisha, wakamjia mwaka uliofuata na kumwambia, “Hatuwezi kuficha ukweli mbele za bwana wetu kwamba, kwa kuwa fedha zetu zimekwisha na wanyama wetu ni mali yako, sasa hakuna chochote kilichosalia kwa ajili ya bwana wetu isipokuwa miili yetu na ardhi yetu.
And that year ended; and they came to him the second year, and said to him, We will not hide [it] from my lord that since [our] money is come to an end, and the herds of cattle are in the possession of my lord, nothing is left before my lord but our bodies and our land.
19 Kwa nini tuangamie mbele ya macho yako, sisi pamoja na nchi yetu? Utununue sisi pamoja na ardhi yetu ili kubadilishana kwa chakula. Nasi pamoja na nchi yetu tutakuwa watumwa wa Farao. Tupe sisi mbegu ili tuweze kuishi wala tusife, nchi yetu isije ikawa ukiwa.”
Why should we die before thine eyes, both we and our land? Buy us and our land for bread, and we and our land will be bondmen to Pharaoh; and give seed, that we may live, and not die, and that the land be not desolate.
20 Kwa hiyo Yosefu akamnunulia Farao nchi yote ya Misri. Wamisri, mmoja baada ya mwingine, waliuza mashamba yao, kwa sababu njaa ilikuwa kali sana kwao. Nchi ikawa mali ya Farao,
And Joseph bought all the soil of Egypt for Pharaoh; for the Egyptians sold every man his field, because the famine prevailed over them; and the land became Pharaoh's.
21 naye Yosefu akawafanya watu watumike kama watumwa, kuanzia upande mmoja wa Misri hadi upande mwingine.
And as for the people, he removed them into the cities, from [one] end of the borders of Egypt even to the [other] end of it.
22 Hata hivyo, hakununua nchi ya makuhani, kwa sababu walikuwa wanapata mgawo wao wa kawaida kutoka kwa Farao, nao walikuwa na chakula cha kuwatosha kutokana na mgawo waliopewa na Farao. Hii ndiyo sababu hawakuuza ardhi yao.
Only the land of the priests he did not buy; for the priests had an assigned portion from Pharaoh, and ate their assigned portion which Pharaoh had given them; so they did not sell their land.
23 Yosefu akawaambia watu, “Kwa vile nimewanunua ninyi pamoja na nchi yenu leo kuwa mali ya Farao, hapa kuna mbegu kwa ajili yenu ili mweze kuziotesha.
And Joseph said to the people, Behold, I have bought you this day and your land for Pharaoh: lo, here is seed for you, and sow the land.
24 Lakini wakati mazao yatakapokuwa tayari, mpeni Farao sehemu ya tano. Sehemu hizo nne zitakazobaki mtaziweka kama mbegu kwa ajili ya mashamba na kwa ajili ya chakula chenu wenyewe na cha watu wa nyumbani mwenu na watoto wenu.”
And it shall come to pass in the increase that ye shall give the fifth to Pharaoh, and the four parts shall be your own, for seed of the field, and for your food, and for them of your households, and for food for your little ones.
25 Wakamwambia, “Umeokoa maisha yetu. Basi na tupate kibali mbele ya macho ya bwana wetu; tutakuwa watumwa wa Farao.”
And they said, Thou hast saved us alive. Let us find favour in the eyes of my lord, and we will be Pharaoh's bondmen.
26 Basi Yosefu akaiweka iwe sheria kuhusu nchi ya Misri, ambayo inatumika mpaka leo, kwamba, sehemu ya tano ya mazao ni mali ya Farao. Ni nchi ya makuhani tu ambayo haikuwa ya Farao.
And Joseph made it a law over the land of Egypt to this day, [that] the fifth should be for Pharaoh, except the land of the priests: theirs alone did not become Pharaoh's.
27 Basi Waisraeli wakaishi Misri katika nchi ya Gosheni. Wakapata mali huko wakastawi na kuongezeka kwa wingi sana.
And Israel dwelt in the land of Egypt, in the land of Goshen; and they had possessions in it, and were fruitful and multiplied exceedingly.
28 Yakobo akaishi Misri miaka kumi na saba, nayo miaka ya maisha yake ilikuwa 147.
And Jacob lived in the land of Egypt seventeen years; and the days of Jacob, the years of his life, were a hundred and forty-seven years.
29 Wakati ulipokaribia wa Israeli kufa, akamwita mwanawe Yosefu na kumwambia, “Kama nimepata kibali machoni pake, weka mkono wako chini ya paja langu na uniahidi kuwa utanifanyia fadhili na uaminifu. Usinizike Misri,
And the days of Israel approached that he should die. And he called his son Joseph, and said to him, If now I have found favour in thine eyes, put, I pray thee, thy hand under my thigh, and deal kindly and truly with me: bury me not, I pray thee, in Egypt;
30 lakini nitakapopumzika na baba zangu, unichukue kutoka Misri, ukanizike walipozikwa.” Yosefu akamwambia, “Nitafanya kama unavyosema.”
but when I shall lie with my fathers, thou shalt carry me out of Egypt, and bury me in their sepulchre. And he said, I will do according to thy word.
31 Akamwambia, “Niapie.” Ndipo Yosefu akamwapia, naye Israeli akaabudu, akiwa ameegemea juu ya kichwa cha fimbo yake.
And he said, Swear to me; and he swore to him. And Israel worshipped on the bed's head.